Ukuaji holela wa Deni la Taifa unatupa picha gani uko tuendako?

Ukuaji holela wa Deni la Taifa unatupa picha gani uko tuendako?

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2021
Posts
1,117
Reaction score
3,153
Unapokopa unawekeza katika miradi inayozalisha zaidi kuliko ile gharama ya kukopa(cost of borrowing), miradi mikubwa tuliyoiona ni ile iliyoanzishwa na Hayati Rais John Pombe Magufuli, miradi wa SGR, Bwawa la Umeme la Julius Nyerere, mradi wa mabasi ya mwendokasi, mradi wa barabara njia nane toka Dar hadi Morogoro, Ununuzi wa ndege Mpya 15, Ujenzi wa Meli za kisasa Ziwa Victoria,Z iwa Tanganyika, na kuhamisha makao makuu toka Dar hadi Dodoma, je, mikopo hiyo ndiyo inakwenda kwenye miradi hiyo muhimu kwa Taifa la Tanzania?,

Unapokopa na ukachezea au ukahamisha hela ya mkopo kwa kitu kisichokusudiwa unaingia kwenye utumwa wa madeni.

Debt is like any other trap, easy enough to get into, but hard enough to get out of.Some debts are fun when you are acquiring them, but none are fun when you set about retiring them, Wars in old times were made to get slaves, the modern implement of imposing slavery is debt.

Hofu ya wananchi ni kwamba, je ni kwa asilia ngapi pesa zinazokopwa zinaenda kufanya lengo lililokusudiwa pasipo kuwa na upotevu wa pesa yoyote.

Hii mikopo kama inafanya mambo ya maana angalau ila kama ni haya mambo yakununua V8 SUV, nimeona kamanda wa Burkina Faso amewekeza kwenye miradi yenye tija badala ya hayo ma V8 kanunua tractors na kupunguza mishahara ya mawaziri huku akiongeza mishahara ya wafanyakazi kwa 50%, ni kiongozi wakuigwa kwa tunakoelekea hili deni si rafiki hata kidogo na hili kwa % kubwa ni haya mambo ya uchaguzi.

Kwa ukubwa wa hii nchi tungewekeza kwenye kilimo, viwanda na kumalizia viporo vya miradi yenye tija, hayo mapikipiki na magari yanatuongezea madeni zaidi, tukumbuke kodi zetu ndizo zitakazolipa hayo madeni, mapato yanayokusanywa ndio yanalipa hilo deni, tukishindwa tujiandae shilingi yenu kuporomoka zaidi kwa sababu ya hilo deni, tuitizame Kenya deni la taifa linavyowaumiza.

Kwa sasa wanakopa deni lenye masharti nafuu kulipa deni lenye masharti magumu, deni likifikia above 45% ya GDP sio himilivu tena, hii ina athari mpaka kwa raia mitaani rejea majirani zetu.

Kwa nini tusiishi kama enzi za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Ali Hassan Mwinyi, katika awamu zao tulikuwa hatukopesheki walikuwa, tulikuwa hatufungamani na upande wowote na mikopo kwa wakomunist ilikuwa marufuku, tulipata mikopo midogo midogo tuu na grants from British government na Scandinavian countries, kwa mikopo hiyo midogo tuliweza kuishi bila madeni, shida ipo kwenye ulazima wa kukopa, ni kweli tunahitaji kukopa? Je, tungejinyima tungeweza kupata hela?

Alipoingia madarakani Hayati Rais John Pombe Magufuli, deni la taifa lilikuwa ni shilingi 35 trillion, kwa mujibu wa taarifa rasmi za bunge la Tanzania, deni likaendelea kukua na kufikia shilingi 60.7 trilioni mwezi April 2021 "Ongezeko la deni la Serikali katika Awamu ya tano ya CCM iliyoongozwa na Hayati Rais John Pombe Magufuli lilitokana na kupokelewa kwa fedha za mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, umeme na maji, na kulipa malimbikizo ya riba ya deni la nje"Awamu ya sita ilipoanza, April 2021 deni la Serikali lilikuwa sh 60.9 trilioni hadi kufikia machi 2024 deni la Serikali lilikuwa trilioni 91.7.

