Umewahi kusumbuliwa na wakala wa Bima za Mitandao ya simu?, Wape majibu haya watakata simu haraka

Umewahi kusumbuliwa na wakala wa Bima za Mitandao ya simu?, Wape majibu haya watakata simu haraka

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Ni watu wanaosumbua sana,

Reality sio matapeli ila jinsi wanavyoshawishi unaona kabisa ni biashara inayoshahabiana na biashara za kitapeli.

Akianza tu mwambie naomba nikuulize swali , akikupa ruhusa muulize hivi; BIMA maana yake ni kuwekeza unufaike wakati ambao huenda utakuwa hauko vizuri kiuchumi, sasa nyie mnataka niwekeze sasa nikiwa mzima halafu nikipata ugonjwa nitoe tena pesa kujitibu nikitarajia malipo pindi nikitoka hospitalini baada ya kulazwa kwa kipindi ambacho mmekitaja ndipo ninufaike au mwenzi wangu apate pesa nikifa, je, huoni kuwa hiyo biashara ni ya vichaa?

Kwanini msitoe bima ambayo mtu atatibiwa kwayo badala ya mtu kutumia pesa zake tena zake kujitibu anapoumwa ilhali alikatwa?

Watakata simu haraka na wewe utaendelea na shughuli zako
 
Ndiyo kusumbuka kiasi chote hicho kwa kutoa hayo maelezo marefu badala ya kuwaambia tu kuwa hauhitaji huduma hiyo? Muda ni mali adimu.
 
Back
Top Bottom