UKWELI UNAUMA: Jimbo la Singida Mashariki ni kama halina mbunge,Wanafunzi wanakaa chini

UKWELI UNAUMA: Jimbo la Singida Mashariki ni kama halina mbunge,Wanafunzi wanakaa chini

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Wakati maeneo mengi nchini wakiendelea kufaidi matunda ya kinachoitwa Elimu Bure/Elimu bila Ada, huko mkoani Singida Wilayani Ikungi kata ya Choda, Shule ya msingi Choda wanafunzi wanataabika kwa kukaa chini madarasani. Ni watoto wa wakulima na wafugaji ambao ni sehemu ya walipa kodi katika wilaya hiyo.

Hili ni tatizo la muda mrefu sana ambalo uongozi wa shule hiyo imekua ukiogopa kulisema pengine kwa kuogopa kuchukuliwa hatua na uongozi wa Wilaya ambapo viongozi wa Chama wilaya wakiongozwa na mwenyeki wa chama wilaya ndugu Mika Likapakapa ambaye amekua akiwatishia walimu ndani ya wilaya hiyo wakisema matatizo yao atawafukuzisha kazi kwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo.
Wananchi kwa kipindi kirefu wameamua kulisema tatizo hili wao wenyewe pengine kelele zao zinaweza kusaidia.

Cha ajabu tatizo hili mbunge wa jimbo hilo ndugu Mitaji Mtaturu analijua kwa muda mrefu, kila aliambiwa amekua akipiga chenga, diwani wa kata ya Choda analifahamu tatizo hili lakini naye awali alikua akilisemea lakini pengine kwa kuogopa kunyimwa posho na Mkurugenzi naye ameamua kupiga kimya sasa.Jimbo zima hali halisi ndio iko hivyo pamoja na jimbo kua na uwakilishi pamoja na uongozi wa wilaya.

Mpaka jicho la Fundi Madirisha linapenya kunako shule hiyo, hali. Ni mbaya sana si kwa sababu hakuna uwezo wa kushughulikia na tatizo hilo au wanafunzi ni wengi, laahasha ni viongozi wameamua kulifumbia macho tatizo ili vijana wa wakulima na fugajj waendelee kukaa chini wakati watoto wako wako English Medium.

Haya si mambo ya kuachwa yaendelee wala kufumbiwa macho wakati hali shwari hasa kwa kipindi hiki ambacho serikali inajinasibu kua ni Elimu bila Ada.

IMG-20210611-WA0034.jpg


IMG-20210611-WA0035.jpg


IMG-20210611-WA0033.jpg
 
Umenena Kiuchonganishi na kimajungu sana , Ulitakiwa tu Useme kunatatizo La Ukosefu wa madawati Mashuleni Jimbo hilo.
 
Hii nchi hii🤔🤔🤔,mazingira ya hiyo shule ni heri serikali ingepeleka pesa ya Elimu bure kwenye utatuzi wa SUALA la wanafunzi kukaa chini.
Inasikitisha Sana karne ya 21 Tanzania tunapambana na uhaba wa madawati wakati CHINA inawaza namna gani watafika kwenye sayari ya Mars!!

The problem is,we choose village fools into offices.
 
Hiki suala si mbunge. Yeye kazi yake ni kuwasemea wananchi bungeni lkn kama serikali haitekelezi iweze.
Ki.sibgi ktk kipindi cha miaka mingi serikali imekuwa ikijitahidi sana kutekeleza manukumu yake kikamilifj. .adarasa ya sasa hujengwa full jd madawati. Zamu ya man wao utafika tu na mabo yataenda. Hawaangalii habari za u ungemfanya siku jz
 
Si tulielewana kua lissu ndio kikwazo!?
Sasa hizi ndio faida za kumtimulia mbali lissu
Linchi la uchumi wa kati linasonga nyuma badala ya mbele
 
Hiki suala si mbunge. Yeye kazi yake ni kuwasemea wananchi bungeni lkn kama serikali haitekelezi iweze.
Ki.sibgi ktk kipindi cha miaka mingi serikali imekuwa ikijitahidi sana kutekeleza manukumu yake kikamilifj. .adarasa ya sasa hujengwa full jd madawati. Zamu ya man wao utafika tu na mabo yataenda. Hawaangalii habari za u ungemfanya siku jz
Ndugai alisema ,Lissu hakuacha alàma.
 
Back
Top Bottom