Uchaguzi 2020 Ukweli tunaotakiwa kujua kuhusu mazao ya biashara: Kila zao lilikuwa na enzi zake

Uchaguzi 2020 Ukweli tunaotakiwa kujua kuhusu mazao ya biashara: Kila zao lilikuwa na enzi zake

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Haya mazao ya kilimo ya biashara bei zake kwenye soko la dunia hupangwa na hao wakubwa (mabepari) wa dunia. Bei hizi hazipangwi na watanzania.

Ukweli ni kuwa haya mazao kila moja lilikuwa na enzi zake kwenye kinara. Kulikuwa na enzi ambayo zao la mkonge lilikuwa ni lulu kwa kutupatia fedha za kigeni. Ululu wake ulikuja kuporomoka baada ya ugunduzi wa kutengeneza kamba za synthetic materials kama za nylon viwandani.

Kuna enzi za pamba kuwa kinara kwenye soko la dunia kwa ajili ya kutengenezea nguo. Ululu wake ukaporomoka baada ya ugunduzi wa kutumia synthetic materials kama tetron na nylon kutengenezea nguo.

Kulikuwa na enzi ya zao la tumbako kutengenezea sigara, cigars na tumbako ya kuvuta kwenye kiko. Enzi zake ziliporomoka baada ya kupiga vita uvutaji wa sigara, cigars na viko baada ya kugundua kuwa uvutaji huo ni hatari kwa afya ya binadamu.

Kuna enzi ya kahawa na chai kuwa kinara wa mazao ya kuingiza hela za kigeni. Ukinara wake uliisha baada ya nchi mbali mbali duniani kuwa na uwezo wa kuzalisha kahawa nyingi na nzuri zaidi ya ile ya kwetu.

Enzi za hivi karibuni korosho ilikuja kuwa kinara baada ya nchi ya China ambayo ina idadi ya watu robo moja ya dunia kupenda kula korosho. Ilifikia mwaka 2016 kilo moja ya korosho ghafi iliuzwa zaidi ya shillingi 5,000/ hadi watu wa Mtwara kuanza kuwanywesha mbuzi wao bia! Ukinara wa korosho uliporomoka baada ya muda mfupi tu kutokana na China kuweza kuzalisha korosho nyingi zake yenyewe.

Huo ndiyo ukweli. Bei hizo hazikutelemka kwenye soko la dunia kwa utashi au kwa makosa ya kisiasa. Njia pekee ambayo tunaweza kupata bei nzuri kwenye soko la dunia ni kuachana na kuuza mazao hayo yakiwa ghafi. Kama ni korosho tunatakiwa tuiuze ikiwa imebanguliwa. Kama ni pamba tunatakiwa tuiuze ikiwa imeshatengenezwa kuwa nguo. Kama ni ngozi ya ng'ombe tuiuze tukiwa tumeitengeneza kuwa kiatu au begi au sofa. Vivyo hivyo kwa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi mengine. Hakuna cha siasa hapa bali ni sayansi na tekinolojia tu.

Hata madini yetu hali ni hiyo hiyo. Tusiyauze yakiwa ghafi. Na hii kwa bahati nzuri ndiyo dhamira ya serikali yetu. Tunatumaini wakipewa miaka mitano mingine watatimiza dhamira hii kwani kwa mara ya kwanza serikali yetu inaongozwa na mwanasayansi aliyebobea. Tumeshuhudia manufaa ya kuongozwa na mwanasayansi katika mapambano ya kisayansi dhidi ya janga la kisayansi la COVID 19! Tusiitupe bahati hii.
 
Kwa nini unadhani hivyo wakati hata huko Zanzibar tumeweka mwanasayansi?
Politiksi ya bongo haipo kuangalia mambo kama haya, kila kiongozi ajaye anapiga kopo teke kwa anayefuata mradi mambo yaende tu.
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Tunajisahau mno, nyanya zote hakuna maendeleo ya kuboresha mazao yetu, achilia mbali ugunduzi wa kuongeza dhamana yake. Kahawa mpaka sasa duniani inanyweka sana, katani bado inahitajika, korosho na cocoa hali kadhalika.

