From Sir With Love
JF-Expert Member
- Sep 13, 2010
- 2,076
- 3,813
Nadhani wewe ni wale watu ambao hutaki kumwingiza mwenzako kwenye matatizo, lakini upo radhi kuingizwa kwenye matatizo, na ukakaa kimya ili uonekane mwana.Ndio marafiki Wa mashaka wana gharimu sana
Japo ni zamani, lakini kuwa namsimamo wako wewe kama wewe ni vizuri.
Rafiki yako anatakiwa ajue msimamo wako kiasi kwamba hata kukusingizia atashindwa aanzie wapi.
Nakumbuka mzee wangu aliombwa hati ya nyumba na rafiki yake ili akachukue mkopo. Mzee alimkatalia kiroho safi japo yule mzee alimind sana.
Kuna mzee mmoja upande wa shemeji yangu, alimpa rafiki yake hati ili akachukue mkopo. Bahati mbaya yule mzee akafariki dunia. Aliyepewa hati anasema hadaiwi kitu na hajui kuhusu hati. Mzee wa watu alimpa rafiki yake hati kienyeji na sasa familia nzima inapata shida.
Kuwa na msimamo ndiyo jibu pekee. Ukiona rafiki haeleweki, songa mbele.