Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wanaume waliokwepa kujiunga na programu ya Jeshi na kwenda klabu kula bata huko Ukraine wamekutana nacho baada ya Jeshi la Nchi hiyo kuanzisha msako wa kuwakamata Wanaume wote waliokwepa programu hiyo kwenye kumbi za starehe, matamasha ya Muziki, sehemu za manunuzi, migahawa na maeneo ya Umma.
Video ya Mwanaume mmoja aliyehudhuria mapema wikiendi hii kwenye tamasha la bendi ya Muziki ya Okean Elzy katika Jumba la Michezo la Kyiv imesambaa mitandaoni ikionyesha akiwa anakamatwa na Maafisa watatu wa Polisi baada ya kukagua hati zake na kuonekana kuwa na kasoro.
Kitu ambacho inawezekana hukijui ni kwamba kulingana na Sheria za Ukraine, Wanaume wote wenye umri kati ya miaka 25 hadi 60 wanastahili kujiunga na programu maalum ya Jeshi na Wanaume wenye umri kati ya miaka 18 hadi 60 pia wamepigwa marufuku kuondoka Nchini humo hivi karibuni.
Soma Pia: Ukraine kapigwa na kitu kizito wapoteza zaidi ya wanajeshi 600
Hii ni Kutokana na uhaba mkubwa wa Wanajeshi ambao Taifa hilo linakabiliana nao wakati vita dhidi yake na Urusi vikipamba moto, Ukraine ilipunguza umri wake wa Watu kuhama kutoka miaka 27 hadi 25 na kufunga mwanya wa Watu kuondoka Nchini humo tangu April mwaka huu.
Takwimu za Huduma ya Walinzi wa Mipakani Nchini humo iliripoti mwezi April kwamba takribani Wanaume 30 walifariki wakijaribu kukimbia Nchi hiyo tangu kuanza kwa vita, mara nyingi wamekufa kwa kuzama walipokuwa wakijaribu kuogelea kwenye mito yenye baridi kali.
Video ya Mwanaume mmoja aliyehudhuria mapema wikiendi hii kwenye tamasha la bendi ya Muziki ya Okean Elzy katika Jumba la Michezo la Kyiv imesambaa mitandaoni ikionyesha akiwa anakamatwa na Maafisa watatu wa Polisi baada ya kukagua hati zake na kuonekana kuwa na kasoro.
Kitu ambacho inawezekana hukijui ni kwamba kulingana na Sheria za Ukraine, Wanaume wote wenye umri kati ya miaka 25 hadi 60 wanastahili kujiunga na programu maalum ya Jeshi na Wanaume wenye umri kati ya miaka 18 hadi 60 pia wamepigwa marufuku kuondoka Nchini humo hivi karibuni.
Soma Pia: Ukraine kapigwa na kitu kizito wapoteza zaidi ya wanajeshi 600
Hii ni Kutokana na uhaba mkubwa wa Wanajeshi ambao Taifa hilo linakabiliana nao wakati vita dhidi yake na Urusi vikipamba moto, Ukraine ilipunguza umri wake wa Watu kuhama kutoka miaka 27 hadi 25 na kufunga mwanya wa Watu kuondoka Nchini humo tangu April mwaka huu.
Takwimu za Huduma ya Walinzi wa Mipakani Nchini humo iliripoti mwezi April kwamba takribani Wanaume 30 walifariki wakijaribu kukimbia Nchi hiyo tangu kuanza kwa vita, mara nyingi wamekufa kwa kuzama walipokuwa wakijaribu kuogelea kwenye mito yenye baridi kali.