Ulikua kikojozi utotoni? Hebu njoo hapa...

torvic

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2016
Posts
3,978
Reaction score
9,841
wakuu!
najua mpooo! wale tulio imbiwa kindumbwe ndumbwe chaaalia!
kindumbwe ndumbwe chaaalia!
kikojozi na nguo kaichoma moto huyoooo! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

nimekumbuka enzi hizo mtaalamu nilikua naachia kojo sana! mpaka nikawa najikataa, usiku ukifika sinywi maji wala cha juice lakin bado nilikua naliachia kojo
alafu sijui kulikua na maajabu gani wakati unalimimina kojo unajiskia rahaaa uku unasindikizwa na kandoto upo toilet unakojoa kumbe ndo unalilimina uku! hahahha

najua umu ndani wapo vikojozi wastaafu wa enzi hizo embu tukumbushane jinsi ilivokua inakuuma baada ya kuchakaza godoro la watu na kojo lako
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Mungu wanguuu[emoji119][emoji119]

Umenikumbusha mbaliii...
Enzi hizo bwana nilikua sijui grade 2.
Hapo ilikua moshi.
Sasa ile baridi bwana nilikua nakojoa balaaa.
Nakumbuka dada wa kazi alikua Isabela. Mzuri balaaa. Na mwingine rozalia. Mzuri huyoo pia. Ila jaman rozalia aliku mkali jaman huyu mdada na vile mama alikuaga anasafiri mara nyingi tunabaki na wadada wa kazi[emoji23][emoji23][emoji119]
Miaka hiyo wazazi wetu walikua wanafanya viashara zote hasa vinuwaji kutoka kenya. Basi sisi kunywa soda ilikua bururu.
Enzi hizo kama mnakumbuka kulikuaga na zile panties za zebra[emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119][emoji119]
Nzuri zilikuaga za cotton. Basi nilikua naletewaga na mama sana.
Kasheshe kwenye suala la kujikojolea.
Hicho kichapo cha dada rozalia ni Yesu aingilie kati. Hapo bado mauji uji tunayopeea ya kulazimishwa[emoji119][emoji23][emoji23][emoji23]
Huo mkojo achenii na ile baridi.
Halafu sasa kabla nipee kitandani naota kabisa nakojoa. Yaani nakua najisikia raha as narelease kitu. Navyoshtuka ndo najua nilichofanya.
Nifanyeje sasa?[emoji23][emoji23] siwezi msingizia mdogo wangu. Naogopa dhambi. Japo yeye akikojoaga alikua ananisogeza mpaka sehemu yake kwahiyo balaa linaniangukia mini[emoji1787][emoji1787]
Na wala simsemei.
Nabondwa sana na dada rozalia.
Sasa nikaanza mchezo. Panties nnazo kibai za zebra zile. Nikipee naamka zangu kimyakimy usiku wa manane, nabadilisha panty[emoji1787] nakua mkavuuu.
Asubuhi nikikaguliwa miye waalaaa.
Mdogo wangu nae alajifunza kubadilisha kaptula. Sasa tunapiga kojo na kubadili asubuhi tukikaguliwa na kunuswa walaaa. Tukaanza katabia tujikojoa tunaanka mapemaaa rozalia anatukuta tunafua zetu mikojo hadi akawa hatubondi tena[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Namiss utotoooo.
Mungu akutunze dada Rozalia. Iko siku nitakutafuta panapo majaaliwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
yani utoto huu wa kujikojolea ukikumbuka lazima utoe ujicheke,

mimi nilikua nina adi mambinu yakiyunani najikojolea nikistuka ntafanya manuva kupakausha hapo, ntaweka manguo manguo πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ mpaka kuna kauka
 
Hiyo ya kuweka manguo ilikuwa inasaidia sana. Unaweka nguo, then unalalia ili unyevu uhamie kwenye nguo.
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Ha ha ha nmemkumbuka mdogo wangu mmoja alikua hata kama kalala saa mbili mkimuamsha kuja kula saa tatu hv unakuta kashamwaga.

