Ukweli mchungu, kama Makamu wa Rais, SSH alibariki kila alichofanya Magufuli!

Ukweli mchungu, kama Makamu wa Rais, SSH alibariki kila alichofanya Magufuli!

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Kwa kweli utetezi mwingine hata hauna maana...eti kama makamu wa Rais hakuwa na chochote cha kufanya zaidi ya kuwa mtiifu kwa Magufuli!

Wapo wanaoenda mbali na kudai eti yako mengi hakuyaunga mkono ila ilibidi akae kimya ili yasimkute yaliyowakuta waliojaribu kumkosoa Magufuli!

Hata hivyo kuna wakati alidiriki kusema anayotenda Magufuli kama Rais hakosei na kwamba maamuzi anayochukua ni katika kutekeleza sera za CCM.

Kwa kifupi alikaa kimya kulinda usalama wake pamoja na kwamba baadhi ya Watanzania walikuwa wakitekwa, kuteswa na hata kupotezwa.

Kwa kweli Watanzania lazima tuanze kutafakari sana aina ya watu tunaowakabidhi madaraka makubwa ya kutulinda kama raia wa taifa hili.
 
Ni wajinga tu ndio huwa na imani hiyo kwamba Samia na JPM hawa kuwa kitu kimoja.

"Haki ni Kama moto hata ufiche wapi bado utaendelea kuunguza"
 
Hizo kauli hutumiwa na wale wanaopenda kuficha udhaifu wake, wanatumia mabaya ya Magufuli kama ngao ya kumkinga Samia.

Kwasababu, kama hakukubaliana na kile mkuu wake alichokuwa anafanya alitakiwa kujiuzulu, lakini kinyume na hapo, anastahili kuhusishwa moja kwa moja na kile mkuu wake alichokuwa akifanya.
 
Hizo kauli hutumiwa na wale wanaopenda kuficha udhaifu wake, wanatumia mabaya ya Magufuli kama ngao ya kumkinga Samia.

Kwasababu, kama hakukubaliana na kile mkuu wake alichokuwa anafanya alitakiwa kujiuzulu, lakini kinyume na hapo, anastahili kuhusishwa moja kwa moja na kile mkuu wake alichokuwa akifanya.
Ndege wafananao huruka pamoja lakini kwa Tanzania si ajabu kumkuta fisi na mbuzi wanaishi pamoja na kushirikiana kwa kila kitu bila tatizo lolote lile.
 
Kwa kweli utetezi mwingine hata hauna maana...eti kama makamu wa Rais hakuwa na chochote cha kufanya zaidi ya kuwa mtiifu kwa Magufuli!

Wapo wanaoenda mbali na kudai eti yako mengi hakuyaunga mkono ila ilibidi akae kimya ili yasimkute yaliyowakuta waliojaribu kumkosoa Magufuli!

Hata hivyo kuna wakati alidiriki kusema anayotenda Magufuli kama Rais hakosei na kwamba maamuzi anayochukua ni katika kutekeleza sera za CCM.

Kwa kifupi alikaa kimya kulinda usalama wake pamoja na kwamba baadhi ya Watanzania walikuwa wakitekwa, kuteswa na hata kupotezwa.

Kwa kweli Watanzania lazima tuanze kutafakari sana aina ya watu tunaowakabidhi madaraka makubwa ya kutulinda kama raia wa taifa hili.
Ukweli mtupu !
 
Ndege wafananao huruka pamoja lakini kwa Tanzania si ajabu kumkuta fisi na mbuzi wanaishi pamoja na kushirikiana kwa kila kitu bila tatizo lolote lile.
Inawezekana endapo mtoto wa fisi atakuwa ananyonya maziwa ya mbuzi au vice versa.
 
Ni Watanzania wachache sana wanaoweza kuelewa nilichokuwa nataka kukisema hapa...it is sad!

Ni Watanzania wachache zaidi wanaweza kupata ujasiri wa kukiri ninachojaribu kukieleza...this is more sad!

Nilichotegemea akifanye toka siku ya kwanza ni kuwaomba radhi Watanzania kwa ushiriki wake 2016 - 2020!

Naandika haya kwa nia njema kabisa ili aweze kuhalalisha hatua anazochukua hivi sasa!
 
Kwa kweli utetezi mwingine hata hauna maana...eti kama makamu wa Rais hakuwa na chochote cha kufanya zaidi ya kuwa mtiifu kwa Magufuli!

Wapo wanaoenda mbali na kudai eti yako mengi hakuyaunga mkono ila ilibidi akae kimya ili yasimkute yaliyowakuta waliojaribu kumkosoa Magufuli!

Hata hivyo kuna wakati alidiriki kusema anayotenda Magufuli kama Rais hakosei na kwamba maamuzi anayochukua ni katika kutekeleza sera za CCM.

Kwa kifupi alikaa kimya kulinda usalama wake pamoja na kwamba baadhi ya Watanzania walikuwa wakitekwa, kuteswa na hata kupotezwa.

Kwa kweli Watanzania lazima tuanze kutafakari sana aina ya watu tunaowakabidhi madaraka makubwa ya kutulinda kama raia wa taifa hili.
Kama alikuwa akiyaona na kunyamaza!
Kwa nini hakujiuzuru?
Ina maana alijali maslahi yake kwanza?
Au ndio plan "B" ya kumuondoa Magufuli ilipoanzia??

Tunalazimika kuamini hivyo,kutokana na Matendo yake na kauli zake kwa sasa!
 
Ni Watanzania wachache sana wanaoweza kuelewa nilichokuwa nataka kukisema hapa...it is sad!

Ni Watanzania wachache zaidi wanaweza kupata ujasiri wa kukiri ninachojaribu kukieleza...this is more sad!

Nilichotegemea akifanye toka siku ya kwanza ni kuwaomba radhi Watanzania kwa ushiriki wake 2016 - 2020!

Naandika haya kwa nia njema kabisa ili aweze kuhalalisha hatua anazochukua hivi sasa!
Haya mambo kwa upande mwingine yanatuonesha watanzania tulivyo wanafiki, tuliojaa ushabiki, na wapenda umbea.

Kelele nyingi zinapigwa kuelekea upande mmoja, na ajabu zaidi, kiongozi wa hizo kelele alikuwa msaidizi wa yule anayemlaumu, nasi tulivyo mazuzu, tunasikiliza umbea wake na kuchangia mada kwa vicheko.
 
Wafuasi wa shujaa mnasubiri nini kwenda kuzikwa pembeni ya kaburi lake? Acheni kutupigia kelele. Mama bado yuko sana hadi 2030.
 
Alipingana nae kwa mambo mengi ila hakuwa na ujasiri wa kujiuzulu..
 
Alipingana nae kwa mambo mengi ila hakuwa na ujasiri wa kujiuzulu..
Believe this and you will believe anything!
Unajuaje? Hebu tutajie jambo moja tu ambalo hakukubaliana nalo!
Kama Magufuli angekuwa hai, hadi lei hii makamu wake angebakia huyo huyo!
 
Back
Top Bottom