Umiliki wa mali kabla ya ndoa na katika maisha ya ndoa

Umiliki wa mali kabla ya ndoa na katika maisha ya ndoa

joshydama

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2016
Posts
4,623
Reaction score
5,039
Habazi za mchana waungwana wa JF? Ni matumaini yangu kwamba wote hamjambo humu ndani.

Waungwana nimependa kuleta huu uzi mzuri kwenu nyie kwa lengo la kuwasaidia vijana wenzangu kuhusu suala la umiliki wa mali wakati mkiwa katika maisha ya uchumba na kila mmoja akiwa amechuma mali zake na mnatarajia kufunga ndoa. Pia ningependa kuelezea umiliki wa mali katika maisha ndoa.

Waungwana kama mjuavyo kila mtu ana haki ya kumiliki mali kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ibara ya 24(1). Mali inaweza kuwa ni Ardhi( kiwanja), nyumba, n.k. katiba inaposema kila mtu inamaanisha kwamba ni mtu mzima yeyote mwenye miaka 18 na zaidi(majority age). Kwa mantiki hiyo haibagi mwanamke kutomiliki mali. Ingawa kuna baadhi ya makabila huwa yanawanyima wanawake kumiliki mali kutokana na mila zao mfano Wakurya, wachaga na Wahaya. Mila zinazomnyima mwanamke asimiliki mali zipo kinyume na katiba ya JMT. Hivyo hizo mila hazifai hata kidogo.

Baada ya utambuzi ni wapi tunapata haki ya kumiliki mali naomba nizungumzie umiliki wa mali kwa wachumba kabla ya ndoa na katika maisha ya ndoa.

I. Umiliki wa mali kwa wachumba kabla ya ndoa.

- kama tulivyoona hapo juu ni kwamba kila mmoja anyone haki ya kumiliki mali. Hivyo basi kijana wa kiume au wa kike ana haki ya kumiliki mali kabla ya ndoa.

Ni nini kifanyike kulinda mali zako kabla ya kufunga ndoa ili kuepuka migogoro ya kisheria ya hapa na pale.

- Kama unamiliki mali zako binafsi mfano nyumba, mashamba, viwanja, magari na unataraji au una nia ya kufunga ndoa na mwenza wako mnatakiwa kuandaa mkataba wa kisheria (prenuptial agreement) ambao utabainisha na kuorodhesha mali zote za kila mmoja alizochuma na pia pawepo na kifungu dhahiri kinachoeleza kwamba mali zilizochumwa na mwenza mmoja kabla ya ndoa ni za kwake peke yake na hazimhusu mwenza mwingine.

Aidha, huo mkataba unatakiwa uweke wazi haki na majukumu ya wahusika katika mkataba huo pale ambapo mtaingia katika maisha ya ndoa.

Ni nini lengo la huu mkataba?

-Lengo kubwa ni kuzuia mgogoro wa mali inapotokea suala la kifo au talaka au pale unapokuwa una shida yako binafsi na unatakiwa kuuza au kuchukua mkopo kupitia hizo mali zako.

- Kumbuka kwa sasa pamekuwa na limbi kubwa la watu kutalakiana na mwisho wa siku kutaka kugawana mali tena katika usawa wa 50% kwa 50%.

- Hivyo basi pakiwepo kwa huo mkataba utazuia migogoro ya hapa na pale.

II. Umiliki wa Mali ndani ya Maisha ya Ndoa

- Baada ya kuingia katika maisha ya ndoa tambua kwamba mali mtakazochuma ni mali ya wanandoa wote wawili hata kama mwanaume au mwanamke atachuma kwa jitihada zake yeye mwenyewe hata kama utaandika kwa jina lako wewe tambua kwamba hiyo mali itakuwa ni mali ya wanandoa wote wawili au mali ya familia labda tu pawepo na mkataba kama nilivyoeleza hapo juu.

- Bila kuwepo na mkataba huo basi kutakuwa na dhanio kwamba hizo mali ni za familia( Matrimonial property or asset) hata kama mwanamke au mwanaume alikukuta na mali ambazo ulikuwa umechuma peke yako.

