Ulimwengu wa 3D Hadi Ulimwengu wa 5D🔰

Ulimwengu wa 3D Hadi Ulimwengu wa 5D🔰

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
🔰Ulimwengu WA 3D Hadi Ulimwengu wa 5D🔰
1737670190345.jpg


👉Hivi sasa ulimwengu wetu umegawanywa katika vipimo tofauti ambavyo unaweza kuchagua na kuamua ni njia gani unataka kwenda. Katika makala hii, napenda kueleza umuhimu wa kuchagua mwelekeo sahihi ili kuishi chini ya dhiki na maisha ya afya.

🧿🧿🧿Ulimwengu wa 3D🧿🧿🧿

🗣️Watu wengi wanaishi na ufahamu wa 3D: matendo yetu yanaongozwa zaidi na hofu, ukosefu, maisha, ujinsia, utu, ushindani na wivu.

🗣️ Mara nyingi tuko katika hali ya wasiwasi kwa kile tunachofanya au tusichokuwa nacho. Ili kusonga zaidi ya 3D, tunahitaji kuinua fahamu zetu na kuomba mwelekeo wa kiroho.

🗣️ Tunapofanya kazi kutokana na ufahamu wa kimwili (3D), kwa kawaida tunapuuza hali yetu ya kiroho. Huenda tusiwe na imani yoyote ya kiroho, au tunaweza kukwama katika mafundisho ya kidini.

🗣️ Tuna mwelekeo wa kufikiria kila kitu kuwa cheusi au cheupe ,kizuri au kibaya.

🗣️ Tunaonyesha ujuzi mdogo wa nguvu ya ulimwengu inayofanya kazi katika maisha yetu.

🗣️ Tunanaswa na mchezo wa kuigiza wa kila siku, uvumi, mahusiano ya matusi, migogoro na tunaweza kuunda hali zenye uchungu kwa urahisi sana.

➡️Mara nyingi tunaweza kulaumu kila mtu kwa kile ambacho ni chetu na tunapaswa kumiliki.

➡️Pia, uwajibikaji wa kibinafsi kwa kiasi kubwa zaidi huwa unakosekana tunapofanya kazi chini ya uhalisia wa 3D pekee.

👁️‍🗨️👁️‍🗨️👁️‍🗨️ ULIMWENGU WA 4D👁️‍🗨️👁️‍🗨️👁️‍🗨️

🗽🗽Tunapokuwa na changamoto ya maisha au shida na kupokea ‘tahadhari ya uamsho’ ili kuanza kufahamu mawazo yetu ya 3D na kuhamia njia ya kuishi ya 4D.

🗽🗽 Utaanza kuelewa kuwa sisi ni kiumbe anayefahamu kuwa na uzoefu wa mwili wa mwanadamu.

🗽🗽Kuishi kwa mtazamo wa 4D kunamaanisha kuwa bado unaishi kimwili katika 3D na unafahamu na unafanya kazi zako vizuri lakini pia unazingatia upendo, kushiriki, huduma, huruma, nguvu ya nafsi na akili na uwezo wa kuvutia na kuunda kile unachotamani.

🗿 Kuishi katika ulimwengu wa 3D, na ufahamu wa 4D ni kawaida kwa watu wengi ambao sasa wako kwenye njia kamili ya kiroho.

♻️♻️♻️♻️ Ulimwengu wa 5D♻️♻️♻️♻️

🗣️Kisha tunakuja kwenye ulimwengu wa 5D: kwa kweli tuna huruma kubwa kwa viumbe vyote vilivyo hai. Huwezi kula Wala kuua kiumbe chenye uhai kiwe mdudu n.k

🗣️ Ufahamu wako unapofanya kazi katika 5D, ulimwengu mwingi wa 3D unakaribia 'kutoonekana' kwako.

🗣️ Huenda usione watu wengine, ambao wanafanya kazi kwa kiwango cha 3D pekee. Vivyo hivyo, watu hawa wanaweza wasikuone pia. Ndiyo maana mahusiano mengi hubadilika mara viwango vyetu vya ufahamu vinapopanda.

