Umeshawahi kupokea matangazo ya kubeti na hujawahi kuomba huduma zao? Unajua pa kushtaki ulipwe kwa wizi huo wa taarifa zako?

Umeshawahi kupokea matangazo ya kubeti na hujawahi kuomba huduma zao? Unajua pa kushtaki ulipwe kwa wizi huo wa taarifa zako?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu, salama huko mlipoamkia?

Naamini wengi wetu tumekuwa tukipokea matangazo kwenye simu zetu ya huduma ambazo hatujawi kuzitaka, na hujawahi kutoa namba yako na kuwaruhusu kukutumia matangazo hayo.

Tena wakati mwingine wanataja mpaka jina lako, mf. Habari Cute Wife, unajua unaweza kujishindia milioni 10 ukitabiri mechi moja tu kwa usahihi? Sasa unabaki kushangaa eeeeh, yaani wana mpaka jina langu?

Unakuta upo ka mimi hujui hata kubeti lakini simu yako imejaa matangazo ya kubeti!

Kama hujatoa mawasiliano na kukubali kutumiwa matangazo haya ina maana namba yako imechukuliwa kimagendo kutoka sehemu fulani ambako uliwahi kuacha namba hii, mfano ulienda kwenye ofisi fulani ukatakiwa uandike jina na namba ya simu ili uweze kuingia, na wakati mwingine inaweza kuwa ni kutoka mtandao wako wa simu unaotumia, yale yaliyomfika Lissu ikawa ni extreme case sababu ya taarifa zako kuuzwa na kutumiwa vibaya.

Sasa umepatwa na kadhia hizi unajua wapi unatakiwa kwenda kushtaki na kulipwa maokoto yako kwa wizi huo wa taarifa zako binafsi?

====

Je, unatakiwa kuripoti wapi? Angalia maelekezo hapa👇👇

Endapo umepokea jumbe za namna hiyo bila ridhaa yako au bila kumpatia mtuma ujumbe namba zako unatakiwa kuwasilisha malalamiko hayo kwa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ambayo imeanzishwa kwa lengo la kusimamia na kulinda Taarifa Binafsi na faragha za watu nchini.

Malalamiko hayao yanaweza kuwasilishwa njia ya kwa maandishi au unaweza kuwasiliana nao kwa njia ya simu ukapewa mwongozo zaidi.

Tume hiyo imeanzishwa chini ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti yao. Na kizuri ni kuwa hakuna presha ya kuwaza kuhusu pesa za wakili kusimamia madai yako, wadau wapo kusimamia sehemu hii kuhakikisha unapata haki yako na kila aliyehusika kwenye kuingilia faragha yako anawajibika ipasavyo

pye Chang shen Nyoka kibisa Kudasai TheChoji
 
Wakaa, salama huko mlipoamkia?

Naamini wengi wetu tumekuwa tukipokea matangazo kwenye simu zetu ya huduma ambazo hatujawi kuzitaka, na hujawahi kutoa namba yako na kuwaruhusu kukutumia matangazo hayo.

Tena wakati mwingine wanataja mpaka jina lako, mf. Habari Cute Wife, unajua unaweza kujishindia milioni 10 ukitabiri mechi moja tu kwa usahihi? Sasa unabaki kushangaa eeeeh, yaani wana mpaka jina langu?

Unakuta upo ka mimi hujui hata kubeti lakini simu yako imejaa matangazo ya kubeti!

Kama hujatoa mawasiliano na kukubali kutumiwa matangazo haya ina maana namba yako imechukuliwa kimagenda kutoka sehemu fulani ambako uliwahi kuacha namba hii, mfano ulienda kwenye ofisi fulani ukatakiwa uandike jina na namba ya simu ili uweze kuingia, na wakati mwingine inaweza kuwa ni kutoka mtandao wako wa simu unaotumia, yale yaliyomfika Lissu ikawa ni extreme case sababu ya taarifa zako kuuzwa na kutumiwa vibaya.