#Kadhalika, baada ya ndoa mnaweza kuamua kumiliki mali kwa pamoja(Joint ownership). Huu umiliki wa mali kwa pamoja unatambulika kisheria na ni mzuri sana kwa sababu kama mnamiliki kwa pamoja. Pindi mmoja wenu anapokufa malizo zote humilikiwa na aliyepo hai( Right of survivorship).

-Pia mtu mwingine hatakuwa na haki nazo ni mpaka pale tu wamiliki wote wa mali hizo mtakapokuwa hampo Duniani au mmefariki Dunia.
- Katika umiliki huu ni kwamba wote mnakuwa na hisa sawa( equal shares of ownership of the property)

-Hapa inabidi pawepo na mkataba unaonesha kwamba mnamiliki mali kwa pamoja.

#Mbali na umiliki ulioelezewa hapo juu, kuna umiliki unaitwa tenancy in common. Huu umiliki ni kinyume chake na huo umiliki wa pamoja (joint ownership). Katika umiliki huu, siyo lazima muwe na hisa sawa za umiliki wa mali bali mmjoa anaweza kuwa anamiliki 1/3 na mwingine 2/3 ya mali hiyo. Katika umiliki huu ni kwamba pindi mmoja wenu akifa hisa (share) yake itaenda kwa mtu aliyemuandika kwenye wosia wake. Pia unaweza uza hisa yako bila matatizo yoyote.

# Kadhalika ni ngumu sana kuhamisha maslahi ya mali ya familia kwenda kwa mtu mwingine bila kuwepo na ridha mwenza (Spousal Consent) mfano huwezi ukapewa mkopo na benki kwa kuweka rehani mali ya familia bila kuwepo na nyaraka ya kisheria inaitwa ridhaa mwenza( Spousal Consent).

#Karibuni kwa michango, maswali pamoja na nyongeza.

#Imeandaliwa na mshauri wa masuala ya kisheria katika masuala yafuatayo:-
  • Ndoa
  • Ardhi
-Mirathi

Ahsanteni sana.
 
Asante kwa elimu nzuri uliyotoa, na pia ingependeza kama ungetaja na hivyo vifungu vya sheria ili tuvipitie na kama una mifano ya kesi zinazohusiana na mambo haya japo kwa ufupi ili kuongeza ufahamu.
 
Hongera! Na Asantee Nimepata Mwangaza katika umiliki Mali maana bado niko Single......
Acha nichape kazi Nishajua Namana ya kuzilinda na Matapeli Watakao Kuja[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hongera! Na Asantee Nimepata Mwangaza katika umiliki Mali maana bado niko Single......
Acha nichape kazi Nishajua Namana ya kuzilinda na Matapeli Watakao Kuja[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sawa mkuu.
 
Asante kwa elimu nzuri uliyotoa, na pia ingependeza kama ungetaja na hivyo vifungu vya sheria ili tuvipitie na kama una mifano ya kesi zinazohusiana na mambo haya japo kwa ufupi ili kuongeza ufahamu.
Kesi siyo muhimu sana pale ambapo sheria ipo wazi mkuu.
 
Habazi za mchana waungwana wa JF? Ni matumaini yangu kwamba wote hamjambo humu ndani.

Waungwana nimependa kuleta huu uzi mzuri kwenu nyie kwa lengo la kuwasaidia vijana wenzangu kuhusu suala la umiliki wa mali wakati mkiwa katika maisha ya uchumba na kila mmoja akiwa amechuma mali zake na mnatarajia kufunga ndoa. Pia ningependa kuelezea umiliki wa mali katika maisha ndoa...
 
Habazi za mchana waungwana wa JF? Ni matumaini yangu kwamba wote hamjambo humu ndani.

Waungwana nimependa kuleta huu uzi mzuri kwenu nyie kwa lengo la kuwasaidia vijana wenzangu kuhusu suala la umiliki wa mali wakati mkiwa katika maisha ya uchumba na kila mmoja akiwa amechuma mali zake na mnatarajia kufunga ndoa. Pia ningependa kuelezea umiliki wa mali katika maisha ndoa...
Hivi pre nuptial agreements inaweza kuwa enforced ktk sheria zetu?