Sasa angalia zana zinazotumika sasa kuzalisha na linganisha na wakati huo tukiwa vinara wa uzalishaji. Utaona ni bora enzi hizo tulikuwa tunajituma, sasa hivi ni hohehahe.
 
Mbona tuliambiwa tunyonywa kwenye korosho zetu mpaka akaamua kutuletea jeshi na kuahidi kuwachapa shangazi zetu.
 
Masoko yanatafutwa na yanagombaniwa pia. Lazma kuwe na mikakati ya kulisaka hilo soko hata km bidhaa inazalishwa kwa wingi. Tunaingia mikataba na nchi nyingi duniani kuingiza bidhaa zao kwetu na sisi tunawekeana mikataba kwamba ukiingiza bidhaa hii kwetu na sisi tutakuuzia mazao haya baada ya kufanya utafiki na kugundua wao wanapenda mazao gani lamda na uzalishaji wao ni mdogo.

Ndio maana unaona maraisi wa nchi kadhaa wanatembelea nchi nyingine na miongoni mwa ajenda zao pia ni kutafuta masoko. Tunaamini wapo mabalozi huko nchi nyingine lakini nguvu ya balozi haifanani na raisi.

Umesema korosho imeshuka bei coz China anazalisha naye kwa wingi sasa, hivi mikorosho inaota km mchicha vile, yaan miaka mitatu nyuma china ananunua kutoka tanzania ghafla kwao mikorosho ushakuwa wanavuna kwa wingi sasa.
 
H
Politiksi ya bongo haipo kuangalia mambo kama haya, kila kiongozi ajaye anapiga kopo teke kwa anayefuata mradi mambo yaende tu.
Hayo yalikuwa zamani. Kwa sasa tuna wanasayansi wanaoongoza nchi kisayansi. Ndiyo maana wamepandisha uchumi wa nchi yetu hadi kifikia wa kati yaani kutoka GNI ya USD 600 mwaka 2015 hadi USD 1,200 mwaka 2019. Wakipata miaka mingine 5 watapandisha GNI hadi kufika USD 6,000 na hivyo uchumi wa nchi yetu kuwa wa juu katikati!
 
Tunajisahau mno, nyanya zote hakuna maendeleo ya kuboresha mazao yetu, achilia mbali ugunduzi wa kuongeza dhamana yake. Kahawa mpaka sasa duniani inanyweka sana, katani bado inahitajika, korosho na cocoa hali kadhalika.

Sasa angalia zana zinazotumika sasa kuzalisha na linganisha na wakati huo tukiwa vinara wa uzalishaji. Utaona ni bora enzi hizo tulikuwa tunajituma, sasa hivi ni hohehahe.
Tatizo ni kuwa kwa sasa mazao ghafi hayanunuliki kabisa kwenye soko la dunia. Hivyo tunalazimika kuyauza kwa makagomba wa kimataifa kwa bei ndogo sana. Makagomba hawa wakishayanunua huyapeleka nchi kwao ambako huyasindika, kuya pack vizuri kwa nembo za nchi zao na kuyauza kwenye hilo soko la dunia kwa bei ya zaidi ya mara mia moja waliyotulipa sisi. Na yanaandikwa yametengenezwa nchini kwao eg Made in India.

Kwa mfano hiyo korosho ghafi ya Mtwara hununuliwa na makagomba wa India ambao ndiyo huiuza China ikiwa imebanguliwa na kupakiwa vizuri na nembo ya made in India. Vivyo hivyo kwa tanzanite na mazao mengine.
 
hivi mikorosho inaota km mchicha vile, yaan miaka mitatu nyuma china ananunua kutoka tanzania ghafla kwao mikorosho ushakuwa wanavuna kwa wingi sasa?
Akikujibu nitag.
Kwa mazao kama mkonge na pamba yuko sawa. Lkn kwa haya mengine hapana. Ametuingiza chaka.
 
