Kwanza zari angekua mwingine angeshatukanana mnooo aisee lakin yupo kimya akitoa bango ni la kisomi linayumbisha melii,sinta labda walipatiana Ugand au ,hlf zari alisema wanagawana na ivan 50/50 kwenye masual y pesaa
For the time being, sioni atapiga vipi labda kama kweli kuna ndoa basi ndoa hiyo idumu kwa muda mrefu! Alipiga za kutosha toka kwa Ivan kwa sababu aliishi na Ivan kwa muda mrefu na ingawaje tangu hapo Ivan alikuwa na hela lakini ali-make zaidi alipokuwa na Zari na hivyo kuonekana kwamba utajiri wao ni kama umetafutwa na wote!
Lakini kwa hapa tulipo kuhusu Zari na Diamond, unless kama nilivyosema waende mbali zaidi, lakini kwa sasa Zari kila kitu amekikuta. Hata leo Zari akijifungua na kuthibitika kwamba mtoto ni wa Diamond kisha wakaachana, bado Zari hawezi kupata kitu... labda aombee Diamond afe, kisha Zari ale vya Diamond kupitia urithi wa mtoto! Wakiachana wakati ndoa haijafika mbali, sana sana atakachoambua ni pesa za matunzo ya mtoto! Mbaya zaidi, unless iwe vinginevyo, kwenye Uislamu hakuna "cha mali hii tumechuma wote" bila kuonesha tangible contribution kwenye mali husika unless kama ni suala la kurithi na sio ugawanaji baada ya ndoa kuvunjika!
Mi bado nimelala mvua imenyesh kubwa basi ndio nalala kabisaaaa,nawe usinitishe sura lako sipati picha lilivyo bayaaaaa ungepew km y Nuhu tungekufwaa,ivi bin ulifikiaga wapi kuhusu kuwek picha humu 😆😆😆😆😆😆😆😆😆
Likizo imekua ndefu sanaaa
Binam habari za asubuhii huku SA mvua kubwaa inanyeshaa
AHahahahhahaahhhah, khaa umbea huu ata mswaki sijapiga apa, lisura limenivimba hatar, ukiniona utakimbia, ivi hamna dawa za kupunguza virus vya umbea mwilin? Naona mie virus vinazidi kuzaliana mwilin, yani ni shidaaaa
Ahahaa lol warumi unavituko wewe! Mi nakushauri utafute kazi kwa wahindi tu ndo dawa
Weee ntake radhi, mie handsome kitu black beauty, warumi kwa sura tu ipo kwa kweli, labda mwili ndio sina, halafu mie mpole binamu, watu wananipendaga wanasema mi mkarimu na gentleman, yani huwezi amini watu wanavyoniheshimu, ila nikiingia humu sasa ninavyokuwa kichaa
SIku ukibahatika kuniona LIVE, utakaa kabisa mimi sio warumi,hakuna atakayeamini kabisa yani, kila mtu atashangaa, ila ndio hvyo wengine tuna vipaji tu vya kuzaliwa, hahahahah hahahahah
Bora ivan ana haki ya kuumia kwa sababu ni mke wake, huyo wema si hawara tu kama walivyokuwa wanawake wote waliotoka na diamond, basi wataumia wengi
Nzuri binamu, mimi nilivyo kwenye maisha ya kawaida ni mpole sana, sio muongeaji, nina aibu sana, sio mkorofi, nina huruma ila nina hasira za haraka ila ndani ya mda mfupi zinaisha, mademu zangu wananioneaga sana kwa kuwa mi mpole na sijui kuongea ata kidogo, ni muoga tofauti na humu nilivyo
Ndio mjifunze mkituroga na malimbwata yenu ya kumani msidhani hayana expire date, Wema amemuonea sana Diamond malipo ni hapa hapa.
Mmh!! Ila zari nae akitoaga dongo lake wala hapanick ila huo ujumbe lazima uchanganyikiwe, mmh yule kiboko asewh
Nilishafanya kwa mhindi mmoja kariakoo, nikavunja ndoa yake kwa umbea, maana boss wangu alikuwa kiwembe hatar, nilikua namuendesha, basi kutwa yeye kupakiza wanawake na kwenda nao guest, kama kawa cha umbea nikafanya yangu na kaz nkafukuzwa
Kisaaa.....
Hivi inakuaje mtu achukizwe au kuumizwa na ndoa ya watu ambao hana uhusiano nao??! Akichukizwa Wema au Ivan, naweza kuelewa kinyume chake ni kujitafutia stress za kujitakia!
Special invitees tu, wanaenda walioalikwa tu, kama hujaalikwa usubir tu kuona picha instagram
Mbea yupi jamani niombe urafiki? Maana mie rafiki zangu wote wambea hatari, mtaa mzima wanatuogopa, warumi akipita lazima wajifiche, chezeya rais wa wambea anapita lazima ukimbie