Yaani ktk mfumo wetu huu wa sheria, kweli pre nuptial unawezaje enforce? Kwa baadhi ya jurisdictions nyingine za wenzetu hiki kitu kinawezekana ila kwetu bado nna mashaka.

Naomba msingi wa kisheria ktk hili.
 
Habazi za mchana waungwana wa JF? Ni matumaini yangu kwamba wote hamjambo humu ndani.

Waungwana nimependa kuleta huu uzi mzuri kwenu nyie kwa lengo la kuwasaidia vijana wenzangu kuhusu suala la umiliki wa mali wakati mkiwa katika maisha ya uchumba na kila mmoja akiwa amechuma mali zake na mnatarajia kufunga ndoa. Pia ningependa kuelezea umiliki wa mali katika maisha ndoa.

Waungwana kama mjuavyo kila mtu ana haki ya kumiliki mali kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ibara ya 24(1). Mali inaweza kuwa ni Ardhi( kiwanja), nyumba, n.k. katiba inaposema kila mtu inamaanisha kwamba ni mtu mzima yeyote mwenye miaka 18 na zaidi(majority age). Kwa mantiki hiyo haibagi mwanamke kutomiliki mali. Ingawa kuna baadhi ya makabila huwa yanawanyima wanawake kumiliki mali kutokana na mila zao mfano Wakurya, wachaga na Wahaya. Mila zinazomnyima mwanamke asimiliki mali zipo kinyume na katiba ya JMT. Hivyo hizo mila hazifai hata kidogo.

Baada ya utambuzi ni wapi tunapata haki ya kumiliki mali naomba nizungumzie umiliki wa mali kwa wachumba kabla ya ndoa na katika maisha ya ndoa.

I. Umiliki wa mali kwa wachumba kabla ya ndoa.

- kama tulivyoona hapo juu ni kwamba kila mmoja anyone haki ya kumiliki mali. Hivyo basi kijana wa kiume au wa kike ana haki ya kumiliki mali kabla ya ndoa.

Ni nini kifanyike kulinda mali zako kabla ya kufunga ndoa ili kuepuka migogoro ya kisheria ya hapa na pale.

- Kama unamiliki mali zako binafsi mfano nyumba, mashamba, viwanja, magari na unataraji au una nia ya kufunga ndoa na mwenza wako mnatakiwa kuandaa mkataba wa kisheria (prenuptial agreement) ambao utabainisha na kuorodhesha mali zote za kila mmoja alizochuma na pia pawepo na kifungu dhahiri kinachoeleza kwamba mali zilizochumwa na mwenza mmoja kabla ya ndoa ni za kwake peke yake na hazimhusu mwenza mwingine.

Aidha, huo mkataba unatakiwa uweke wazi haki na majukumu ya wahusika katika mkataba huo pale ambapo mtaingia katika maisha ya ndoa.

Ni nini lengo la huu mkataba?

-Lengo kubwa ni kuzuia mgogoro wa mali inapotokea suala la kifo au talaka au pale unapokuwa una shida yako binafsi na unatakiwa kuuza au kuchukua mkopo kupitia hizo mali zako.

- Kumbuka kwa sasa pamekuwa na limbi kubwa la watu kutalakiana na mwisho wa siku kutaka kugawana mali tena katika usawa wa 50% kwa 50%.

- Hivyo basi pakiwepo kwa huo mkataba utazuia migogoro ya hapa na pale.

II. Umiliki wa Mali ndani ya Maisha ya Ndoa

- Baada ya kuingia katika maisha ya ndoa tambua kwamba mali mtakazochuma ni mali ya wanandoa wote wawili hata kama mwanaume au mwanamke atachuma kwa jitihada zake yeye mwenyewe hata kama utaandika kwa jina lako wewe tambua kwamba hiyo mali itakuwa ni mali ya wanandoa wote wawili au mali ya familia labda tu pawepo na mkataba kama nilivyoeleza hapo juu.

- Bila kuwepo na mkataba huo basi kutakuwa na dhanio kwamba hizo mali ni za familia( Matrimonial property or asset) hata kama mwanamke au mwanaume alikukuta na mali ambazo ulikuwa umechuma peke yako.

