Umemuandalia nini mtoto asubuhi? Chakula chetu cha leo ni rojo la Karoti na Nanasi

Umemuandalia nini mtoto asubuhi? Chakula chetu cha leo ni rojo la Karoti na Nanasi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Ni chakula kizuri sana kutumia kama kifungua kinywa (breakfast) cha mtoto kwa sababu kina kiasi kikubwa sana cha virutubisho.

Chakula hiki kitamfanya mtoto wako awe na siku nzuri yenye uchangamfu. Chakula hiki pia ni kizuri sana kama una shughuli nyingi, kwani utakiandaa kwa muda mchache tu.

Chakula: Rojo la karoti na nanasi
Uuda wa kuandaa: Takribani dakika 20
Umri: Kuanzia miezi nane

Katika kuandaa chakula hiki utahitaji

½ kikombe cha vipande vya nanasi,
Karoti moja ambayo umeikata vizuri na
Mdalasini.

Namna ya kuandaa

> Anza kwa kuchanganya vipande vya karoti na nanasi katika chombo kimoja kisha upike mchanganyiko wako kwa muda wa dakika 7 – 10 au mpaka utakaporidhikia na ulaini.

> Baada ya kupoa hamishia kila kitu kwenye blenda na usage mpaka utakapopata wepesi sahihi kwa mtoto wako. Kama mtoto wako amefikia miezi 10 unaweza kuponda badala ya kutumia blenda.

> Unaweza kutumia maji au maziwa katika kudhibiti wepesi wakati wa kusaga au kuponda.

> Malizia kwa kuongeza kiungo ambacho mtoto wako anakipenda, mimi nimetumia mdalasini.

> Wewe unaweza kutumia kiungo ambacho kinampendeza mtoto.

Unaweza kutunza chakula hiki kwenye friji na kumpa mtoto kidogo kidogo.
 
Bosslady nina shida na wewe [emoji4][emoji4][emoji4]
 
Ni chakula kizuri sana kutumia kama kifungua kinywa (breakfast) cha mtoto kwa sababu kina kiasi kikubwa sana cha virutubisho.

Chakula hiki kitamfanya mtoto wako awe na siku nzuri yenye uchangamfu. Chakula hiki pia ni kizuri sana kama una shughuli nyingi, kwani utakiandaa kwa muda mchache tu.

Chakula: Rojo la karoti na nanasi
Uuda wa kuandaa: Takribani dakika 20
Umri: Kuanzia miezi nane

Katika kuandaa chakula hiki utahitaji

½ kikombe cha vipande vya nanasi,
Karoti moja ambayo umeikata vizuri na
Mdalasini.

Namna ya kuandaa

Anza kwa kuchanganya vipande vya karoti na nanasi katika chombo kimoja kisha upike mchanganyiko wako kwa muda wa dakika 7 – 10 au mpaka utakaporidhikia na ulaini.

Baada ya kupoa hamishia kila kitu kwenye blenda na usage mpaka utakapopata wepesi sahihi kwa mtoto wako. Kama mtoto wako amefikia miezi 10 unaweza kuponda badala ya kutumia blenda.

Unaweza kutumia maji au maziwa katika kudhibiti wepesi wakati wa kusaga au kuponda.

Malizia kwa kuongeza kiungo ambacho mtoto wako anakipenda, mimi nimetumia mdalasini.

Wewe unaweza kutumia kiungo ambacho kinampendeza mtoto.

Unaweza kutunza chakula hiki kwenye friji na kumpa mtoto kidogo kidogo.
Hi boss lady nmepitia nyuzi nmeona uko vzuri kutoa ushauri wa chakula cha mtoto..

Wangu ni miaka 2 na nusu ila naona amechoka viaz, samak na wali...naomba unisaidie meal mfano lunch na jion
 
Hi boss lady nmepitia nyuzi nmeona uko vzuri kutoa ushauri wa chakula cha mtoto..

Wangu ni miaka 2 na nusu ila naona amechoka viaz, samak na wali...naomba unisaidie meal mfano lunch na jion
Mtori, ndizi, Rojo la magimbi pia ni poa kwa mtoto
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Back
Top Bottom