Akikujibu nitag.
Kwa mazao kama mkonge na pamba yuko sawa. Lkn kwa haya mengine hapana. Ametuingiza chaka.
Walianza kuipanda miaka kadhaa iliyopita. Sasa imeanza kuzaa matunda. Bado soko lipo lakini kwa ile iliyobanguliwa na kufungwa vizuri. Wanaipata kupitia India.
 
Bado soko lipo lakini kwa ile iliyobanguliwa na kufungwa vizuri. Wanaipata kupitia India.
Kwahiyo unakubaliana na hoja kwamba sera mbovu za kiuchumi na mihemuko au mikurupuko ya John imechangia kushusha bei ya korosho za mikoa ya kusini?
 
Bahati mbaya sana kuna watu wataamini hiki kitu unachoandika hapa. .
Labda nikwambie tu...

1.Mlaji mkubwa wa Korosho ya Tanzania ni pamoja na Indians.... uwekezaji wake kwenye soko hilo ukoje?
2.Sigara ni addictive na demand yake haijwah kushuka. .regardless of heath awareness and environmental blab la, Issue ni value chain management na namna gani unalinda viwanda vyetu vingi vimeuwawa na Chama kushika hatam
3.Pamba. .. dunia nzima inahitaji pamba ila uzalishaji wetu duni unafanya pambana yetu iwe na low market value. . Kuna kipindi walikuwa wanaweza had vimawe ili iongezeke yote hii inachangiwa na uzalishaji duni
4.Mkonge bado demand ipo.. Muulize tapeli MO akwambie. .... shida ni production and value chain management
5.Serikali haina mpango wowote na kilimo. .. kilimo kwa nchi yetu= umasikini wa kujitakia. .
6.Madini. . Naona Magufuli ameamua kulivalia njuga ni vizur na nadhan tunaenda sawa.. shida ipo kwenye gas na mafuta kama yapo
 
Haya mazao ya kilimo ya biashara bei zake kwenye soko la dunia hupangwa na hao wakubwa (mabepari) wa dunia. Bei hizi hazipangwi na watanzania.

Ukweli ni kuwa haya mazao kila moja lilikuwa na enzi zake kwenye kinara. Kulikuwa na enzi ambayo zao la mkonge lilikuwa ni lulu kwa kutupatia fedha za kigeni. Ululu wake ulikuja kuporomoka baada ya ugunduzi wa kutengeneza kamba za synthetic materials kama za nylon viwandani.

Kuna enzi za pamba kuwa kinara kwenye soko la dunia kwa ajili ya kutengenezea nguo. Ululu wake ukaporomoka baada ya ugunduzi wa kutumia synthetic materials kama tetron na nylon kutengenezea nguo.

Kulikuwa na enzi ya zao la tumbako kutengenezea sigara, cigars na tumbako ya kuvuta kwenye kiko. Enzi zake ziliporomoka baada ya kupiga vita uvutaji wa sigara, cigars na viko baada ya kugundua kuwa uvutaji huo ni hatari kwa afya ya binadamu.

Kuna enzi ya kahawa na chai kuwa kinara wa mazao ya kuingiza hela za kigeni. Ukinara wake uliisha baada ya nchi mbali mbali duniani kuwa na uwezo wa kuzalisha kahawa nyingi na nzuri zaidi ya ile ya kwetu.

Enzi za hivi karibuni korosho ilikuja kuwa kinara baada ya nchi ya China ambayo ina idadi ya watu robo moja ya dunia kupenda kula korosho. Ilifikia mwaka 2016 kilo moja ya korosho ghafi iliuzwa zaidi ya shillingi 5,000/ hadi watu wa Mtwara kuanza kuwanywesha mbuzi wao bia! Ukinara wa korosho uliporomoka baada ya muda mfupi tu kutokana na China kuweza kuzalisha korosho nyingi zake yenyewe.

