Ulishamuona your first love?

hivi kuna mtaa kule uswahili enzi zile ambao ulikosa jumba bovu? ila bahati mbaya jumba bovu la mtaani kwetu lilikuwa na mashetani....lol

Enzi zile hasa kwa sisi tuliozaliwa na kukulia Dar sidhani kama Uswazini kulikuwa kuna mtaa uliokuwa hauna jumba bovu. Unajua watu walikuwa wanaanza kujenga halafu sijui nini kinatokea ujenzi unaishia njiani. Basi hiyo ilisababisha kuwepo na majumba mabovu kibao. Nadhani wengi wa wamiliki wa hayo majumba walikuwa ni wale wahujumu uchumi na kilipowaungulia basi wakashindwa kuendelea na ujenzi wao.

Mijumba mibovu mingi ya mtaani kwetu ilikuwa na kenge kibao na mimbwa koko.
 
Mh miye nilikutana naye std 5, alìhamia shuleni kwe2 enz hzo nikiwakimbiza mbaya academically, alikuwa karibu kwan mara nying nilikuwa nikimsaidia hesabu, shule nzma wakajua kwamba cc ni wachumba. Std 7 tulifaulu kwenda shule moja ya day, baadaye alihama na miye nikahama. Nilimwambia nampenda baada ya kwenda mbali, hakunijibu ki2. Urafk ulizd kupungua, na uislamu wake ndo uliofanya nimkose. Now nasikia yupo AIAA
 
Mzuanda
Wewe ni mkareee!
Hii ni stori yangu, nilichelewa kuingia darasani (darasa la kwanza) kidogo wakati wenzangu walikuwa weshaanza masomo.
Nilikuwa na miaka 8, siku niliyoingia nilipangiwa benchi la nyuma kabisa, wakati tunataka kutoka siku hiyo nilimuona huyo mtoto.
Anaitwa "Nic", nilipata vihisia ambavyo sikuwahi kijisikia hivyo kabla mbele ya watoto wakike.
Nilimfuata, nikamwambia "wewe ni mchumba wangu"... akacheka tu!
Toka siku ile takaanza uchumba rasmi, na darasa lote lilifahamu hilo.
Niliendelea nae kwa mpaka darasa la saba japo hapo katikati kuna vijimambo vilijitokeza so kukawa kuna kuachana na kurudiana.
Darasa la saba aliniandikia barua rasmi ya kunitamkia kuwa "ananipenda" unaweza ku-imagine hiyo barua... lol.
Mazingira yalibana hatukuwezaga ku-du.
Baada ya primary, tulitengana!
Tulikuja kuonana wakati yupo chuo kikuu (mwaka wa pili).
Ofcoz tulianzia tulipoishia, japo hatukufika mbali sana sababu anamchumba wake. Huwa tunakumbushia mara moja moja kwa heshima ya hisia zetu lol
 

hapo kwenye red umenimaliza.ina maana hakuna kuachana?
 

dearest nina mazungumzo na wewe....naona kama siku zako za kuhesabu zimeisha.....l.o.l
 
mimi nakumbuka nilikuwa standard 7,sielewi zilikuwa feelings au laa,ila tulikuwa tunaangaliana sana na kijana mmoja, tulisoma wote madarasa tofauti.ndugu zake walikuwa wananitania mchumba wa fulani.ila nilikuwa sipendi huo utani.ajabu tulikuwa hatuongei zaidi ya kuangaliana tu.na tulikuwa jirani.tukionana ni kuangaliana tu.baada ya miaka mingi bado anaishi kwao,nikienda kumsalimia mama huwa namuona,kuna siku tulikutana kwani ni majirani,aliniambia wewe ulinikataa,na kaka ake aliniambia kwa nini ulimkataa mdogo wangu?nabaki kushangaa kwani hakuwahi kuniambia neno lolote lile.kwa sasa namuona mtu tu wa kawaida.visichana vya sasa,darasa la 4 wana ma boyfriend.na wanajua kila kitu
 
Da...siku hizi ameolewa na mchungaji tena jamaa ni rev. wa kanisa letu ana watoto watatu. Tulipendana sana tulipokuwa primary school, na tulipoteana baada ya std seven. Tulionana tena wiki chache kabla hajaolewa, aliniahidi tuonane faragha na tufanye farewel.....niliogopa na nikaingia mitini, alichukizwa sana na mimi kuingia mitini.
So kila nikienda kanisani jpili nikimwangalia huyu mchungaji napata so much memories! Mkewe nae haishi kuniangalia hata tukiwa humo kanisani. Nahisi soon nitahamia kanisa jingine...ili kuepusha balaa kama ktk yale ya ile movie ya "Preacher's Wife"
 
dearest nina mazungumzo na wewe....naona kama siku zako za kuhesabu zimeisha.....l.o.l

Hahahahhaa....dearest ntahitaji mtu wa kuniwakilisha kwenye mazungumzo???Naogopa kukutwa na hatia!!!Alafu we mbona hutuambii kuhusu yule aliyekua anakutungulia mapera....!
 
Tabia mbaya kutembea na mke wa mwenzako....kama mlipendana sana simngeoana???
 
Hahahahhaa....dearest ntahitaji mtu wa kuniwakilisha kwenye mazungumzo???Naogopa kukutwa na hatia!!!Alafu we mbona hutuambii kuhusu yule aliyekua anakutungulia mapera....!

Mapera yanatunguliwa au yanaanguliwa?
 

You should have initiated a chain reaction right away. Remember, a golden chance never come twice! I hope u meet him someday coz it seems u will be the happiest woman alive!
 
My childhood crush was kwa huyu kijana sijui ilikuwaje alikuwa mkubwa sana kuliko mimi,kama 18-21, na mie nilikuwa 13 yaani nilimpenda huyu mkaka sijawahi ona mpaka nikawa napoteza hamu ya kula, na kwenda nyumbani ni lazima upite kwao yaani nikimuona yupo nje najikwaa hata mara nne. sikuwahi kumwambia na wala yeye hakuniambia mpaka tulihama mtaa na mpaka leo sijawahi muona tena
 
Duh! Mmenikumbusha mbali sana!! Niliewahi kuwa nae utotoni mpaka darasa la saba na nilimpenda kweli ila nilipoingia o-level tukapoteana coz nilihama mkoa!!

Nilikuja kukutana nae kwenye semina moja hivi Morogoro inayohusu watumishi wa umma mwaka jana mwezi wa tisa!!! Hahahahahaaaaaa!!!! Nacheka coz kilichotokea sikuamini, mbele za watu alinikumbatia na kuniuliza kwa nini nilimkimbia huku analia!!!??

Nashindwa nisemeje lakini kilichofuata ni alihamishia mizigo yake room kwangu na kuwa pamoja kipindi chote cha semina na kufanya kile tulichoshindwa enzi za utotoni. Nilikuja gundua badae kumbe ni mke wa mtu ana ana mtoto mmoja

Yeye amefanikiwa saaaana ni msomi pia na anavutia sana!!!! Kama si kuolewa.........!!!? Tunaendelea kuwasiliana mpaka leo.
 
Duh kwa hiyo bado mnakumbushia???
 
Namtafuta nikimpata na kama yuko single
mmmhhh ..

Sitaki mtu yeyote anipe
lecture kwa nililosema...
asanteni
AD
 


thanks kiongozi!!!!
 
mlivyofika huko mkabanjua amri ya 6?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…