Pre GE2025 Umaarufu wa CHADEMA waongezeka mara dufu, Vyombo vya habari vya Kimataifa vyaripoti kushikiliwa viongozi wao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kauli gongana toka polisi

Polisi: Hatujapiga marufuku mikutano ya hadhara​

August 12, 2024

Msemaji wa Polisi, DCP David Misime

JESHI la Polisi limesema halijapiga marufuku kufanyika mikutano ya nje ya hadhara na ile ya ndani ili mradi inafuata matakwa ya sheria za nchi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 12 Agosti 2024 na Msemaji wa Jeshi hilo nchini, DCP – David Misime, killichopigwa marufuku ni mkusanyiko uliokuwa umeitishwa na Viongozi wa Chadema huko Jijini Mbeya kwa kivuli cha kuadhimisha Siku ya Vijana Duniani.

Hayo yanajiri wakati Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) likiwa limeratibu kongamano la maadhimisho ya siku ya vijana duniani lililotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya.

Maadhimisho hayo ambayo yalikuwa yafanyike leo Jumatatu, mgeni rasmi alitarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
 
Hivyo vyombo vya habari vya nje n mara ya kwanza kuripoti habari hizo na lipi likatokea?
 
Maridhiano na maelewano na mageuzi ya uongo. Rais mwongo. Alijisemea tu hakujua maana yake nini.

.....reconciliation sijui reform.... kajiongelea tu... wishy washy empty talk ambazo wala hakujijua anasema nini
 
Kwahiyo hivyo vyombo vya habari unavyoviita vya kimataifa ndio vitakuja kuipigia kura chadema?! Yaani hadi Leo chadema Bado wanatafuta umaarufu badala ya kutafuta kushika Dola?! Na unadhani hata chadema iwe maarufu ndio itakuwa maarufu kuishinda CCM ambayo imetawala tangu 05/02/1977 baada ya ASP na TANU kuungana.?! CCM ndio chama maarufu kushinda vyama vyote TZ.
 
Nchi yako ni omba omba, huku kwenye mataifa ni noma
 
Ndani ya Chama cha CCM wanamhujumu! na kumchafua mama wetu.
Sio kweli huu nao ni ujinga mwingine,nani anamteua IGP? Unadhan rais akitamka asikamatwe kiongoz yeyote wa upinzani bila kosa kuna polisi atathubutu? Tatizo linaanzia juu
 
Umaarufu wa chama chochote cha siasa NI ndani ya nchi ambalo Ndiko kwenye wapiga kura sio nje ya nchi

Mfano ukipita mitaani asilimia kubwa hakuna mwenye habari hata ya kujua kuwa kuna viongozi wa Chadema wamekamatwa .Watu wanaendelea Tu na shughuli zao za kutafuta maisha hawana habari za Chadema

Hata humu Jamii Forums angalia post za Chadema zinazopostiwa views na reply chache mno

Wanaoona Tukio hilo NI kubwa NI baadhi Tu ya wana chadema tena wachache mno Sana Sana NI viongozi baadhi wa Chadema na hao baadhi waliokamatwa wachache ndio wana post post humu na vi ID ID tofauti tofauti lakini all in all response ya watu humu Jamii Forums NI ndogo Sana kwenye Hizo post za Chadema.Huo ni ujumbe tosha kwa Chadema kuwa hakina umaarufu Sana ndani ya nchi walipo wapiga kura ikiwemo humu Jamii Forums
 
unaandika kama umekatwa kichwa!
Unajua kuna wakati gri ilipinduka , mtu mmoja kichwa kikakatika. mashuhuda waliona na usikia kichwa kikisema "nimesalimika, bila nyie wamnanchi hii gari ingelituua"! Ndivyo unavyoongea!
 
unaandika kama umekatwa kichwa!
Unajua kuna wakati gri ilipinduka , mtu mmoja kichwa kikakatika. mashuhuda waliona na usikia kichwa kikisema "nimesalimika, bila nyie wamnanchi hii gari ingelituua"! Ndivyo unavyoongea!
Wenye akili wanaelewa nilichoandika
 
Polisi inabidi ipongezwe, imefanya kazi nzuri ya kutukuka
 
Hichi ndicho Chadema walikuwa wanakutaka,pia soma Kuelekea 2025 - Kama Mara ya Kwanza Waliachwa Wakaandamana, Wakiachwa tena na Sasa na Wakapewa Ulinzi Kuna shida Gani?
 
Hapa ndipo tunapojidangsnya watawala. Matokeo yake tunatumia tena nguvu kubwa na rasilimali zetu kimakosa. Kwa mikoa niliyopita mimi nakuambia Hao jamaa ni maarufu kuliko unavyodhan, ndio maana viongozi wetu wanawapa hadhi kubwa. Tambua hilo.
Ndio maana mikutank ya Zccm na act hujaiona huko duniani lkn hii ndio hivyo. So tuendelee kutangaza 4 R huku tukijua kwamba Chadema ni chama kwelikweli
 
Mikoa ipi umepita wewe intake ambako Hilo la Chadema ningumxo kubwa mitaani?

Hamna kitu watu Saba Sana gumzo utasikia wanaongea NI mambo ya Simba na Yanga Tu hamna cha ya Chadema
 
Hivi wewe huwa hukamatwagi, au una mbio sana 😅
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…