Hyo siku amekula kalala mapema mie bado nazuga nkasema ngoja nijinyooshe kidogo ni buy time nikaoge mara naona mtu kaamka kapiga magoti anaanza kukojoa aisee nilimtia bonge la banzi mpka nikaingia huruma

Mama Kuja anashangaa dogo analia anauliza nn namwambia mwanao kaamka hapa kaanza kukojoa kama yupo chooni ikabd acheke tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahahahhaa!!! Ngoja nitie kambi hapa nishuhudie wazee wa kulimwaga.

Nilikuwa nalimwaga lakini kiwango hakikutosheleza, sikuwa professional. Yaani sikufikia caliber ya international talents kama mtoa mada na wachangiaji wengineo.

Cc JF Members
 
Nilishawahi kumwaga kojo sebureni na mzee yupo mvua ilikuwa inanyesha nikapitiwa usingizi juu ya kochi tena ni mchana! Nilijilaumu sana hlf nilikuwa sielewi nini kilinikumba mpk kufanya upuuzi ule wkt mahali pangu pa kujikojolea ilikuwa ni kitandani πŸ˜‚ nililamba stiki na ubaridi ule inakera sana😠😠
 
Hahahah hii ya kukausha ndo yenyewe. Kuna katoto home kama kakilimwaga nachukua shuka lingine naweka juu. Bado naendeleza mbinu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninekumbuka mbali sana, nilikojolea kitanda (godoro ni ngozi) hadi ngozi ikatoboka. Mpk std 5 nakojoa. Siku nikajaribu kufungua kidudu na kamba ili mkojo usipite lakn sijui kamba ilitokaje. Nikabadili mbinu Nika tafuta kichupa nikawa naingiza kidudu wakati nalala lakini nashangaa asbh niko upande mwingine na mkojo umeshamwagika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha wewe ulikuwa kiboko yani ulifikia maamuzi hayo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi mpaka leo sijapata jibu..Kwanini kojo la utotoni hua linanukia ubwabwa.?
hahaha mdau inaoneka ulivyokuwa mtoto ulikuwa unapenda ubwabwa sana
 
Hahahahahahhaa!!! Ngoja nitie kambi hapa nishuhudie wazee wa kulimwaga.

Nilikuwa nalimwaga lakini kiwango hakikutosheleza, sikuwa professional. Yaani sikufikia caliber ya international talents kama mtoa mada na wachangiaji wengineo.

Cc JF Members
hahaha
wewe jamaa! eti hukuwa professional kama mtoa mada!
ata mtoa mada hakua talented kiviilee kama unavyo mpa mapwointi
 
Michango yenu itakuwa ya maana kwa wengi mkitueleza nliwezaje kupona. Kumbuka wadogo zenu wanapitia hali kama zenu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
mkuu wewe ulikuwa mzoefu kazini, kazi kazi mpaka kwenye makochi ya alafu mchana sasa! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
mkuu wewe ulikuwa mzoefu kazini, kazi kazi mpaka kwenye makochi ya alafu mchana sasa! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Kazi kazi ilikuwa ni pale unywe ma juice cola kisha ukalale kale ka njozi ketu pendwa kalikuwa kananitembelea nami bila hiana namwaga jikojo hilo Sasa ulemkojo wa juice cola unavyonuka hulali kabla ya kushushiwa kipondo ule mkojo tu unakuwa umeshakutesa kwa harufu maana harufu yake ilivyombaya ni kana kwamba unakuimbia ule wimbo wa utotoni "Leooo leoo utakoma!!!"πŸ˜‚πŸ˜‚
Presha juu ya presha hapo ukiulalia unawasha kishenzi na hakuna muujiza wa kuukausha!! Tumetoka mbali Basi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…