Umewahi kuwa mtalii ndani ya Tz na kujionea maajabu haya?

Umewahi kuwa mtalii ndani ya Tz na kujionea maajabu haya?

J.K.Rayhope

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2011
Posts
316
Reaction score
31
Nabaki na maswali mengi sana kichwani,hivi kweli serikali yetu ina mpango gani wa kizalendo wa kukuza utalii wa ndani?Mlima Kilimanjaro uko tz,hivi kweli mjerman anatumia mamilioni ya maili kuja kuuona,halafu mimi mtz nasaga ndala na sina muda wa kufanya utali wa ndani,kwanza mimi kama mtz sijahamasishwa hata na wenye mamlaka,au hata kwa motisha.Kwa ujumla niseme wote tumelala.Kisiwa cha Saa 8 (mfano)akilichopo ndani ya Ziwa Victoria nililazimika kukitembelea baada ya mwl wangu wa somo la history nikiwa Kibasila sec,(Dar) kuzungumzia juu ya kisiwa hicho,nilipotembelea mwanza baadae niliamua kuupata ukweli wa maneno ya mwalimu wangu,niliridhika sana tu,utalii wa ndani kwa tz upo chini sana.Sehemu zote zenye vivutio tuzitembelee tujifunze,au ndio wageni kwanza wenyeji b'dae?Tuwe na desturi ya kujifunza NATUREWORK YA MUNGU.Uone fahari ya kuwa MTANZANIA
 
Bosi ungejua kwa hali ya kimaisha ilivo ngumu, sina hamu na ufahari wa Tanzania. Wenzetu wanachapa kazi ,wanalipwa vizuri then anachukua likizo kupumzika na ana akiba ya kutosha. Sisi hapa hatuna National Insurance, Ada za shule juu, sembe juu, umeme juu, maharage juu, bati juu..halafu mtu apate wapi hela ya kwenda Kilimanjaro? Mimi siwalaumu watu. Siku maisha yakiwa bora utashangaa watu watakavyojaa huku. Siyo kuwa hatupendi bali huwezi kuacha kulipa kodi ya meza kwa kuangalia wanyama ati!
 
Bosi ungejua kwa hali ya kimaisha ilivo ngumu, sina hamu na ufahari wa Tanzania. Wenzetu wanachapa kazi ,wanalipwa vizuri then anachukua likizo kupumzika na ana akiba ya kutosha. Sisi hapa hatuna National Insurance, Ada za shule juu, sembe juu, umeme juu, maharage juu, bati juu..halafu mtu apate wapi hela ya kwenda Kilimanjaro? Mimi siwalaumu watu. Siku maisha yakiwa bora utashangaa watu watakavyojaa huku. Siyo kuwa hatupendi bali huwezi kuacha kulipa kodi ya meza kwa kuangalia wanyama ati!
Nakuunga mkono Mkuu. Umesema kweli kabisa. Umetuwakilisha vema sisi wakesha-hoi. Mi natamani sana lakini kipato changu kimezidiwa na majukumu, hatimaye kuzima ndoto zangu.
 
Nabaki na maswali mengi sana kichwani,hivi kweli serikali yetu ina mpango gani wa kizalendo wa kukuza utalii wa ndani?Mlima Kilimanjaro uko tz,hivi kweli mjerman anatumia mamilioni ya maili kuja kuuona,halafu mimi mtz nasaga ndala na sina muda wa kufanya utali wa ndani,kwanza mimi kama mtz sijahamasishwa hata na wenye mamlaka,au hata kwa motisha.Kwa ujumla niseme wote tumelala.Kisiwa cha Saa 8 (mfano)akilichopo ndani ya Ziwa Victoria nililazimika kukitembelea baada ya mwl wangu wa somo la history nikiwa Kibasila sec,(Dar) kuzungumzia juu ya kisiwa hicho,nilipotembelea mwanza baadae niliamua kuupata ukweli wa maneno ya mwalimu wangu,niliridhika sana tu,utalii wa ndani kwa tz upo chini sana.Sehemu zote zenye vivutio tuzitembelee tujifunze,au ndio wageni kwanza wenyeji b'dae?Tuwe na desturi ya kujifunza NATUREWORK YA MUNGU.Uone fahari ya kuwa MTANZANIA

Mbona haujatuhamasisha sasa? Hicho kisiwa kina vivutio gani na sisi tutamani kwenda kukiona? Mimi nimetalia kiasi TZ, Kili nimepanda, Ngorongoro, Serengeti etc.
 
Mbona haujatuhamasisha sasa? Hicho kisiwa kina vivutio gani na sisi tutamani kwenda kukiona? Mimi nimetalia kiasi TZ, Kili nimepanda, Ngorongoro, Serengeti etc.

Utakuwa mmoja wa waliofaidi kauli mbiu ya CCM, 'Maisha Bora kwa Kila Mtanzania....mwenye uwezo wa kuchonga dili halali au haramu" teh teh teh
 
Utakuwa mmoja wa waliofaidi kauli mbiu ya CCM, 'Maisha Bora kwa Kila Mtanzania....mwenye uwezo wa kuchonga dili halali au haramu" teh teh teh

Wabongo wengi wakikata bajeti ya Bia,Kitimoto na za kuhonga wanawake mwezi mmoja tu wanapata pesa ya kupanda Kili, ni priorities tu.
 
Mbona haujatuhamasisha sasa? Hicho kisiwa kina vivutio gani na sisi tutamani kwenda kukiona? Mimi nimetalia kiasi TZ, Kili nimepanda, Ngorongoro, Serengeti etc.

Ilikuwa ni sanctuary ya wanyama tu na ndege. Sijui kama bado wapo.
 
nakumbuka nilikwenda kishule kutembelea mikumi lakini baada ya hapo sijabahatika kutembelea sehemu nyingine tena.
 
Utakuwa mmoja wa waliofaidi kauli mbiu ya CCM, 'Maisha Bora kwa Kila Mtanzania....mwenye uwezo wa kuchonga dili halali au haramu" teh teh teh

NCAA mwezi wa 12 huwa wanatoa gari kwa ajilia ya wazawa kwenda Ngorongoro kwa bei nafuu kama vikundi.
Nauli huwa around buku 10 na kiingilio ni kama Tsh 1500.
Msosi unajitegemea lakini ni day trip.
Pamoja na kwamba wanapigaga promo, lakini response bado inakuaga ndogo kinoma.
Huwezi niambia kwa mwaka mzima unashindwa kijipanga ukakosa buku 15 kuvisit mahali bomba kama Ngorongoro.
 
Wabongo wengi wakikata bajeti ya Bia,Kitimoto na za kuhonga wanawake mwezi mmoja tu wanapata pesa ya kupanda Kili, ni priorities tu.
Hzo nzo ni starehe kama kwenda kuangalia mlm kilimanjaro. Kwa hali ya umaskini tanzania na kwenye familia zetu c dhani kama tunachoice. Hizo hela za starehe ni bora kusomesha watoto wa ndugu na na marafiki. Tusiige kila kitu wanachofanya wazungu kwaani hali yao inawaruhusu.
 
Back
Top Bottom