Fahami Matsawili
Senior Member
- Mar 8, 2018
- 172
- 153
Umefika muda sekta ya Vicoba itungiwe sheria ya kuwasimamia na kupewa chombo maalum cha kuwa mwangalizi wao kuliko ilivyo sasa haijulikani wapo wizara gani kati ya wizara ya fedha na mipango au wizara ya viwanda Biashara na Uwekezaji...
Kwa sasa Wananchi milioni 5 wamejiunga kwenye Vicoba kwa nia ya kujipatia kipato hadi Leo vikundi vya Vicoba nchi Nzima vina Mtaji Trillion 1.4
Fedha hizi ni nyingi sana hasa kwenye uelekeo wa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wetu John Magufuli ya Ujenzi wa Sekta ya Viwanda kuelekea uchumi wa kati 2025...
Badala ya Vicoba kuwa kwenye mfumo wa kuweka akiba na kukopa tuu sasa ni wakati wa Vicoba kutumia fedha hizi katika kuwekeza kwenye Viwanda na Miradi mikubwa ambayo mtazalisha ajira zaidi na mtapata faida zaidi ya miradi yenu mtakayooanzisha....
Tumeona hayo kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii imetoka kwenye mfumo wa kuweka akiba tu hadi pension na sasa mifuko imeanza uwekezaji wa miradi mikubwa ya kiuchumi...
Sasa muda wa kuwa na sheria na chombo Maalum cha kuwalea na kuwasaidia nadhani Umefika lakini zaidi nimefurahi zaidi kuona vijana wa bodaboda na bajaji wameanza kuitikia mfumo huu wa Vicoba kwa kujiunga pamoja na kuchangishana na kuweka akiba nimepita kwenye banda lao wamenambia wengine wamenunua bajaji zao kutoka bajaji za mikopo kupitia mfumo huu wa Vicoba......
Tuna Vijana wengi wapo kwenye sekta ya bodaboda na bajaji karibu vijana milioni 2 wamejiajili huko na wengine wanaendesha maisha maisha yao, wamejenga na wengine wanalipa kodi kupitia bajaji na bodaboda.....
Kazi ya Mamlaka husika ni kuwasaidia hawa vijana wenzangu kuondoa changamoto zinazowakabili kama Elimu ya usalama barabarani ya Mara kwa Mara wawe na Vazi rasmi lenye no na kituo Maalum kama wenzenu wa nchi ya Rwanda.
Polisi wawe rafiki na bodaboda na bajaji katika kuwasaidia badala ya kuwachukulia kama wahalifu na wahuni.
Vijana wa Bodaboda na bajaji milioni 2 tulionao sasa kama kila mmoja anakusanya wastani wa Elfu 10 kila Mmoja kwa siku ina maana sekta ya bodaboda na bajaji kwa siku nchi Nzima wanaingiza Shillingi billioni 20 kwa siku..
Ina maana hawa wakisaidiwa kupewa Elimu ya kujiunga na kujiwekea akiba kiasi kidogo tu kutoka kwenye hiyo Elfu 10 wanayopata kila siku kama hawa wenzao ambao tayari wameanza tutakuwa na vijana wenye vipato vizuri na watawekeza kwenye miradi mikubwa ya Uzalishaji wa kiuchumi..
Kwa sasa Wananchi milioni 5 wamejiunga kwenye Vicoba kwa nia ya kujipatia kipato hadi Leo vikundi vya Vicoba nchi Nzima vina Mtaji Trillion 1.4
Fedha hizi ni nyingi sana hasa kwenye uelekeo wa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wetu John Magufuli ya Ujenzi wa Sekta ya Viwanda kuelekea uchumi wa kati 2025...
Badala ya Vicoba kuwa kwenye mfumo wa kuweka akiba na kukopa tuu sasa ni wakati wa Vicoba kutumia fedha hizi katika kuwekeza kwenye Viwanda na Miradi mikubwa ambayo mtazalisha ajira zaidi na mtapata faida zaidi ya miradi yenu mtakayooanzisha....
Tumeona hayo kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii imetoka kwenye mfumo wa kuweka akiba tu hadi pension na sasa mifuko imeanza uwekezaji wa miradi mikubwa ya kiuchumi...
Sasa muda wa kuwa na sheria na chombo Maalum cha kuwalea na kuwasaidia nadhani Umefika lakini zaidi nimefurahi zaidi kuona vijana wa bodaboda na bajaji wameanza kuitikia mfumo huu wa Vicoba kwa kujiunga pamoja na kuchangishana na kuweka akiba nimepita kwenye banda lao wamenambia wengine wamenunua bajaji zao kutoka bajaji za mikopo kupitia mfumo huu wa Vicoba......
Tuna Vijana wengi wapo kwenye sekta ya bodaboda na bajaji karibu vijana milioni 2 wamejiajili huko na wengine wanaendesha maisha maisha yao, wamejenga na wengine wanalipa kodi kupitia bajaji na bodaboda.....
Kazi ya Mamlaka husika ni kuwasaidia hawa vijana wenzangu kuondoa changamoto zinazowakabili kama Elimu ya usalama barabarani ya Mara kwa Mara wawe na Vazi rasmi lenye no na kituo Maalum kama wenzenu wa nchi ya Rwanda.
Polisi wawe rafiki na bodaboda na bajaji katika kuwasaidia badala ya kuwachukulia kama wahalifu na wahuni.
Vijana wa Bodaboda na bajaji milioni 2 tulionao sasa kama kila mmoja anakusanya wastani wa Elfu 10 kila Mmoja kwa siku ina maana sekta ya bodaboda na bajaji kwa siku nchi Nzima wanaingiza Shillingi billioni 20 kwa siku..
Ina maana hawa wakisaidiwa kupewa Elimu ya kujiunga na kujiwekea akiba kiasi kidogo tu kutoka kwenye hiyo Elfu 10 wanayopata kila siku kama hawa wenzao ambao tayari wameanza tutakuwa na vijana wenye vipato vizuri na watawekeza kwenye miradi mikubwa ya Uzalishaji wa kiuchumi..