Ulimbukeni wa akina Hasheem Thabit

m nafikiri n PROBLEM YA WATZ WOOOOOTE


Sio kweli mzee mimi niko nje ya tz miaka kibao sana lakini kiswahili nakiongea kama kawaida sijasahau hata neno 1'tena nakitukuza sana hata huku jamaa kibao nimeshawafundisha kiswahili wanajua maneno kibao tu'sema ulimbukeni tu kupenda vya wenzetu na kuchukia vyetu ndio tabu hyo'
 

Hizi ndo kauli,ukiskia majembe ndo kama wewe..NAKUPA TANO ILIYOSHIBA!!
 
Hata Le Mutuz Kiswahili kasahau na Kiingereza hakijui vizuri, sijui Kigogo nacho anakikumbuka?
 
Ni vema na Haki kwa ulilolisema hapa lakini alinishawishi mimi kuona kuwa nilazima Hashmu aonge kiswahili ambacho kitampa tabu kueleweka kwenye jamii yake......mfano ni Kajumlo wakati akiishi Sheraton..sasa Serena alijitahidi kuongea kiswahili lakini alishindwa hivyo mimi kama sioni wapi alipo kosea mpaka kumanzishia uzi!!wewe unaye jua lugha 3 sitatizo yawezekana hukuwahi kukaa kawenye nchi hizo kwakipindi chote chakukufanya ukasahau kiswahili......Pili ujue ukikaa mahali kwa takiribani miaka 5 hauongei lugha yoyote uliyokulia kunauwezekano mkubwa wakusahau baadhi ya vitu siyo kila kitu utakuwa unajua ila kwakuzingatia umri wake na kwakuwa nikijana na wengi wa vijana wetu hupenda tamaduni za magharibi na yeye mungu kampa kitu alichokitamani...anajisikia kuongea kama mmarekani..na ndo vijana wetu wanavyopenda acha lugha hata mavazi nk!
 

Acha uwivu wa kizaramo wewe hata utawire uchi ukwel utabaki ukwel kwamba hata fedha za ukoo wenu wote haziwezi kunusa za huyu kijana,
inasikitisha sana kuona unashadadia uswahili wakati wenzako wanachapa pesa,ulitegemea kwa kipindi chote alichokuwepo mbele arudi na kiswahili cha kina shaaban robert au mrisho mpoto??
inaonyesha jinsi gani ulivyo na elim duni ya kunyambua psychological facts,mabadiliko ya kutokitumia kiswahili kwa mda mrefu yana uwezo wa kupoteza utashi wake wa kuinyambua misamiati ya hiyo lugha,hasa kwa jimbo alilokulia!na ndicho kilichomkuta huyu kijana aliyebarikiwa na rabbana kwa kukukimbiza hata wew kwa mshiko..
UJINGA SANA UNAO UFANYA,KAA CHINI BUNI MBINU ZA KUKUTOA NA SIO MBINU ZA KUDISCUS MAISHA YA WATU AMBAO HAWAJAWAHI HATA KUKUFIKIRIA NA HAWATO FANYA HIVYO KAMWE!!
 
Mimi ananiudhi tu John Tendwa anavyozungumza...huwa natamani kumtandika bakora kujifanya sharobaro...

Heri wewe umesema! Ananichosha kweli yule baba karibu ataangukia kule kule kwa ......wa aiiiitiiiviiiii....
 
Wivu wa kike....wivu wa kijinga.....wivu wamaendeleo............wivu wivu wivu utakuua!!Au wewe ujui kama Hashmu ni Superstar?? celebrity??

We kweli kaka kiazi.....ukiwa superstar wa kitanzania ndio uache utamaduni wako??? Mojawapo ya kazi za superstar kwa nchi yake ni kuitangaza nchi yake pamoja na tamaduni zake, ikiwemo lugha kwa mataifa mbali mbali.....acha kufikiria kwa kutumia masaburi.
 
Ujinga ni kwenda Marekani miezi 3 kurudi unaongea "whaatss mameen", You know i'm sayin', Aiyt, Holla"....wakati ukienda India 4 years unarudi na kiswazi kile kile. wala huna "Vee arrr doing werry Vell MY friend"
 

Una wivu wa kike wewe
 
Ujinga ni kwenda Marekani miezi 3 kurudi unaongea "whaatss mameen", You know i'm sayin', Aiyt, Holla"....wakati ukienda India 4 years unarudi na kiswazi kile kile. wala huna "Vee arrr doing werry Vell MY friend"

Umeona eeeh! Ahahahahahah! Alafu wakichanwa ukweli wanajaa povu!
 
Tido mhando kakaa sana uingereza lakini hajasahau kiswahili. Mabalozi wengi wamekaa sana nje lakini hawajasahau kiswahili.

alikuwa anatangazia bbc kwa lugha gani?

samahani kidogo
 
We Jamaa acha Wivu...alokwambia Hashimu amesahau kiswahili nani ??? Mbona anaongea Kiswahili fresh tu,sema amemiss Misamiati kadhaa ya Mtaani Kinachokuchanya ni Vocal na accent...
Nilikaa Iringa 4yrs kurudi Dar nikawa naoneka na rafudhi ya Kihehe...ivoivo nilivoenda Ujerumani kurudi nikawa naongea Kama natafuna Mahindi nachekwa..Hashimu Hakai na brokeAssNigger wa mtaani hakuna waswahili anaokaa nao zaidi ya Friends zake...Rafudhi/rafuzi lazima ipotee

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 

Na wewe ni wale wale akina Hasheem!
 
Hashim Thabit ni limbukeni tu mbona humu humu JF watu kama Nyani Ngabu wanakaa huko huko state na wanaongea Kiswahili mpaka Kisukuma bila shobo kama za Hashim Thabit
 
Last edited by a moderator:
Na wewe ni wale wale akina Hasheem!

Ukiona watu wanabadili mpaka uasili wa majina yao huyo usimtegemee kuwa balozi wa anakotokea..muacheni utoto na utajiri wa ghafla umpumbaze akijashtuka treni ishaondoka kitambo...,asisahau hii Bongo Go East go West..
 
HAKUNA MTU ALIYEENDA ULAYA MTU MZIMA AKASAHAU LUGHA YAKE. LABDA KAMA ALIENDA MTOTO SANA. HAPO BADO NIMEKATAA. KAMA ANAONGEA KIINGLISH-KINUGU-KIAMERIKA HILO CHAGUO LAKE. LAKINI KASAHAU KIBANTU...NONONONO...:nono:
 
Hasheem kinachomsumbua ni ushamba wa kuzaliwa nao....watu wanashindwa kuelewa kwamba ata ma-celeb wapo washamba,tena wengi tu mkitaka nitawaorodheshea wachache..ushamba na ki2 ambacho kipo nje ya uwezo wake kukiacha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…