Ukomo wa umri kugombea uraisi na ubunge!!! Katiba haijasema chochote.

Ukomo wa umri kugombea uraisi na ubunge!!! Katiba haijasema chochote.

Insabhunsa Gusa

Senior Member
Joined
May 13, 2011
Posts
109
Reaction score
88

Wana JF,

Kama Raisi, Waziri, Mbunge nk ni watumishi wa umma. Kwa nini rasimu ya KATIBA mpya haijatamka umri wa ukomo kugombea nyadhifa hizo, ilhali imetamka umri kianzio wa miaka 40 kwa uraisi.

Nijuavyo, umri wa ukomo wa utumishi wa umma ni miaka 55 kwa hiari na miaka 60 kwa mujibu wa sheria. Nilidhani Raisi kama mtumishi wa umma, hatakiwi kuwa madarakani akiwa na umri zaidi ya miaka 60!!! Napendekeza, umri wa ukomo kugombea Uraisi, ubunge, uwaziri, ukatibu mkuu nk nk nk uwe miaka 50, ili atumikiapo vipindi/awamu mbili awe na miaka 60, tayari kwa KUSTAAFU!!!!!! Yasije yakatukuta ya BABU Mugabe, tusilaumu tu pengine Katiba ya Zimbabwe inaruhusu umri wowote.
 
Navyojua mie, rais atakua madarakani awamu mbili tu bila kujali umri wake. Chamuhimu awe na miaka 40 au zaid wakati wa kugombea. Na kwa mbunge atakua madarakan awamu 3 tu
 
Ukomo wa Umri ni jambo mhimu kwa viongozi wa Serikali,,napendekeza ukomo wa Rais, Mbunge na Waziri iwe miaka 65 tu na si zaidi ya hapo..Maana zaidi ya miaka 65 mtu hubaki na busara tu kama alijariwa na mwenyezi lakini kikazi huwa amechoka na hawezi tena mudu mikiki mizito.
 
Back
Top Bottom