Umewahi kubadili namba yako ya simu na kuanza kusajili ndugu na marafiki upya?

Umewahi kubadili namba yako ya simu na kuanza kusajili ndugu na marafiki upya?

66KV

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2014
Posts
1,322
Reaction score
2,610
Dunia uwanja wa fujo, Dunia tambara bovu, Waswahili walisema.

Kuna muda nafsi inachoka kabisa na harakati au mtindo wa maisha ulionao, unatamani kupiga chini kila kitu na kuanza upya kabisa ukiwa focused. Eneo linalochosha zaidi ni namba ya simu ya muda mrefu inayogeuka kuwa mzigo usiobebeka.

Makundi ya WhatsApp yasiyo na kichwa wala miguu, kuwa na namba za watu ambao hamuwasiliani hata miaka 10, na wakikutafuta ujue unapigwa kirungu.

Umewahi kufikiria kubadili namba ya simu kwa lengo la kujipa muda wa tafakari, kujiboresha wewe na kuboresha mahusiano yako ama kupunguza cycle ya watu ukiwa na matumaini ya kuanza upya kabisa?

Kama upo, naomba uzoefu wako. Hasara zipi ulipata na faida zipi ulipata? Naamini penye wengi hapakosi neno la busara.

Mkawe na wakati mzuri.
 
Kwa mm sikubadili namba ila nilifuta namba zote. nikaanza ku save namba upya za ndugu zangu nao n baadhi, pia kuna baadhi ya Wana wakarib nami tunao shinda nao kweny harakat pia nika save namba zao.

na pia nilibadilish namba ya whatsap niliyozoelek san na watu na kuwek nyingin ambay sipatikan mara kwa mara kwa lain hiyo.
Kwa kufanya ivo kdg najion nimepunguz ule kujuan san na pia kule kujuana san. Pia kuna wana wengin ambao walikuw wakinitafut kipind nikizipat saiz hamna.

Jambo kuu la msingi kabisa mpka kufikia kubadili na whatssap namb ni Wanawake() nilipunguza kujuan sana mpk wanakuzoea. ni hivyo tu mkuu​

 
Icho kipindi nimewai kukipitia nikafanya hivo na kimejiludia tena sahivi nnavo sema apa toka tar 21 nime badili namba ya simu pia whtsp sitaki interaction isiyo na umuhimu ya kuna watu ni mna angaliana status tu hakuna kipya kinaendelea wala kutafutana kawaida japo kusalimiana yani kiufupi kuna vitu vingi sana siwezi kuandika kwa pamoja ila nnacho kuaga na hofia ni kupishana na fursa tu yani naogopaga kusije kukawa na mchongo wa maana alafu nikashindwa kupatikana uenda yote ni mtu uyo nilikua nimeshaona simu hitaji tena na hakua na namba yangu mpya kwaiyo akashindwa kunipata JITAHIDI kuangalia baazi ya watu usipotezane nao na kumuomba pia mungu akutangulie usisababishe kukutana na kitu ambacho hakikua sahihi kutokana na maamuzi hayo lakini SIZANI KAMA NI KOSA KUFANYA HIVO NA UNA MKOSEA MWENYEZI MUNGU AU KUVUNJA SHERIA YOYOTE YA NCHI
 
Back
Top Bottom