Ulitumia mbinu gani kukabiliana na jambo gumu la kukukatisha tamaa mpaka ukalishinda?

Ulitumia mbinu gani kukabiliana na jambo gumu la kukukatisha tamaa mpaka ukalishinda?

JF Toons

Digital Art by JF
Joined
Feb 19, 2024
Posts
33
Reaction score
73
mvumilivu.PNG

Katika harakati za kupambana na maisha, tunakutana na chanamoto hapa na pale ambazo wakati fulani unaweza kuona dunia imeisha na hakuna pakutokea, lakini amini kwamba hayo magumu unayopitia yana mlango wa mafanikio, usikate tamaa sababu kuna siku utapata ufumbuzi na magumu yote yabaki kama historia na funzo kwako.

Wahenga walisema mvumilivu hula mbivu, lakini pia mchumia juani hulia kivulini.

Ulifanyaje kukabiliana na jambo gumu la kukukatisha tamaa mpaka ukalishinda?
 
Jambo la kwanza ni kumuamini Mungu na kujiamini kuwa utashinda katika kila hatua kupitia yeye, pambana kuhakikisha unashinda yale yote magumu yaliyo mbele yako kwa sababu dawa ya tatizo ni kukabiliana nalo.
Hii ni kweli kbs mungu n Kila kitu hasa ukimtanguliza kwa Kila jambo iwe gumu ama furaha..
 
Kama huna choice, inabidi upambane mwenyewe. Ukate usikate tamaa, utajijua.
 
Ulifanyaje kukabiliana na jambo gumu la kukukatisha tamaa mpaka ukalishinda?
Sikupoteza muda kuendelea kulitafuta balaa nilitafuta uchochoro nikala Kona baada ya hapo nikajikuta nimeingia mitini,
 
Unaamka asubuhi mtoto analia njaa...ndani huna kitu....madeni kila duka na genge...umebadilisha njia mpaka huna pa kupita....nguo chafu huna sabuni wala maji....kesho kodi inakwisha...simu haina salio....kila unayemuona ni kama vile anakukwepa hataki japo kukusikiliza....
Na jana ulilala njaa.....
 
Back
Top Bottom