Shida ni nini? Je ni kushuka kwa thamani ya shilingi yetu ndio maana deni la Taifa linaongezeka au mikopo tunayoendelea kuchukua? rekodi ya kushuka kwa thamani ya shilingi yetu ipo kama ifuatavyo ;- Mwaka 2020. 1 Dollar -Tshs 2,314.8
Mwaka 2021. 1Dollar -Tshs 2,314.3
Mwaka 2022. 1Dollar- Tshs 2,326.1
Mwaka 2023 1Dollar- Tshs 2,419.6
Mwaka 2024 1Dollar- Tshs 2,463.5(Jan -June)

Sasa hivi June 2024 1Dollar -Tshs 2,627.5 sasa kwa nini hela yetu inashuka sana thamani? Je, Devaluation ya local currency pia ni mbinu ya uchumu ku-promote export na ku-discurrage import, tuna import mno.

Inatakiwe tuzalishe wenyewe na vingine tuanze kuexport nje ndio tutabalance trade, Dollar rate inakua determined na balance of trade i.e imports vs exports tanzania has imbalance terms of trade kila kitu tuna import na sie tuna export kidogo, Mama aongeze nguvu kwenye tourism inaweza kutuokoa.

-Nini lifanyike;-

Serikali ijikite kuongeza uzalishaji na mauzo ya nje, Serikali ivutie zaidi miradi ya uwekezaji, Serikali iongeze juhudi kwenye kuzalisha bidhaa ambazo tunaagiza nje ya nchi kama ngano, mafuta, maziwa, furnitures na bidhaa za mifugo.

Nimalizie kwa kusema kwamba hata mtaani mtu anapokuwa na madeni mengi unaona anavyoangaika, maisha yake hayawi sawa tena, anakuwa mtumwa, pengine vitu vyake nyumbani vitapigwa mnada, mkopo si mzuri, na hasa hii mikopo ya siku hizi yenye jina la "kausha damu" damu ni uhai, ikikauka maana yake ni kifo, kwa nini tufe na madeni!??

====

Pia soma: Prof. Mkumbo: Deni la Taifa lafikia Trilioni 92.7

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es salaam.
0755078854

-Bachelor of business administration in International business.
-Master of Leadership and Management.
Recent Publications;-
-Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.
 
Nimeambiwa issue ambayo haisemwi hapa ni kukopa..kukopa kwa maana kwamba ni lazima kukopa..ni moja ya mikataba wakati tunapewa uhuru wa bendera. Leo ukichaguliwa kuwa Rais ni lazima kukopa..siyo ombi.
 
Ukuaji wa deni la taifa nchini Tanzania unatupa picha ya changamoto za kifedha ambazo zinaweza kujitokeza katika miaka ijayo. Hali hii inahitaji kuzingatiwa kwa makini ili kuepuka athari mbaya kwa uchumi na maisha ya wananchi. Baadhi ya mambo ya kuzingatia ni:

1. Ongezeko la Malipo ya Madeni: Deni la taifa likiongezeka, serikali inalazimika kutenga sehemu kubwa ya mapato yake kwa ajili ya malipo ya riba na marejesho ya deni. Hii inaweza kupunguza uwezo wa serikali kutoa huduma za kijamii na kuboresha miundombinu.

2. Ukosefu wa Rasilimali za Ndani: Ili kukabiliana na deni la taifa, serikali inaweza kuongeza kodi au kukopa zaidi, ambayo inaweza kuathiri uchumi kwa kusababisha mzigo mkubwa kwa wananchi na biashara.

3. Hatari ya Kupungua kwa Uwezo wa Kukopa: Deni kubwa la taifa linaweza kusababisha nchi kushindwa kupata mikopo kwa masharti nafuu au hata kushuka kwa rating ya nchi, ambayo inaweza kuathiri vibaya uwezo wa nchi kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

4. Marekebisho ya Sera za Kifedha na Kiuchumi: Serikali inapaswa kuchukua hatua za makini katika marekebisho ya sera za kifedha na kiuchumi ili kuhakikisha kuwa deni la taifa linadhibitiwa na uchumi unakuwa imara. Hatua hizi zinaweza kujumuisha kudhibiti matumizi ya umma, kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, na kuboresha mazingira ya biashara.

Kwa hiyo, ni muhimu kwa serikali ya Tanzania kwa kupitia Bunge lake kuchukua hatua madhubuti za kifedha na kiuchumi ikiwemo pia kupokea mapendekezo ya wawakilishi wake juu ya namna bora ya kuweza kuendesha miradi mikubwa ya kimkakati nchini kwa mujibu wa sheria ili kudhibiti ukuaji wa deni la taifa na kuhakikisha maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi katika miaka ijayo.
 
Ukuaji wa deni la taifa nchini Tanzania unatupa picha ya changamoto za kifedha ambazo zinaweza kujitokeza katika miaka ijayo. Hali hii inahitaji kuzingatiwa kwa makini ili kuepuka athari mbaya kwa uchumi na maisha ya wananchi. Baadhi ya mambo ya kuzingatia ni:

1. Ongezeko la Malipo ya Madeni: Deni la taifa likiongezeka, serikali inalazimika kutenga sehemu kubwa ya mapato yake kwa ajili ya malipo ya riba na marejesho ya deni. Hii inaweza kupunguza uwezo wa serikali kutoa huduma za kijamii na kuboresha miundombinu.

2. Ukosefu wa Rasilimali za Ndani: Ili kukabiliana na deni la taifa, serikali inaweza kuongeza kodi au kukopa zaidi, ambayo inaweza kuathiri uchumi kwa kusababisha mzigo mkubwa kwa wananchi na biashara.

3. Hatari ya Kupungua kwa Uwezo wa Kukopa: Deni kubwa la taifa linaweza kusababisha nchi kushindwa kupata mikopo kwa masharti nafuu au hata kushuka kwa rating ya nchi, ambayo inaweza kuathiri vibaya uwezo wa nchi kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

4. Marekebisho ya Sera za Kifedha na Kiuchumi: Serikali inapaswa kuchukua hatua za makini katika marekebisho ya sera za kifedha na kiuchumi ili kuhakikisha kuwa deni la taifa linadhibitiwa na uchumi unakuwa imara. Hatua hizi zinaweza kujumuisha kudhibiti matumizi ya Mali ya umma, kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, na kuboresha mazingira ya biashara.

Kwa hiyo, ni muhimu kwa serikali ya Tanzania kwa kupitia Bunge lake kuchukua hatua madhubuti za kifedha na kiuchumi ikiwemo pia kupokea mapendekezo ya wawakilishi wake juu ya namna bora ya kuweza kuendesha miradi mikubwa ya kimkakati nchini kwa mujibu wa sheria ili kudhibiti ukuaji wa deni la taifa na kuhakikisha maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi katika miaka ijayo.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es salaam.
0755078854

-Bachelor of business administration in International

-Master of Leadership and Management.

Recent Publications;-
-Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.
 
Iache serikali na vipaumbele vyake...


Cc: Mahondaw
Hawa wanandoa sasa wameanza kukera, kama si kuzingua.

Hivi hamjui kwamba sie wananchi ndio tumeiajiri serikali ili ifanye kazi kwa niaba yetu?

Kuna vipaumbele gani muhimu vya serikali kuliko ustawi wa raia wake?

Tusipoinyoshea mkono serikali pale inapofanya makosa hasa ya kiutendaji, matokeo yake bila shaka ni wananchi kupigwa mnada mwishowe.
 
Hawa wanandoa sasa wameanza kukera, kama si kuzingua.

Hivi hamjui kwamba sie wananchi ndio tumeiajiri serikali ili ifanye kazi kwa niaba yetu?

Kuna vipaumbele gani muhimu vya serikali kuliko ustawi wa raia wake?

Tusipoinyoshea mkono serikali pale inapofanya makosa hasa ya kiutendaji, matokeo yake bila shaka ni wananchi kupigwa mnada mwishowe.
Tatizo serikali haisikilizi chochote zaidi ya kusifiwa ujinga na wachache...


Cc: Mahondaw
 
Mikopo ni asilimia 30 ya bajeti yetu. Pia marejesho ni asilimia 30. Tukiendelea kukopa Kuna siku bajeti yote itakua ni kulipa madeni tu. Kuna vitu vingesubiri tu. Hatuna hizo haraka kama itakua ni Kwa kukopa kopa. Kwenye scale zao wanaona ni himivu lakini je wanaona linakula asilimia ngapi ya budget?
Uhimivu wake unapimwa Kwa vinavyozalishwa humu ndani lakini ni vingapi vinazalishwa na sio vyetu? Wazalishaji wakubwa wanalipia Kodi kiasi Gani? Maana Kuna mzalishaji anayeweza kulipa Kodi ya ongezeko la thamani labda TSH 300 billion lakini huo ni mchango aliobeba Kwa wananchi. Anachozalisha yeye kila siku kina hasara. Ukifika kwenye corporate tax unakuta kalipa minimal tax maana ana hasara ya kwenye vitabu kila mwaka. Let's be realistic
 
Back
Top Bottom