🗣️Pia utapata kwamba kile kilichokuwa kikikusumbua kuhusu ulimwengu wa 3D kinakuwa chini ya lengo lako, kwani badala yake, unalenga kwa dhati kuongoza maisha yako bora ili uweze kuinua sayari na wale wote unaokutana nao.

🗣️ Ni kama uko kwenye 'misheni' unapofanya kazi kutoka 5D.

Umejitolea, unawajibika, na uko tayari kutumikia kwa ujumla.

JE, KUNA NAMNA GANI YA KUISHI KATIKA ULIMWENGU WA 3D UKIWA KATIKA MAZINGIRA YA 5D?

➡️Ulimwengu wako wa kila siku utaonekana mara nyingi sawa kwako, lakini utazingatiwa zaidi katika kila kitu unachochagua kufanya. Baadhi ya watu wanaona kuwa mazingira yao yanapata hisia laini (zaidi ya ukali) wanapozingatia 5D na kutokana na ufahamu wa kiroho.

➡️Kuna uwezekano mkubwa kwamba bado utakuwa nje ya dunia ukifanya kazi, unaishi, unahusiana, unapendana na unapokea kila siku - kama vile ulivyokuwa ukifanya siku zote.

➡️Ili kuhama kuelekea dunia mpya, niliamua kuchagua furaha, kuzingatia hisia zangu mwenyewe, kuwa na ufahamu wa hisia zangu, na kuchunguza uzuri wa kipindi hiki cha mpito.

Ninyi nyote muwe na furaha na muwe na utulivu

🧿🧿🧿🧿🧿🙏🙏🙏🙏🧿🧿🧿🧿🧿🧿
 
💥💥💥FAHAMU KUHUSU NDOTO💥💥💥💥
☑️Maana ya ndoto;

👉Ndoto ni matokeo ya matendo yetu ya siku wakati wa kupumzisha mwili wa kifizikia.

👉Ndoto ni hali inayotokea kwa mtu wakati anapokuwa katika usingizi mzito; hiyo hali ni udhihirisho wa kama hayupo usingizini na anafanya mambo fulani ya kawaida (yaliyo dhahiri) ama mambo yasiyo ya kawaidi (yasiyo dhahiri)

✔️Mambo dhahiri; Haya mambo ni kama kuota ndoto ambamo muna kama watu, wanyama waliopo duniano na vitu vya kawaida vilivyopo duniani.

✔️Mambo yasiyo dhahiri; Haya ni mambo ya ajabu, mara nyingi hayapo katika ulimwengu wa kawaida. Unaota nyoka anabadili umbo anakuwa na umbo la mpira wa miguu, unaota wanyama wa kutisha sana, ama viumbe au vitu ambavyo havipo kabisa katika ulimwengu huu wa mwili na nyama.

👉Ndoto ni mfululizo mawazo ,picha au hisia ambazo hutokea akilini kupitia nguvu za asili.

🔔🔔🔔AINA ZA NDOTO🔔🔔🔔

1.NDOTO ZA KAWAIDA
👉Hizi hutokana na wasiwasi au hofu ambayo inatawala akili ndogo tambuzi.

mfano:
hali sumbufu ya maisha yako au sehemu uipendayo.
👉ndoto hii ni rahisi kuitafsiri kwa kutumia akili ndogo tambuzi.

2.NDOTO ZA UJUMBE

👉Hizi ni ndoto za mafumbo,picha na alama
👉ndoto hii huongozwa na roho,malaika au mtu umpendaye aliyefariki.
👉huzungumza na sisi na kuonyesha matendo nje ya maisha ya kawaida.
👉ndoto hii huonyesha watu,mazingira na maeneo yasiyoyakawaida.
👉kwahiyo katika ndoto hii sisi bi watazamaji wa matukio

📢ili uweze kutafsiri ndoto hii basi lazima utambue code za siri.

3.NDOTO ZA KINABII.
👉Hizi ni ndoto zinazokutahadharisha juu ya matukio yajayo.
👉matokeo hayo huweza kuwa mazuri au mabaya ila lengo lake ni wewe kujiandaa na kuchukua hatua.

