Umeshawahi kukutana na mtu ameuchapa usingizi kwenye daladala?

Umeshawahi kukutana na mtu ameuchapa usingizi kwenye daladala?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Binafsi niliwahi kusinzia kwenye usafiri wa daladala hadi kupitilza kituo nilichokusudia kushuka. So, sikuona kama ni jambo la kushangaza sana.

Lakini leo hii Anti yangu ananisimulia kwa kushangaa alichokishuhudia kwenye daladala huko Dar es salaam, ati ameketi kwenye siti na pembeni yake kuna abiria mwingine aliesinzia na anakoroma na kuvibrate kama kiswaswadu, huku akistukastuka na kumuegemea mabegani mwake huku akiwa ameachama mdomo wazi kukoroma na udenda ukichuruzika...

Vipi wewe umeshakumbana na hali kama hii, kwenye dalalala mjini achilia mbali mabasi au safari ndefu za mikoani ambazo mara nyingi kuuchapa usingizi ni kawaida?
 
Ha ha ha mkuu watu wanachoka sana mjini hapa wee fikiria mtu anakaa chanika anafanya mishe kkoo ili awahi anatoka saa 11 alfajiri na kurudi kwake wengine mpk saa usiku afike huko chanika saa 7 alale 11 aamke tena kwanini asikorome kwenye daladala?
 
Enzi ninaskuli, nishasinzia sana kwenye daladala....
 
Kuna siku niko kwenye daladala natoka segerea naenda makumbusho, nimekaa na mkaka yaan kalala hana hata habari,

Alikua kainama hivi, aseeh kuja kustuka hiviii, udenda unamtokaa.
Nlishangaa, yule mkaka hafananii na kutoa udenda akiwa amelala, woiiiiih
 
Nilikua natoka K/koo naelekea Maeneo Fulani nikaamua kulalaa Ile nashtuka nakuta nimepitiliza Vituo Viwili Toka pale nilipotaka kushuka
 
Back
Top Bottom