Sasa umepatwa na kadhia hizi unajua wapi unatakiwa kwenda kushtaki na kulipwa maokoto yako kwa wizi huo wa taarifa zako binafsi?
Cute Wife,
Hebu endelea kumwaga maujanja wapi pa kuanzia.
 
Watu jinsi walivyo na njaa + jumlisha idadi ya watu ambao tushawahi pokea msg hizi za kipuuzi, hizo kampuni zitafilisika mchana kweupee
😂
 
Bongo hii hii ukashitaki wapi sasa sanasana utapoteza mda wako tuu
 
Mpaji Mungu na Pondamali Kufakwaja mnacheka nini?😃😃 Mtushirikishe na sisi tufurahi
Mara nyingi hayo makampuni ya kubeti/kubashiri hawachukui namba zako popote wanachofanya wao wanaenda kwa mtandao husika labda Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel & TTCL wanalipa kiasi flan Cha hela kutegemeana na idadi ya wateja wa mtandao husika....then mtandao ndo unawatumiaa sms wateja wake wote
 
Mara nyingi hayo makampuni ya kubeti/kubashiri hawachukui namba zako popote wanachofanya wao wanaenda kwa mtandao husika labda Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel & TTCL wanalipa kiasi flan Cha hela kutegemeana na idadi ya wateja wa mtandao husika....then mtandao ndo unawatumiaa sms wateja wake wote
Sasa ndio wameuza taarifa zako, kinyume na sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi, wanafaidika kupitia utu wako....unatakiwa kufidiwa kwa ukiukwaji huu
 
Sasa ndio wameuza taarifa zako, kinyume na sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi, wanafaidika kupitia utu wako....unatakiwa kufidiwa kwa ukiukwaji huu
Inatakiwa kua hivo ila sasa rushwa mwanangu rushwa rushwa rushwa
 
Endapo umepokea jumbe za namna hiyo bila ridhaa yako au bila kumpatia mtuma ujumbe namba zako unatakiwa kuwasilisha malalamiko hayo kwa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ambayo imeanzishwa kwa lengo la kusimamia na kulinda Taarifa Binafsi na faragha za watu nchini.

Malalamiko hayao yanaweza kuwasilishwa njia ya kwa maandishi au unaweza kuwasiliana nao kwa njia ya simu ukapewa mwongozo zaidi.

Tume hiyo imeanzishwa chini ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti yao. Na kizuri ni kuwa hakuna presha ya kuwaza kuhusu pesa za wakili kusimamia madai yako, wadau wapo kusimamia sehemu hii kuhakikisha unapata haki yako na kila aliyehusika kwenye kuingilia faragha yako anawajibika ipasavyo

pye Chang shen Nyoka kibisa Kudasai TheChoji
 
Bongo hii hii ukashitaki wapi sasa sanasana utapoteza mda wako tuu
Acha kukariri, kama umepitia changamoto hii na una vithibitisho peleka malalamiko yako kwa tume hiyo na utaleta mrejesho hapa kama suala lako limefanyiwa kazi au lah!
 
Endapo umepokea jumbe za namna hiyo bila ridhaa yako au bila kumpatia mtuma ujumbe namba zako unatakiwa kuwasilisha malalamiko hayo kwa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ambayo imeanzishwa kwa lengo la kusimamia na kulinda Taarifa Binafsi na faragha za watu nchini.

Malalamiko hayao yanaweza kuwasilishwa njia ya kwa maandishi au unaweza kuwasiliana nao kwa njia ya simu ukapewa mwongozo zaidi.

Tume hiyo imeanzishwa chini ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022. Kwa msaada zaidi tembelea tovuti yao. Na kizuri ni kuwa hakuna presha ya kuwaza kuhusu pesa za wakili kusimamia madai yako, wadau wapo kusimamia sehemu hii kuhakikisha unapata haki yako na kila aliyehusika kwenye kuingilia faragha yako anawajibika ipasavyo

pye Chang shen Nyoka kibisa Kudasai TheChoji
Nimechungulia huko, pako vizuri ila lugha tu, inabidi ujue kiinglish ili ujaze form sasa huo nao ni mkwamo flani

Sio kila mtu ni tulia
 
Back
Top Bottom