Aman iwe nanyi wakuu
Huu uzi unatuhusu wale wajanja ambao tulipigwa kiboya sana na wajanja wa mjini tukaachwa kwenye mataa
Aisee iko hivi namna ambavyo nilipigwa kiboya sana
Ilikuwa munamo mwaka 2010 niko darasa la tano mimi beira boy nikiwa nimeagizwa sukari dukan nikaondoka na basikel yangu ya gia ambayo nilikuwa nimeletewa na sister kutoka huko mjini
Nakumbuka ilikuwa mida ya jion ndo nilipopigwa kiboya sana aisee
Nilikutana na jamaa mmoja mshamba mshamba sana jamaa amekaa kama msukuma sijui wa wapi tu yaan
Jamaa akanambia wewe dogo simama, dah bila hiyana si nikasimama aisee jamaa akaanza kunipiga fix kuwa kuna gari limepata ajari na kwenye lile kulikuwa na wazungu wanatoka mgodini geita hivyo wale wazungu walidondosha dhahabu zao hivyo jamaa akaziokota na kwa sasa ni tajiri maana anaenda kuuza mjini
Dah jamaa akaendelea kutiririka namsikiliza tu ndo shetan akanipitia jamaa akanambia nimpe sh elf tano na pia nimpe baskel ile nami anipe madini nami niwe tajiri
Kwa utumbafu pasipo kujua kama naingizwa mkenge si nikampa aisee jamaa akanipa yale madini yaliyo kuwa yakiwaka waka
Akanambia weka mfukon watu wasikuone mdogo wangu hiyo ni bahati yako tu
Daah
Jamaa akachomoka na basikel yangu nikampata sh elf tatu ambayo nilikuwa nimepewa nyumban na MAMA
Nikaanza kurud zangu kwa mguu ile nafika home shap shap nikamfata MAMA ndan nikamwambia mama nimebadilisha baisikel na dhahab, nimepewa dhahabu, mama nani kakupa na hiyo dhahabu iko wapi si ndo nikampa aione
Aisee nilichezea kofi moja machoni had nikaona kama malyenge flan dizain rangi mbili flan hivi
Dah sitakaa nisahau kumbe jamaa alikuwaga amesaga chupa chupa tu wala hazikuwa dhahabu wala nini
Dah nilipigwa kiboya sana aisee
#KIBOYA SANA#
LONDON BOY
Sent using
Jamii Forums mobile app