Asa nikwambie kitu kiongozi!chips mayai ni ghali zaidi ya chakula alacho daywaka!chips mayai si chini ya sh2000 wakati daywaka wengi wanakula kwa mama lishe!kwa mama lishe chakula bei yake,wali/ugali nyama una mboga za majani kidogo na wkt mwingine unapata na kipande cha tunda la msimu la wakati huo bei yake ni 1000 mpaka 1500 halafu anakunywa na maji mengi!Mla chips mayai/kuku ataweka tomato sosi,chill sosi halafu anashushia na soda barrrdiiiii!
Umesahau kwa mama ntilie kuna hamira pia....
Chakula bora kamwe hakipo kwa mama ntilie. Ni kile unachopika mwenyewe au kupikiwa nyumbani. Chapaswa kiwe ni mlo kamili.
WANGA kiasi (ugali, chipsi, chapati, wali, maandazi, n.k.), MBOGAMBOGA(mchicha, spinachi, nyanya, karoti, vitunguu, boga, n.k.), NYAMA kiasi/jamii za MAHARAGE/MAYAI (moja kienyeji kila siku), matunda, MBEGUMBEGU(za boga, karanga, korosho, ubuyu, ufuta, n.k.), VIUNGO (hiliki, nazi, tangawizi, n.k.), MAFUTA mazuri (alizeti, mawese, ya karanga, siagi kiasi, samli, n.k.), MAZIWA (hasa mtindi kwa watu wazima, jibini, n.k.)....
Sasa huo mkusanyiko ni lazima uupate kila siku japo si kila aina kwa wakati mmoja. Ila matunda, wanga, protini na mbogamboga ni kila ulapo.
Chipsi zege na kachumbari ina virutubisho vingi kuliko alae ugali nyama. Anachokosea mla chipsi ni kutumia soda badala ya mtindi na yai kisasa badala ya kienyeji.
Usijumuishe tu kua chipsi yai inaharibu vijana.......