Elections 2010 Umaarufu wa Kikwete Mkoa wa Mbeya utatetereka?

Elections 2010 Umaarufu wa Kikwete Mkoa wa Mbeya utatetereka?

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2008
Posts
4,768
Reaction score
2,361
JK asipuuzie suala la siasa za Mbeya kama zilivyojionyesha katika chaguzi za kura za Chama kuteua Wabunge.
Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa ambayo JK alipata kura nyingi sana hata kuzigi the National average.Mbeya ilikuwa na wastani wa 87-92%
Ukilinganisha na Dar es salaam, kiwango cha kura kutoka Jiji kuu hili lilikuwa CHINI ya kiwango..Dar es salaam ilikuwa na wastani wa 65-75%(National Average 80.28%)
Mivutano iliyojitokeza haimgusi moja kwa moja JK, lakini mteule wake Mkuu wa Mkoa ni mtu aliye karibu sana na mafisadi wasio utakia mema Mkoa wa Mbeya.
Pamekuwapo maoni kadhaa kutaka Mzee Mwakipesile ahamishiwe mikoa mingine ambayo hana mahusiano binafsi kisiasa, hilo halijafanyika.
Siyo siri kuwa RC hana mahusiano mazuri na karibu wabunge WOTE wa Mkoa wa Mbeya.Wabunge hawa wengi wao ambao wamepita kinyang'anyiro cha uteuzi wa kugombea ubunge wanakubalika sana na wananchi mkoani na ni wapinga ufisadi.
Wabunge wawili walioshindwa kinyang'anyiro cha uteuzi wa ubunge, Mama Kilasi wa Mbarali na G Sigonda wa Songwe/Chunya walikuwa na misimamo isiyoelewaka ukilinganisha na wabunge wenzao.Hawa wamebwagwa.
Vile vile Wabunge wa Mkoani Mbeya wameonyesha mshikamano mzuri sana na juhudi zao kisiasa zinakubalika kwa wananchi
Mada hii ni ya kukitahadharisha chama, mahsusi Mwenyekiti wa Chama, JK asipuuzie msimamo wa wananchi ili umaarufu wake usije ukatetereka Mkoani Mbeya, hasa tukielekea uchaguzi mkuu.
 
jk anaungwa mkon na watz wengi 95% ni ushindi mwaka huu
hujakosea hasa kwa sababu ccm, inawategemea sana ma 'shake well' kama wewe, kwani watu wasiyojitambua na wenye ufahamu wa kushikiwa ni mtaji mkubwa sana ccm, na watu kama wewe ni wengi sana
 
JK kama angekuwa anautakia mema Mkoa wa Mbeya angetatua mgogoro kati ya RC Mwakipesile na Wabunge karibu wote wa Mkoa huo! Maoni ya watu wengi wa majimbo yenye wabunge ambao Mwakipesile hawapendi hawamtaki JK kwa kuwa amewaletea mkuu wa Mkoa asiyewatakia mema! Jina la Dkt Slaa linazidi kung'ara Mbeya kwa sasa!
 
IMG_0355.JPG
 
hivi Jk bado ana umaarufu wowote kwa manufaa ya Nchi??au umaarufu wa kutabasamu na mambo ya kudensi kama picha hapo juu
 
Hata wasipopata kura wanaweza iba kwani ccm hawaeleweki. kwa hiyo hilo la kushuka umaarufu sijui kama linamsumbua. we shall see, we acha usiwakumbushe kwanza tuone kama huyu mnyama mkubwa hapa nchi anaweza angushwa.
 
Siasa za Tanzania zina kisirani na mkoa wa Mbeya.
Tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere hadi Kikwete.
Mkapa na Kikwete hawatasahau jinsi wananchi wa mkoa wa Mbeya walivyo waonyesha kwa kuvitendo kuwa hawatakiwi mkoani humo.
Mkapa aliumbuliwa na umati uliokuwa umefurika kwenye uwanja wa Sokoine,
alipopanda ili aanze kuhutubia umati wote ukatoka nje.
FFU wakaambiwa wafunge milango yote ili watu wasiondoke uwanjani hapo, lakini watu wakaparamia ukuta na kutokomea.
Kipigo cha mawe alichokipata Kikwete kamwe hato kusahau Mbeya.
Habari ndio hiyo
 
