Ukweli ni upi juu ya wimbo wa Mandojo na Domokaya?

Aragorn son of Arathorn

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
789
Reaction score
829
Nasikiliza wimbo wa Mandojo na Domokaya, unaitwa Dingi, huu wimbo unaonekana kama ni true story ila sijabahatika kusoma au kusikia sehemu yoyote wakithibitisha kuhusu hili.

Jamaa wanazungumzia maisha halisi ya baadhi ya familia za kipato cha kati, unakuta Mdingi anampunga ila ndani ya nyumba hakuna amani na hata watoto hawafaidi kipato cha Mdingi.

Baba unakuta ni fulu anasa;ananunulia vimada magari na kuwajengea nyumba, anazungusha round bar ila homu unakuta mambo si mambo.

Haya maisha nimekua nayaona mtaani ila siku hizi naona kama trend imepungua, watu wamekuwa responsible na familia zao( ni just observation inaweza ikawa au isiwe sahihi).

Kingine nilichokipenda kuhusu huu wimbo ni pale mwishoni Mandojo anamalizia kwa kusema bado anammiss Mshua pamoja na yote. Kiufupi huu wimbo ni elimu tosha.

Kwa faida ya ambao hawaufahamu nimeweka link ya youtube;mashairi nimekosa(mwenye lyrics zake anaweza kuweka hapa).

 
Hii ngoma kali sana, halafu ina verse moja tu.
Hii makitu ni hamna Mkuu, bonge la pini.
Inaonesha roles za mama zetu kwenye malezi yetu, walikuwa wanauza vitumbua ili tusome, hadi kuna kipindi unajiuliza Mbona wao shule zao zilikuwa ndogo lakini walikuwa wanatukomalia shule kuliko hata Washua waliokuwa wamekata vidato.
 
Stori inamuhusu Domo Kaya,ina uhalisia na maisha ya home kwao kitambo hicho...
 
Hawa wasanii walifanya kazi kipindi hamna haya ma social netwek sioni kama kuna msanii wa sasa angetia miguu hapo walikuwa wanaandika sana sasa hivi mtu anaimba sijui weka mate niteleze mara anataka vya pooltable mwingine ana mandinga mapya daaaa

Kipindi hicho hamna cha wema na zari ili nyimbo yako ifanye poa sokoni
 
Domokaya kaachia Album yake Isikilize Boomplayer mkuu.. Jamaa bado wanafanya kazi nzuri tuu tatizo game yetu Bongo ni ya Kushushana zaidi kuliko kuinuana.. Roho za hivi sana.
 
Story ina ukweli kwa asilimia 60. Kwa tunaoifahamu familia ya Mandojo hatushangai sana.
Mzee unaweza kushare kidogo, maana jamaa kazungumzia kwamba mshua alikuwa katibu mkuu wizara ya fedha, kazungumzia vile vile kuhusu kuvunjwa kwa baraza( ingawa hii naona si kweli, makatibu wakuu na wizara wapi wapi), na vipi kuhusu kupotezana na mshua wake.
 
Zamani nilikuwa na mawazo kama yako, dingi anaishi maisha yake, akishakufa nanyi inakuwa zamu yenu kula bata kupitia urithi atakaouacha. Waacheni madingi wale bata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…