Umasikini, ukosefu wa lishe bora huleta maradhi mengi miongoni mwetu

Umasikini, ukosefu wa lishe bora huleta maradhi mengi miongoni mwetu

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Magonjwa yamekuwa mengi sana siku hizi, hospital nyingi zimezidiwa na wagonjwa.

Pamoja na mambo mengine ukosefu wa lishe bora nao pia ndio chanzo cha baadhi ya magonjwa mengi.

Kutokana na umaskini uliokithiri miongoni mwetu watu hula chochote kilicho mbele yao kutokana na wengi kutoweza kumudu gharama za mlo kamili. Wengi hawana vipato vinavyoeleweka na wengine hukosa kipato kwa siku. Wiki, nk.

Asilimia kubwa ya watu wa vipato vya chini ugali na mboga za majani ndio mlo wao wa kila siku. Mchana na usiku.,amejitahidi sana kubadilisha atakula wali maharage.

Vyakula kama samaki, maziwa, maini, magimbi. Viazi vitamu, kuku. Na matunda matunda kwao ni anasa

Pombe kali za bei rahisi ambazo ndio chanzo cha magonjwa ya figo au ini. Ndio hujipooza nayo baada ya mahangaiko ya hapa na pale.
 
Back
Top Bottom