JK kama angekuwa anautakia mema Mkoa wa Mbeya angetatua mgogoro kati ya RC Mwakipesile na Wabunge karibu wote wa Mkoa huo! Maoni ya watu wengi wa majimbo yenye wabunge ambao Mwakipesile hawapendi hawamtaki JK kwa kuwa amewaletea mkuu wa Mkoa asiyewatakia mema! Jina la Dkt Slaa linazidi kung'ara Mbeya kwa sasa!
Umenena mkuu!
Mimi naona yanayoendelea sasa ni kumpa urais Dr Slaa on a silver platter.Kura ya Mbunge kwa CCM lakini urais kwa CHADEMA.
 
naona mwakipesile aliwekwa hapo kwa kazi maalumu ambayo ameshindwa kuifanya, naona waliompa hiyo kazi mwakipesile , walikuwa hawajawachunguza vizuri watu wa mbeya, walichukulia jambo kirahi rahisi kama kule nzega.
 
JK kama angekuwa anautakia mema Mkoa wa Mbeya angetatua mgogoro kati ya RC Mwakipesile na Wabunge karibu wote wa Mkoa huo! Maoni ya watu wengi wa majimbo yenye wabunge ambao Mwakipesile hawapendi hawamtaki JK kwa kuwa amewaletea mkuu wa Mkoa asiyewatakia mema! Jina la Dkt Slaa linazidi kung'ara Mbeya kwa sasa!

Ukweli ndio huo,visasi vya Jakaya dhidi ya Mwandosya na waliomuunga mkono kwenye kinyang'any'iro cha urais mwaka 2005 kiko pale pale
ingawa amekuwa anazuga kwa kumpa Mwandosya uwaziri!! It is too late kwa Jakaya kuredeem kura toka mkoa wa Mbeya kwani damage kimaendeleo aliyoifanya Mwakipesile kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ni kubwa mno kiasi kwamba haisameheki!! Inaelekea wanaMbeya have resigned to face anaother five years of stagnation if need be!! HAO NDIO WANAITWA" banyambala"
 
Ukweli ndio huo,visasi vya Jakaya dhidi ya Mwandosya na waliomuunga mkono kwenye kinyang'any'iro cha urais mwaka 2005 kiko pale pale
ingawa amekuwa anazuga kwa kumpa Mwandosya uwaziri!! It is too late kwa Jakaya kuredeem kura toka mkoa wa Mbeya kwani damage kimaendeleo aliyoifanya Mwakipesile kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ni kubwa mno kiasi kwamba haisameheki!! Inaelekea wanaMbeya have resigned to face anaother five years of stagnation if need be!! HAO NDIO WANAITWA" banyambala"

Sifa za Mwakipesile ni hizi:
1. Akipewa majungu na mtu wake wa karibu huyaamini moja kwa moja bila maswali. Mtu yeyote atakayemwambia vinginevyo hakubaliani naye hata kidogo!
2. Kinyongo huwa hakiishi milele kwa mzee huyu! Ukipishana naye kidogo tu ndio imetoka hiyo! Amejaa visasi mzee huyu!
3. Ni mtu wa kujiongezea maadui kila uchao! Kwa mfano kama wewe ni rafiki wa adui yake maana yake na wewe ni adui yake, yaani umepita bila kupingwa kuwa adui yake!
4. Ni mtu wa makundi, sio wa kuunganisha watu ili kutafuta maendeleo! Ukiamua kupeleka maendeleo Mkoani Mbeya kama ni adui wa Mwakipesile yeye anahesabu kuwa hayo si maendeleo!
5. Mtu wake wa karibu akikosea humkingia kifua kwa gharama yoyote! Watu wa Mwakipesile kwake yeye Mwakipesile ni wateule, huwa hawafanyi makosa! Kosa kwa Mwakipesile ni kuwa kinyume naye, basi!
6. n.k.......
Huyo ndiye Mwakipesile, kipenzi cha JK, ambaye ni adui (yaani JK na Mwakipesile) wa maendeleo na umoja wa watu wa Mkoa wa Mbeya!
 
Upinzani inabidi u concentrate sana sehemu ambazo zinajulikana ku support upinzani tayari.

1. Dar
2. Arusha
3. Kilimanjaro
4. Kagera
5. Mara
6. Kigoma
7. Mbeya ( Sugu ? )
8. Zanzibar
 
JK akishinda kura mby basi kaiba, hadi sasa ana changamoto tatu kuu hapo mby, one kuwadhalilisha wafanyakazi, pili ujio wa dr slaa kwenye kinyang'anyiro cha urais na tatu kumng'ang'ania mwakipesile mby. wananchi wanasema wanachoangalia uweo na sio chama kama ilivyokuwa huko nyuma
 
Siasa za Tanzania zina kisirani na mkoa wa Mbeya.
Tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere hadi Kikwete.
Mkapa na Kikwete hawatasahau jinsi wananchi wa mkoa wa Mbeya walivyo waonyesha kwa kuvitendo kuwa hawatakiwi mkoani humo.
Mkapa aliumbuliwa na umati uliokuwa umefurika kwenye uwanja wa Sokoine,
alipopanda ili aanze kuhutubia umati wote ukatoka nje.
FFU wakaambiwa wafunge milango yote ili watu wasiondoke uwanjani hapo, lakini watu wakaparamia ukuta na kutokomea.
Kipigo cha mawe alichokipata Kikwete kamwe hato kusahau Mbeya.
Habari ndio hiyo

Mkoa wa Mbeya ni mkoa ambao unaporomooka kimaendaleo kila siku, quality ya life Mbeya imeporomoka sana kuliko ilivyokuwa miaka ya 80 ya utawala wa mwalimu. Umuhimu wake kitaifa unazidi kuporomoka kutokana na siasa za ovyo. Mwakipesile amewekwa pale ili kuuvuruga mkoa wa mbeya na kuusambaratisha, and he is doing a great job. Wabunge wengi wa Mbeya wanajua hilo ndio maana hawaivi naye.
 
JK asipuuzie suala la siasa za Mbeya kama zilivyojionyesha katika chaguzi za kura za Chama kuteua Wabunge.
Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa ambayo JK alipata kura nyingi sana hata kuzigi the National average.Mbeya ilikuwa na wastani wa 87-92%
Ukilinganisha na Dar es salaam, kiwango cha kura kutoka Jiji kuu hili lilikuwa CHINI ya kiwango..Dar es salaam ilikuwa na wastani wa 65-75%(National Average 80.28%)
Mivutano iliyojitokeza haimgusi moja kwa moja JK, lakini mteule wake Mkuu wa Mkoa ni mtu aliye karibu sana na mafisadi wasio utakia mema Mkoa wa Mbeya.
Pamekuwapo maoni kadhaa kutaka Mzee Mwakipesile ahamishiwe mikoa mingine ambayo hana mahusiano binafsi kisiasa, hilo halijafanyika.
Siyo siri kuwa RC hana mahusiano mazuri na karibu wabunge WOTE wa Mkoa wa Mbeya.Wabunge hawa wengi wao ambao wamepita kinyang'anyiro cha uteuzi wa kugombea ubunge wanakubalika sana na wananchi mkoani na ni wapinga ufisadi.
Wabunge wawili walioshindwa kinyang'anyiro cha uteuzi wa ubunge, Mama Kilasi wa Mbarali na G Sigonda wa Songwe/Chunya walikuwa na misimamo isiyoelewaka ukilinganisha na wabunge wenzao.Hawa wamebwagwa.
Vile vile Wabunge wa Mkoani Mbeya wameonyesha mshikamano mzuri sana na juhudi zao kisiasa zinakubalika kwa wananchi
Mada hii ni ya kukitahadharisha chama, mahsusi Mwenyekiti wa Chama, JK asipuuzie msimamo wa wananchi ili umaarufu wake usije ukatetereka Mkoani Mbeya, hasa tukielekea uchaguzi mkuu.

Mkuu vipi aisee.........yaani unamsikitikia JK kupoteza umaarufu!!!..............yaani una matumaini kwamba JK atabadilika na kuleta maisha bora kwa kila mmoja wetu.............duh
 
Back
Top Bottom