Umachinga mikoani unalipa pia

yassird200

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2025
Posts
466
Reaction score
813
Habari za zenu wana JF.

Leo nimeona ni share experience yangu hapo nyuma. Binafsi nimeajiriwa but private sector, baada ya kuhitimu elimu ya juu nilihangaika sana kwani nilihisi elimu yangu ingenisaidia.

Lakini nikuja kugundua this TZ. Yeah, nilianza hustle za umachinga 2020/2023. Mwanzo nilipitia ugumu fulani kukubali hali ile lakini at least sikuwa nategemea wazazi.

Nashauri vijana wanaohangaika huko Dar es Salaam huku ni wa mikoani, hata waliozaliwa huko. Njoeni mikoani mjitafute.

Kijana, hizo simu zenu kama huna uhakika wa kula, uza – ni mtaji tosha. Acheni kuhangaisha wazazi huku uwezo mnao (laki mbili inatosha kuanzia maisha).

Punguzeni kulalamikia serikali, fanyeni kazi. Hata hao mashangazi watawachoka, sio mama zenu hao.

NB: Thamani ya mtu hutengenezwa na yeye pekee. Vijana, vueni aibu, pambaneni, tutengeneze kesho yetu wenyewe.
 
Mwandiko wa mhitimu huu Tena ukute ni wa kitivo Cha Sheria pale chuo kikuu huria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…