#Kadhalika, baada ya ndoa mnaweza kuamua kumiliki mali kwa pamoja(Joint ownership). Huu umiliki wa mali kwa pamoja unatambulika kisheria na ni mzuri sana kwa sababu kama mnamiliki kwa pamoja. Pindi mmoja wenu anapokufa malizo zote humilikiwa na aliyepo hai( Right of survivorship).

-Pia mtu mwingine hatakuwa na haki nazo ni mpaka pale tu wamiliki wote wa mali hizo mtakapokuwa hampo Duniani au mmefariki Dunia.
- Katika umiliki huu ni kwamba wote mnakuwa na hisa sawa( equal shares of ownership of the property)

-Hapa inabidi pawepo na mkataba unaonesha kwamba mnamiliki mali kwa pamoja.

#Mbali na umiliki ulioelezewa hapo juu, kuna umiliki unaitwa tenancy in common. Huu umiliki ni kinyume chake na huo umiliki wa pamoja (joint ownership). Katika umiliki huu, siyo lazima muwe na hisa sawa za umiliki wa mali bali mmjoa anaweza kuwa anamiliki 1/3 na mwingine 2/3 ya mali hiyo. Katika umiliki huu ni kwamba pindi mmoja wenu akifa hisa (share) yake itaenda kwa mtu aliyemuandika kwenye wosia wake. Pia unaweza uza hisa yako bila matatizo yoyote.

# Kadhalika ni ngumu sana kuhamisha maslahi ya mali ya familia kwenda kwa mtu mwingine bila kuwepo na ridha mwenza (Spousal Consent) mfano huwezi ukapewa mkopo na benki kwa kuweka rehani mali ya familia bila kuwepo na nyaraka ya kisheria inaitwa ridhaa mwenza( Spousal Consent).

#Karibuni kwa michango, maswali pamoja na nyongeza.

#Imeandaliwa na mshauri wa masuala ya kisheria katika masuala yafuatayo:-
  • Ndoa
  • Ardhi
-Mirathi

Ahsanteni sana.
Ili mambo yasiwe mengi ni kutumia Hakimi law
 
Hivi pre nuptial agreements inaweza kuwa enforced ktk sheria zetu?

Yaani ktk mfumo wetu huu wa sheria, kweli pre nuptial unawezaje enforce? Kwa baadhi ya jurisdictions nyingine za wenzetu hiki kitu kinawezekana ila kwetu bado nna mashaka.

Naomba msingi wa kisheria ktk hili.
<nimecopy mahali>

In Tanzania, the Law of Marriage Act is silent on the issue. The Courts have also not been brought to test this and hence our answer is based on our reading of the subject in addition to the general legal framework in Tanzania.

The legality of these type of agreements in Tanzania will very likely depend on the way the pre nuptial agreement is drafted. If it undermines morality or if it is against public policy, the agreement will likely be held to be void. The next question is what types of provisions would undermine morality or would render the agreement against public policy. This will likely be a subjective test and the background of the parties, their religion and culture may likely play a key role in determining this.

The law here looks at marriage as a life time bond. This might have been a strong notion when the law came into effect in the early 70’s but with decreasing tolerance levels amongst couples today, increased level of openness and awareness of the law have resulted in record high divorce rates at the moment. This is not only true in Tanzania but all over the world. If the Courts were to look at a public policy from a broader angle considering the changing times (we are not sure if they would), we do not see why these agreements should be held illegal. However as said above, this has not been tested in Courts here and much as you would like us to, we cannot give you a firm answer.

There is however no harm in drafting this kind of agreement and we highly recommend that you do so. It would not only save a lot of time, money and energy to litigants but also lessen the burden on Courts. If the agreement is held not to be tenable or executable in a court of law, it can at best be an indication of the intent of the parties. A clause to exclude any provisions of the agreement that are held to be illegal should be included so that the other provisions of the agreement may be held to be enforceable.
 
Povu lote Hilo usikute Mali unazoziongelea Ni nyumba moja.
 
Back
Top Bottom