📣WALIOOTA NDOTO KATIKA BIBLIA📣

1. Mfalme ABIMELEKI wa Gerari (Misri):
📚 Mwanzo 20:3.

Mungu alimjia Abimeleki katika NDOTO usiku, siku ambapo alilala na mke wa Ibrahim, Sara… Mungu akamjia mmataifa (Gentile) kwa ndoto kinyume cha kawaida, kwasababu ya mtu wake mpendwa Ibrahim.

“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.”

2. YAKOBO mwana wa Isaka;
📚Mwanzo 28:12

Yakobo aliota NDOTO yake akiwa ameondoka nyumbani, akafika sehemu iitwa Luzu ambapo yeye akapabatiza jina la BETHELI kwa maana ya kuamini kwamba ndipo penye lango la Mbinguni. Aliota ndoto ya KUBARIKIWA KWAKE.

“Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.”

Yakobo akaota NDOTO nyingine tena akiwa katika machungo ya mifugo wa mjomba wake Laban. Pale walipokubaliana na Laban kuhusu mshahara wa kuchunga… Bado Yakobo aliota ndoto ya BARAKA.

“Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka.” 📚📚Mwanzo 31:10

3. LABAN mjomba wa Yakobo, na mkwe.
📚📚Mwanzo 31:24

Laban akiwa katika kumfuatia Yakobo baada ya kuondoka na miungu yake/vitu vya thamani na kwa kutoroka… Mungu alimjia huyu mtu wa mataifa tena kinyume na kawaida ila kwa manufaa ya mwanawe Yakobo. Alimwonya asije akamgusa Yakobo.

“Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.”

4. YUSUFU mwana wa Yakobo;
📚📚Mwanzo 37:9

Yusufu akiwa na nduguze 12 kwa baba yao Yakobo; aliota ndoto ya ukuu wake juu ya watu wa kwao ikiwa ni pamoja na Baba na mama. Aliota ukuu wake na Kubarikiwa kwake.

📚📚Mwanzo 37:5

“Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;”

“Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.”

5. MWOKAJI na MNYWESHAJI wa Ufalme wa Misri;
📚📚Mwanzo 40:5-6

👉Hawa wawili wakiwa wamefungwa gereza moja pamoja na Yusufu; waliota ndoto katika usiku mmoja. Ni ndoto hizo ndizo zilizokusudiwa na Mungu kwaajili ya kumtoa kifungoni Yusufu na kuliinua jina lake.

“Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika.”

6. FARAO, Mfalme wa Misri:

📚📚Mwanzo 41:1

Farao aliota ndoto, tena mara mbili katika usiku mmoja na akahitaji fasiri ya ndoto yake. Mungu alikusudia kumwotesha ndoto huyu mpagani kwaajili ya kuliinua jina la Yusufu na kutimiza ile ndoto ya Yusufu kuwa mkuu juu ya watu wa kwao.

“Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto; na tazama, amesimama kando ya mto.”

“Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema.”📚 Mwanzo 41:5

“Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.” 📚Mwanzo 41:7

7. MMIDIANI na mwenzake;

📚📚Waamuzi 7:13-15

👉Mungu aliikusudia ndoto ile ambayo mmidiani aliiota na kufasiriwa na mwenzake tena kwa ufunuo wa Mungu; lengo lake ni kumjaza imani Gideon na jeshi lake dogo, hakika Gideon alijaa imani kama makusudi ya NDOTO.

“Hata Gideoni alipofika, tazama, palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa akimhadithia mwenziwe ndoto, akasema, Tazama, naliota ndoto, na tazama, mkate wa shayiri ulianguka katika kambi ya Wamidiani, ukafika hata hema moja, ukaipiga hata ikaanguka, nao ukaipindua, hata ikalala chini. Mwenzake akamjibu akasema, Habari hii haikosi kuwa upanga wa Gideoni, mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote katika mkono wake. Ikawa, aliposikia habari ya ile ndoto, na kufasiriwa kwake, akasujudu; akarudi katika jeshi la Israeli akasema, Inukeni, kwa maana Bwana amelitia jeshi la Midiani mikononi mwenu.”

8. Mfalme SULEMANI wa Israel;

Kwa hakika wapendwa tunafahamu sana kuwa Suleiman alikuwa Mfalme mwenye hekima sana na tajiri aliyebarikiwa mno… Na tunajua alipewa fursa (favor) na akaomba kupewa HEKIMA. Fursa alikuwa amepewa “kwa njia ya NDOTO.” Nachelea kusema wengi wetu tumepoteza baraka nyingi kwasababu ya kupuuza ndoto ama kukosa ujasiri katika ndoto.

“Na huko Gibeoni Bwana akamtokea Sulemani katika ndoto ya usiku; Mungu akamwambia, Omba utakalo nikupe.” 1 Wafalme 3:5

9. Mfalme NEBUKADREZA wa Babeli;
📚📚Danieli 2:3

Mfalme huyu mpagani aliota ndoto na akataka fasiri bila kuwaambia ndoto, alisema ameisahau; alipoona hawajui akataka kuwachinja… Ndipo Daniel jina lake likasimama. Hapa utagundua kuwa pamoja na maana nyingine, ila Mungu alikusudia kumwinua mwanae kwa njia hiyo. Mfalme aliota kuhusu ile “sanamu kubwa ya dhahabu safi inayong’aa sana”.

“Mfalme akawaambia, Nimeota ndoto, na roho yangu imefadhaika hata niijue tafsiri yake.”

10. DANIEL aliyeitwa Belteshaza;
📚📚Danieli 7:1

Daniel aliota ndoto muhimu sana katika utumishi wake. Ndiyo hii ndoto iliyomfanyabkuitwa kwa jina NABII. Alioota ndoto nayo akaiandika ndiyo inayoweka mlango wa saba wa kitabu chake. Ni ndoto ya ufunuo wa nyakati zilizopo kuendelea hadi zijazo.

“Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.”

11. YUSUFU mume wa Maria;
📚📚Mathayo 1:20

Mungu alisema na Yusufu kwa njia ya NDOTO hata mara mbili. Alimwambia asimwache mchumba wake Maria kwaajili ya mimba. Na wakati mwingine akamwambia kuhusu kifo cha Herode na kwamba sasa warudi nyumbani kutoka uhamishoni.

“Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.”

“Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,” 2:19

12. MAMAJUSI wa Mashariki;

Hawa walipokwenda kwenye ufalme wa Herode aliwaambia mkimwona mfamle ajaye mrudi kunipasha habari nikamsabahi nikampe nami zawadi. Lakini Mungu akasema na hawa mamajusi kwa njia ya NDOTO kuhusu dhamira ya Herodi na kwamba waondoke kwa kupitia njia nyingine.

“Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.” Mathayo 2:12

📚📚Mathayo 2:13

“Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.”

📚13. MKEWE Pilato;

📚Akiwa katika kutaka kutoa hukumu juu ya Yesu wa Nazareth, Pilato mkewe alimjia na kumuonya kutokunyoosha mkono wake juu ya Yesu kwasababu anakiri kupatabsana tabu usiku katika ndoto ya kwamba huyu Yesu kwamba ni mtu wa Haki na wala hana hatia. Nadhani utakumbuka ni Pilato ndiye aliyesema “mimi sioni hatia juu ya mtu huyu, nimenawa mikono yangu na damu yake isiwe juu yangu na nyumba yangu.”

📚“Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.” Mathayo 27:19

💥💥Tofauti Ya Ndoto Na Maono:💥💥💥💥

👉Zipo namna tatu za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Namna hizo ni kwa NDOTO na MAONO na MAOMBI. Kwa maana hiyo NDOTO na MAONO zote ni njia za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Lakini pia NDOTO ni ufunuo wa picha na matukio; ilhali MAONO pia.

📚Tofauti yao inakuja kwamba MAONO humpata mtu akiwa macho kabisa, ubongo wake ukiwa active wakati NDOTO inamtokea mtu akiwa katika usingizi mzito sana, mwili umepumzika na ubongo unafanya kazi.

📚Ukisoma Biblia utakuta karibu maeneo yote; ndoto na maono yametumiwa kwa namna moja. Unaweza kukuta ndoto inaitwa maono ama maono yakaitwa ndoto. Lakini pia haijaathiri maana halisi ya tofauti zao.
...............

.
🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom