"Ulimbukeni" wa Joyce Banda na Uhuru Kenyatta ndio unaoathiri mahusiano ya nchi zao na Tanzania

"Ulimbukeni" wa Joyce Banda na Uhuru Kenyatta ndio unaoathiri mahusiano ya nchi zao na Tanzania

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,346
Huwa baadhi ya watu wakiingia katika nafasi za uongozi kwa mara ya kwanza, wanakuwa na 'moto' fulani ambao baada ya muda hupoa. Tunashuhudia hayo sio kwa maraisi tu bali hata kwa viongozi wadogo kama wakuu wa wilaya, mikoa au hata wakuu wa vitengo na taasisi serikalini.

Pengine ni kutokana na ambitions kubwa wanazokuwa nazo na kwa viongozi wa nchi pale wanapokuwa na uzoefu mdogo kwenye mambo ya kidiplomasia ndipo athari zinakuwa dhahiri zaidi.

Tulishuhudia Joyce Banda alipoingia madarakani, akaja na "moto" fulani wa kutaka kufanya mageuzi ya kiuchumi na kimaisha kwa Wamalawi over night.. Moto wake huo ukasababisha hata mahusiano yake na Tz yakatatizika kwa muda kwa jambo ambalo ni la kihistoria, na historia hiyo haionyeshi uwezekano wa jambo hilo kutatuliwa miaka ya karibuni. Tumelizoea, tunaishi nalo na pengine watakiamua vizazi vyetu vijavyo huko.

Banda baada ya kukaa na maraisi wenzake na kupewa cheo huko sijui SADC, kajifunza diplomasia. Sasa hivi kama mpolee, hatumsikii tena akitoa matamko ya hovyo hovyo... Keshajifunza "table manner", jinsi ya kula na maraisi wenzake...

Baada ya Banda, kaja tena Uhuru. Nae kaja na moto ule ule, diplomasia sifuri. Nae amerukaruka na akina Mu7 na Kagame ambao wana "interests zao", lakini tunaona anamtuma Amina Mohamed, aje Tanzania kubembeleza. Baada ya ziara zake mbili tatu, Uhuru nae anaanza kujifunza Table manner.. Baada ya miezi miwili mitatu atajua nini maana ya diplomasia, na hizi sarakasi za northern corridor sijui na nini hatutazisikia tena...
 
Sidhani, Kenya siku zote wamo kwenye jumuia strategically, siyo kwa sababu za kulipenda eneo lote la afrika ya mashariki na watu wake bali ni kwa jinsi gani wataneemeka na jumuia hiyo. Hiyo Northern corridor ni programa ambayo strategically ni nzuri sana kwa Kenya kuliko Rwanda na Uganda, kwa hiyo sidhani kama Uhuru na Kenya wana cha kukosa katika project hiyo. Tatizo kubwa la Uhuru litatokana na uroho kwa vile anajua pia kuwa Kenya itafaidika zaidi ikishirikiana na Tanzania kuliko hao wengine. Kenya ina investment nyingi sana Tanzania kuliko nchi nyingine yoyote nje ya Kenya. Uhuru mwenye ana investments nyingi sana za maziwa katika Tanzania kuliko sehemu nyingine yoyote. Kwa hiyo analofanya hapo ni kuuma na kupulizia, ni wajibu wa watanzania kujua ni lipi la maana kwa Tanzania. Iwapo Kenya wangekuwa wanaitakia mema Tanzania wasingejenga kiwanja kikubwa sana cha ndege karibu sana na KIA ilihali wakijua kuwa KIA ndiyo gateway ya watalii kwenda mbugani, wanataka KIA ife kusudi watalii wawe wanapitia Kenya iwapo mipaka itakuwa iko wazi. Sasa hivi ananusa uwezekano wa Tanzania kuweka ugumu wa kuvuka mipaka yake kwa hiyo anajaribu kutupooza tusiwawekee mchanga kwenye kitumbua caho.
 
kuna Mkenya mmoja nilikutana naye akasema wana wasiwasi kama Uhuru yuko sawa upstairs
 
huyu jamaa ameingia Urais kama ujiko tu, sidhani kama anatosha
Sidhani, Kenya siku zote wamo kwenye jumuia strategically, siyo kwa sababu za kulipenda eneo lote la afrika ya mashariki na watu wake bali ni kwa jinsi gani wataneemeka na jumuia hiyo. Hiyo Northern corridor ni programa ambayo strategically ni nzuri sana kwa Kenya kuliko Rwanda na Uganda, kwa hiyo sidhani kama Uhuru na Kenya wana cha kukosa katika project hiyo. Tatizo kubwa la Uhuru litatokana na uroho kwa vile anajua pia kuwa Kenya itafaidika zaidi ikishirikiana na Tanzania kuliko hao wengine. Kenya ina investment nyingi sana Tanzania kuliko nchi nyingine yoyote nje ya Kenya. Uhuru mwenye ana investments nyingi sana za maziwa katika Tanzania kuliko sehemu nyingine yoyote. Kwa hiyo analofanya hapo ni kuuma na kupulizia, ni wajibu wa watanzania kujua ni lipi la maana kwa Tanzania. Iwapo Kenya wangekuwa wanaitakia mema Tanzania wasingejenga kiwanja kikubwa sana cha ndege karibu sana na KIA ilihali wakijua kuwa KIA ndiyo gateway ya watalii kwenda mbugani, wanataka KIA ife kusudi watalii wawe wanapitia Kenya iwapo mipaka itakuwa iko wazi. Sasa hivi ananusa uwezekano wa Tanzania kuweka ugumu wa kuvuka mipaka yake kwa hiyo anajaribu kutupooza tusiwawekee mchanga kwenye kitumbua caho.
 
Viongozi wa Kenya wanajua FIKA kile kitu Wananchi wa Kenya wanahitaji kwenye haya mashirikiano......hivyo ukiwasikia wanashirikiana na Uganda na Rwanda ujue wao kuna target moja au mbili tayari wanakamilisha.........sisi wengine tunaingia kwenye haya ashirikiano huku hatujui Wananchi wetu wanahitaji nini......

Kule mipakani ndio utajua/utaona ni kwa jinsi gani sisi tumezubaa kwa shughuli za uchumi....kazi kupiga domo la siasa kila kukicha......Wakulima wetu kule mipakani kwao ni bora wakauza mazao yao nchi jirani kuliko kuuza ndani ya nchi......sasa angalia rishwa zinavyotembea kule........

Mbali na Uhuru kuwa na biashara zake Tanzania........lakini pia ana kinyongo fulani kwa sababu ya mambo yanayomuandama kule The Hague......
 
Sidhani, Kenya siku zote wamo kwenye jumuia strategically, siyo kwa sababu za kulipenda eneo lote la afrika ya mashariki na watu wake bali ni kwa jinsi gani wataneemeka na jumuia hiyo. Hiyo Northern corridor ni programa ambayo strategically ni nzuri sana kwa Kenya kuliko Rwanda na Uganda, kwa hiyo sidhani kama Uhuru na Kenya wana cha kukosa katika project hiyo. Tatizo kubwa la Uhuru litatokana na uroho kwa vile anajua pia kuwa Kenya itafaidika zaidi ikishirikiana na Tanzania kuliko hao wengine. Kenya ina investment nyingi sana Tanzania kuliko nchi nyingine yoyote nje ya Kenya. Uhuru mwenye ana investments nyingi sana za maziwa katika Tanzania kuliko sehemu nyingine yoyote. Kwa hiyo analofanya hapo ni kuuma na kupulizia, ni wajibu wa watanzania kujua ni lipi la maana kwa Tanzania. Iwapo Kenya wangekuwa wanaitakia mema Tanzania wasingejenga kiwanja kikubwa sana cha ndege karibu sana na KIA ilihali wakijua kuwa KIA ndiyo gateway ya watalii kwenda mbugani, wanataka KIA ife kusudi watalii wawe wanapitia Kenya iwapo mipaka itakuwa iko wazi. Sasa hivi ananusa uwezekano wa Tanzania kuweka ugumu wa kuvuka mipaka yake kwa hiyo anajaribu kutupooza tusiwawekee mchanga kwenye kitumbua caho.
hamna airport inayojengwa karibu na KIA yaani ile ya Taveta! Ile ilikuwa April fools gimmick
 
Back
Top Bottom