Uliza swali lolote kuhusu jinsi ya kutumia mtandao kupata wateja!

Video haifunguki na YouTube naambiwa video not found
 
Nina digital copy ya poetry book(english), tamthiliya ya kiswahili na digital magazine(kiswahili na kiingereza inayohusu mada mbalimbali, huwa nalitoa kwa mwezi mara moja. Vipi naweza badilisha yote haya kuwa biashara ktk mtandao?
 
Nina digital copy ya poetry book(english), tamthiliya ya kiswahili na digital magazine(kiswahili na kiingereza inayohusu mada mbalimbali, huwa nalitoa kwa mwezi mara moja. Vipi naweza badilisha yote haya kuwa biashara ktk mtandao?

Inategemea.

  1. Walengwa ni kina nani? (target audience yako) na
  2. Ni kubwa kiasi gani? (Hivi sasa una wangapi wana consume information zako)?
 
Sijajua namna ya ku-attach pictures na kuzituma, hasa humu jf, nafanyaje? Coz miongoni mwa wateja wangu wamo jf
 
Mkuu sisi tunao jishughulisha na mambo ya ufugaji tunaweza pata msaada toka kwako? mfano mimi natotoresha vifaranga. nipo morogoro soko limekuwa shida!
 
Mkuu sisi tunao jishughulisha na mambo ya ufugaji tunaweza pata msaada toka kwako? mfano mimi natotoresha vifaranga. nipo morogoro soko limekuwa shida!
kampuni yako ina brand?
 
Ni kwa namna gani naweza kupata watu wa kunisaidia plan zangu za kibiashara mtandaoni..? Mfano nataka kufuga kuku sasa naomba msaada wa kipesa mtandaoni
 
Ni kwa namna gani naweza kupata watu wa kunisaidia plan zangu za kibiashara mtandaoni..? Mfano nataka kufuga kuku sasa naomba msaada wa kipesa mtandaoni
Samahani. Sina jibu la swali lako. Kama una bidhaa / huduma unayouza tayari naweza kukushauri namna gani ya kutumia mtandao kuwafikia wateja wako watarajiwa.
 
We mkali
 
Hivi ukifungua Facebook pages, kama sports, mitindo,.... Unaweza kutengeneza Dolla? Na unatengenezaje?
 
Kila nikifungua page huwa niki google ile page iliyoko fb sihioni
 
Hivi ukifungua Facebook pages, kama sports, mitindo,.... Unaweza kutengeneza Dolla? Na unatengenezaje?

Pesa nyingi hutengenezwa kwa kuuza bidhaa au huduma inayohitaji kwenye soko.

Kama Facebook page ni kwa ajili ya biashara yenye bidhaa au huduma unazotoa basi utaweza kutengeneza pesa.

Kama kurasa yako ni kwa ajili ya ku linki na blogu yako ya habari au riyadha na unategemea kutengeneza pesa kupitia matangazo, utahitaji traffic kubwa sana jambo ambalo sishauri ufanye unless wewe na mwandishi hodari na unatengeneza makala mazuri yenye mvuto.

Option nzuri ni kutumia blogu kama njia ya kufanya mauzo ya bidhaa au huduma za biashara yako.

Kama huna bidhaa au huduma za kuuza, basi tafuta kwanza ikisha tumia blogu yako kukupelekea kufanya mauzo.
 
Mimi nina kampuni yangu na nimeipromote kwenye social media je napataje wateja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…