figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
Salaam Wakuu,
Natamani kuona kila mtu akihesabiwa kwa maendeleo sawa ya nchi yetu.
Ila bado nailaumu Serikali na NBS kwa kulifanya lionekane swala la Kisiasa.
Wameshindwa kutumia Teknolojia kufanikisha hili swala kwa 50% siku ya kwanza badala yake siku ya kwanza wanaenda kufanyiwa Sensa watu 9%.
Kwanza hawajatoa Elimu ya kutosha kwa Wananchi. Watanzania wanaamini kuwahesabu ni kuwachulia kifo, hatoi namba sahihi.
Pili sehemu za Mijini wangetumia Application za simu ambazo mtu naweza kujaza ile fomu yake hata kama yupo ndani ya basi anasafiri.
Pia miezi miwili kabla walitakiwa wawe wameshasambaza maswali wanayouliza ili watu wajiandae, eti leo mtu anaulizwa namba ya NIDA, kweli?
Wanasiasa wa CCM wiki mbili za mwisho kutumia Mgongo wa Sensa kujitangaza ndo imefanya ionekana ni swala la CCM. kumvuka wanachama wa CCM hawazidi Mil 10 kati ya Watanzania Mil 60.
Serikali ilishindwa kutumia Mitandao Mikubwa kama JamiiForums kutoa elimu ya Sensa, wanaishia hela kuisambaza kwa Wanavikundi wa CCM Wafanye Mabonanza na maonesho. Hakuna hata mmoja alofanya onesho wala Bonanza Vijijini.
Hii kazi ingefanywa na Walimu kuliko kuwapa watu wasiojua hata kutumia tablets. Watu wa Sensa wamepewa nafasi kulipana fadhira
Je, kwanini Serikali haijatumia Teknolojia kufanya Sensa?
Kwanini Wametumia wana CCM wawe Makalani wa Sensa? Wananchi hawaongei ila wanajua.
Pamoja na mapungufu yetu, bado Sensa ni Muhimu kwa Nchi ili kutoa huduma sawa.
Chonde chonde, kubali kuhesabiwa
Sensa si ya Samia wala Mbowe bali ya Watanzania
Natamani kuona kila mtu akihesabiwa kwa maendeleo sawa ya nchi yetu.
Ila bado nailaumu Serikali na NBS kwa kulifanya lionekane swala la Kisiasa.
Wameshindwa kutumia Teknolojia kufanikisha hili swala kwa 50% siku ya kwanza badala yake siku ya kwanza wanaenda kufanyiwa Sensa watu 9%.
Kwanza hawajatoa Elimu ya kutosha kwa Wananchi. Watanzania wanaamini kuwahesabu ni kuwachulia kifo, hatoi namba sahihi.
Pili sehemu za Mijini wangetumia Application za simu ambazo mtu naweza kujaza ile fomu yake hata kama yupo ndani ya basi anasafiri.
Pia miezi miwili kabla walitakiwa wawe wameshasambaza maswali wanayouliza ili watu wajiandae, eti leo mtu anaulizwa namba ya NIDA, kweli?
Wanasiasa wa CCM wiki mbili za mwisho kutumia Mgongo wa Sensa kujitangaza ndo imefanya ionekana ni swala la CCM. kumvuka wanachama wa CCM hawazidi Mil 10 kati ya Watanzania Mil 60.
Serikali ilishindwa kutumia Mitandao Mikubwa kama JamiiForums kutoa elimu ya Sensa, wanaishia hela kuisambaza kwa Wanavikundi wa CCM Wafanye Mabonanza na maonesho. Hakuna hata mmoja alofanya onesho wala Bonanza Vijijini.
Hii kazi ingefanywa na Walimu kuliko kuwapa watu wasiojua hata kutumia tablets. Watu wa Sensa wamepewa nafasi kulipana fadhira
Je, kwanini Serikali haijatumia Teknolojia kufanya Sensa?
Kwanini Wametumia wana CCM wawe Makalani wa Sensa? Wananchi hawaongei ila wanajua.
Pamoja na mapungufu yetu, bado Sensa ni Muhimu kwa Nchi ili kutoa huduma sawa.
Chonde chonde, kubali kuhesabiwa
Sensa si ya Samia wala Mbowe bali ya Watanzania