Umeme: kipindi mwaka 2000 - 2012 hakuna bwawa jipya la umeme lilojengwa?

Umeme: kipindi mwaka 2000 - 2012 hakuna bwawa jipya la umeme lilojengwa?

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
Wanabodi ya JamiiForums,
Tanzania ina upungufu mkubwa wa umeme, lakini tukiangalia miaka ya awamu ya kwanza chini ya Mwl. J.K Nyerere, Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa kulikuwa na juhudi za makusudi kuongeza vyanzo vya umeme utokanao na maji ili kukidhi mahitaji ya umeme nchini.

Kila mmoja anajua kuwa kuna chanzo cha Stielger Gorge (Tanzania: Stiegler's Gorge Power Project MOU Signed allAfrica.com: Tanzania: Stiegler's Gorge Power Project MOU Signed ) chenye uwezo-tajwa 2100MW lakini hakuna juhudi au kelele nyingi za serikali ya awamu hii ya 2005-2015 kufanikisha ujenzi na kisha uzalishaji wa umeme kuondoa kabisa tatizo la umeme.

Umeme wa Stielger Gorge 2100 MW pamoja na vyanzo vya umeme utokanao na gesi pamoja na makaa ya mawe ungeweza kuiweka Tanzania katika chati ya nchi zisizo na tatizo la nishati na kuwezesha kuleta mapinduzi ya viwanda, usafiri wa treni, mabasi ya umeme(trams) na kuifanya nchi ya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa.

Basi tutizame vyanzo vya sasa vya umeme utokanao na vyanzo vya maji na miaka miradi hiyo ilipokamilika:

Historia ya ujenzi wa mabwawa ya umeme:
  • 1964- Hale uwezo megawati 21MW
  • 1965 - Nyumba ya Mungu megawati 8MW
  • 1979- Mtera megawati 80MW
  • 1980s- Kidatu (Phase I & II) megawati 204MW
  • 2000 - Lower Kihansi megawati 180MW

Wanabodi, tatizo ni nini hasa hata kuifanya serikali isiwe na mshawasha wa kumaliza tatizo la nishati na kuleta mapinduzi ya kimaendeleo hapa Tanzania?

Jakaya-Kikwete-akitangaza-Baraza-la-Mawaziri.jpg


Sources;
Welcome to TANESCO
The United Republic of Tanzania – Ministry of Energy and Minerals
 
Wanabodi ya JamiiForums,
Tanzania ina upungufu mkubwa wa umeme, lakini tukiangalia miaka ya awamu ya kwanza chini ya Mwl. J.K Nyerere, Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa kulikuwa na juhudi za makusudi kuongeza vyanzo vya umeme utokanao na maji ili kukidhi mahitaji ya umeme nchini.

Kila mmoja anajua kuwa kuna chanzo cha Stielger Gorge (Tanzania: Stiegler's Gorge Power Project MOU Signed allAfrica.com: Tanzania: Stiegler's Gorge Power Project MOU Signed ) chenye uwezo-tajwa 2100MW lakini hakuna juhudi au kelele nyingi za serikali ya awamu hii ya 2005-2015 kufanikisha ujenzi na kisha uzalishaji wa umeme kuondoa kabisa tatizo la umeme.

Umeme wa Stielger Gorge 2100 MW pamoja na vyanzo vya umeme utokanao na gesi pamoja na makaa ya mawe ungeweza kuiweka Tanzania katika chati ya nchi zisizo na tatizo la nishati na kuwezesha kuleta mapinduzi ya viwanda, usafiri wa treni, mabasi ya umeme(trams) na kuifanya nchi ya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa.

Basi tutizame vyanzo vya sasa vya umeme utokanao na vyanzo vya maji na miaka miradi hiyo ilipokamilika:

Historia ya ujenzi wa mabwawa ya umeme:
  • 1964- Hale uwezo megawati 21MW
  • 1965 - Nyumba ya Mungu megawati 8MW
  • 1979- Mtera megawati 80MW
  • 1980s- Kidatu (Phase I & II) megawati 204MW
  • 2000 - Lower Kihansi megawati 180MW

Wanabodi, tatizo ni nini hasa hata kuifanya serikali isiwe na mshawasha wa kumaliza tatizo la nishati na kuleta mapinduzi ya kimaendeleo hapa Tanzania?

Jakaya-Kikwete-akitangaza-Baraza-la-Mawaziri.jpg


Sources;
Welcome to TANESCO
The United Republic of Tanzania – Ministry of Energy and Minerals
bwawa la maji?
 
Mchakato waa Stielger Gorge ushaanza sasa na tuna umeme wa gesi. Many more to come.
 
Back
Top Bottom