Huo ndiyo ukweli. Bei hizo hazikutelemka kwenye soko la dunia kwa utashi au kwa makosa ya kisiasa. Njia pekee ambayo tunaweza kupata bei nzuri kwenye soko la dunia ni kuachana na kuuza mazao hayo yakiwa ghafi. Kama ni korosho tunatakiwa tuiuze ikiwa imebanguliwa. Kama ni pamba tunatakiwa tuiuze ikiwa imeshatengenezwa kuwa nguo. Kama ni ngozi ya ng'ombe tuiuze tukiwa tumeitengeneza kuwa kiatu au begi au sofa. Vivyo hivyo kwa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi mengine. Hakuna cha siasa hapa bali ni sayansi na tekinolojia tu.

Hata madini yetu hali ni hiyo hiyo. Tusiyauze yakiwa ghafi. Na hii kwa bahati nzuri ndiyo dhamira ya serikali yetu. Tunatumaini wakipewa miaka mitano mingine watatimiza dhamira hii kwani kwa mara ya kwanza serikali yetu inaongozwa na mwanasayansi aliyebobea. Tumeshuhudia manufaa ya kuongozwa na mwanasayansi katika mapambano ya kisayansi dhidi ya janga la kisayansi la COVID 19! Tusiitupe bahati hii.
Umeandika vizuri Sana huko juu..ukaharisha para ya mwisho🙃
 
Bahati mbaya sana kuna watu wataamini hiki kitu unachoandika hapa. .
Labda nikwambie tu...

1.Mlaji mkubwa wa Korosho ya Tanzania ni pamoja na Indians.... uwekezaji wake kwenye soko hilo ukoje?
2.Sigara ni addictive na demand yake haijwah kushuka. .regardless of heath awareness and environmental blab la, Issue ni value chain management na namna gani unalinda viwanda vyetu vingi vimeuwawa na Chama kushika hatam
3.Pamba. .. dunia nzima inahitaji pamba ila uzalishaji wetu duni unafanya pambana yetu iwe na low market value. . Kuna kipindi walikuwa wanaweza had vimawe ili iongezeke yote hii inachangiwa na uzalishaji duni
4.Mkonge bado demand ipo.. Muulize tapeli MO akwambie. .... shida ni production and value chain management
5.Serikali haina mpango wowote na kilimo. .. kilimo kwa nchi yetu= umasikini wa kujitakia. .
6.Madini. . Naona Magufuli ameamua kulivalia njuga ni vizur na nadhan tunaenda sawa.. shida ipo kwenye gas na mafuta kama yapo

Comment ya kiume hii
 
Kwahiyo unakubaliana na hoja kwamba sera mbovu za kiuchumi na mihemuko au mikurupuko ya John imechangia kushusha bei ya korosho za mikoa ya kusini?
Sera siyo mbovu kwani sera zinasema mazao haya yote yaongezewe thamani kabla ya kuyauza nje. Sera zinasema tusiyauze nje yakiwa ghafi. Tuyaongezee thamani hapa hapa kwani faida yake ni kubwa sana ikiwamo kuzalisha ajira nyingi kwa vijana wetu.

Sera hiyo nzuri kama zilivyo sera zetu zote ni ya zamani sana, tangia enzi za Mwalimu Nyerere. Watanzania ni wazuri sana duniani kwa kutunga sera nzuri. Shida yetu imekuwa ni utekelezaji wa hizo sera.

Matokeo yake imekuwa sera nzuri zinaandaliwa Tanzania lakini utekelezaji wake unafanywa ma nchi zingine ambazo huja kwetu ku copy sera zetu. Kwa mfano sera ya kuhamisha makao makuu kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, Nigeria ilii copy na kuitekeleza kwao kwa kuhamisha makao makuu yao kutoka Lagos kwenda Abudja. Kenya ndiyo usiombee: sera za ma fly over, international airport designs, tanzanite refinery etc wamezikopi kwetu na kuzitekeleza kwao. Sisi zinabaki kwenye makaratasi.

Bahato nzuri miaka 5 iliyopita tumepata mwanasayansi aliyejikita kuzitekeleza sera hizo, tena kwa spidi ya ajaabu. Amezikuta ziozea kwenye makabati na kuamua kulala nazo.mbele kwa mbele. Na kwa hakika atakapopata miaka mitano mingine atazimaliza zote na kuweka zingine mpya. Huu ndiyo ukweli.
 
Back
Top Bottom