Umiss sasa kwa kadi ya kliniki

Umiss sasa kwa kadi ya kliniki

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Hii ni kutoka kwa kamati ya miss Tanzania kwamba kuepusha utata wa umri na udanganyifu kamati imeamua kuanzia sasa warembo wote wanaotaka kugombea taji hilo maarufu waonyeshe pia na kadi zao za kliniki

Yaani baada ya sekeseke la binti mtemvu ndio kamati imekuja na ufumbuzi huu...!

======================================================================================================================


Kwa ufupi
Alisema kuwa dunia ya leo imebadilika na kamwe huwezi kumuamini mtu moja kwa moja na kwa kujua hilo, tumeamua kuchukua tahadhari mapema.

Katika hali ya kuchukua ahadhari zaidi, waandaaji wa mashindano ya kumsaka Miss Universe Tanzania 2014, wameamua kutumia kadi za kliniki za watoto kujiridhisha katika suala la kupata umri halisi wa warembo wao.

Mratibu wa mashindano hayo, Mwanakombo Salim alisema kuwa warembo hao 12, watakaochuana Ijumaa wamepewa sharti hilo ili kuepuka malumbano ya umri.
Mwanakombo alisema suala la umri ni nyeti na mbali ya kutumia vyeti vya kuzaliwa, wao wameamua kwenda mbali zaidi kwa kutaka kadi zao za kliniki za utotoni.

"Miss Universe anatakiwa kuwa na vigezo mbalimbali pamoja na umri uziozidi miaka 25, asiwe ameolewa wala kuzaa mtoto, lakini hivi karibuni kumetokea malumbano ya umri kwa wenzetu, sitaki kuingia huko, sisi tumeamua kwenda mbali zaidi na warembo wameambia hayo na tunashuru hakuna tatizo mpaka sasa," alisema Mwanakombo.

Alisema kuwa dunia ya leo imebadilika na kamwe huwezi kumuamini mtu moja kwa moja na kwa kujua hilo, tumeamua kuchukua tahadhari mapema.

Awali Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications, Maria Sarungi Tsehai alisema kuwa mwaka huu wamepanua wigo wa mashindano yao kwa kumshirikisha mrembo kutoka Zanzibar. Maria alimtaja mrembo huyo kuwa ni Zahra Bedel ambaye tayari yupo kambini.

Warembo wengine ambao wameanza kambi kwa ajili ya mashindano hayo ni Christine Halamga, Amina Sangalwe, Faith Felix, Belinda Lugenge, Magreth Geddy na Carolyne Benard ambao wote wanatoka Dar es Salaam.

Wegine ni Nale Boniface, Neema John (Dar es Salaam), Zahra Bedel (Zanzibar), Lucy Charles, Faudhia Haruna (Mwanza) na Atukuzwe Fabian kutoka Mbeya.

Alisema kuwa maandalizi ya mashindano hayo yamekwisha kamilika na mshindi atachukua taji kutoka kwa Miss Universe anayemaliza muda wake, Betty Boniface ambaye kwa sasa anafanyakazi Azam Televisheni.

CHANZO: Mwananchi
 
Hii ni kutoka kwa kamati ya miss Tanzania kwamba kuepusha utata wa umri na udanganyifu kamati imeamua kuanzia sasa warembo wote wanaotaka kugombea taji hilo maarufu waonyeshe pia na kadi zao za kliniki
Yaani baada ya sekeseke la binti mtemvu ndio kamati imekuja na ufumbuzi huu...!

mkuu, hizo kadi za kliniki zinatolewa na malaika??
 
Hakuna kudanganya umri tena

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kiukweli na kiuhalisia kabisa mamiss wengi ni mamrs wasio rasmi wengi wao walishatotoa na kuua zaidi ya mara moja....!!!
Ukweli ndo huo saiz wakitaka mamis wchukue miaka 12 hao hata kama wanakuwa hawana utepe lakn kuchomoa mimba wanakuwa bado
 
bibi bomba arudishe taji la watu kwanza
 
Wawe wanachekiwa kama ni virgin, na iwe ojii kama ni ya kichina hakuna kushiriki.
 
Sasa cheti cha Kliniki watakuwa wanawapima pia Ultrasound hahaha
 
Itabidi wazazi wanaotaka watoto zao kuwa ma miss wahifadhi kadi za clinic...... hii itakua imesaidia wazazi kupanga future ya mtoto pindi anapozaliwa.....hihihihi Daaaah ama kweli!!!!
 
Itabidi wazazi wanaotaka watoto zao kuwa ma miss wahifadhi kadi za clinic...... hii itakua imesaidia wazazi kupanga future ya mtoto pindi anapozaliwa.....hihihihi Daaaah ama kweli!!!!

Hahahahaaaaa
 
mshana jr ..miss tz na miss universe ni vitu viwili tofaut kabiSaaaa.

Miss tz inaandaliwa na lino agency ya lundenga

Miss universe inaandaliwa na compass comm. Ya maria sarungi t.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom