Ulishawahi kujiuliza maswali haya na kuapata majibu? Part I

Ulishawahi kujiuliza maswali haya na kuapata majibu? Part I

Tony Laurent

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
5,606
Reaction score
7,032
Tokea umejitambua je, ulishakaa chini na kujiuliza maswali haya? Kama ulishawahi kujiuliza. Je, ungependa kutushirikisha majibu uliyopata? Karibuni.



  1. Je, kuna tofauti yoyote kati ya mtu kuishi duniani na kuwepo duniani
  2. Kuna kitu chochote umekiweka moyoni mwako iwe kwa muda mfupi au mrefu ambacho usingependa kiendelee kuwepo?
  3. Je, unafurahia jinsi ulivyo? Unajikubali au ungependa kuwa kama mtu fulani?
  4. Mara nyingi tumezoea kusema mtu hujifunza kutokana na makosa. Kama tunajifunza kutokana na makosa kwanini tunaogopa kufanya makosa?
  5. Kama maisha ni mafupi kiasi tunachofikiri, kwanini wakati mwingine tunalazimika kufanya mambo au kazi tusizozipenda na kujikuta tunatamani mambo au kazi ambazo tunashia kutokuzifanya kabisa maishani mwetu?
  6. Endapo ungepewa uwezo wa kuangalia yaliyomo ndani ya moyo wa adui yako,unafikiri ungekuta nini ambacho ni tofauti na kilichomo ndani ya moyo wako ?
  7. Kwanini unafikiri kuishi kwako au kuwepo kwako duniani ni muhimu?
  8. Leo ingekuwa ndio siku yako ya mwisho kuwepo duniani, je, bado ungefanya kile ulichokuwa umekusudia kukifanya leo?
  9. Je, ni kitu gani unachofikiria kinakukwaza kufikia malengo uliyojiwekea katika maisha yako? Na unafanya jitihada gani kukiondoa?
  10. Kitu gani unachokijua sasa ambacho unajuta kwa kukijua katika maisha yako?
 
Maswali mengi ni mepesi mepesi, wala hayahitaji intelijensia...
 
Back
Top Bottom