Ukweli kuhusu maisha ya sanaa na wasanii

Mtoa Mada umeongea point sana, Tumuangalie Michael Jackson ndiye mwanamuziki aliyrefanya matamasha makubwa zaidi ya kimuziki tena sold out za mapema kabisa ikiwa anatumia nyimbo zake za zamani tu. Ikumbukwe kua nyimbo mpya aliyotoa Kama bonus track ni rock the world tu. Pia Kuna Marehemu Milium Makeba yeye ulikua anaalikwa kwenye majukwaa makubwa bila kua na nyimbo mpya ila ulikua anakonga nyoyo za mashabiki kwa nyimbo zake za ujana kama Patapata, Hapo zamani na Maraika, sijajua Hawa wakwetu wanapigania vikumbo vya nini wakati ilikua wako wasubiri kupewa collaboration na wasanii wasasa ili kuonesha ukubwa wao.

Hivi hawajui kua hata Boby Brown bado anapiga shows je yeye ametoa nyimbo Gani mpya!?
 
Hii kitu ya maana sana wakongwe waache uoga bado wana mashabiki wengi sana tena sana.

Mwaka ule Sugu alipiga show kijitonyama na Vinega ilikuwa bonge ya show wakina Soggy,babu,Nature,Mkoloni walipanda jukwaani na kila shabiki aliimba nao nyimbo za zamani.

Wasifikilie kutoa ngoma mpya wajikusanye wafanye matamasha wapige hata tour nchi nzima.

Watu kama Majani na Master Jay wanaweza kusimamia hii kitu na kikawa kitu kikubwa tu
 
Mi nakumbuka nilisikia kwa jirani mtangazaji wa radio one anasema "ifuatayi ni nyimbo mpya ya Prof J Bongo Dar es salaam" tukasogea na kutega sikio kwenye fensi mi na Dada yangu kwa ajili ya kusikiliza
 
ulichokisema ni sahihi sana huwa najiuliza mfano anatokea MB dog kwa stage aisee sipati picha zile nyimbo (ratifa, naona raha, e.t.c) kwa kweli zinanikumbusha mambo mengi ya miaka hiyo(2007+ nilivyokuwa natoroka manyanyaso ya ndugu niliekuwa naishi nae, arafu ndani ya basi nyimbo hizo zilivyokuwa zinani burudisha) kiukweli huwa nakumbuka mbali sana..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaha hapo mwisho nimecheka mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…