Pre GE2025 Ummy Mwalimu awahimiza wakazi wa Tanga kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura

Pre GE2025 Ummy Mwalimu awahimiza wakazi wa Tanga kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu amewahimiza wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, ili kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Mhe. Ummy ametoa wito huo, Februari 14, 2025, baada ya kuboresha taarifa zake katika Kituo cha Suji, Mtaa wa Suji, Kata ya Mzingani.

"Nahimiza wananchi wa Tanga Mjini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao. Pia, kwa wale wanaotarajia kufikisha umri wa miaka 18 mwezi wa 10, wanapaswa kujiandikisha mapema ili wapate vitambulisho vya kupiga kura ambavyo vina faida nyingi, ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti benki na kuomba mikopo," alisema Mhe. Ummy.

 
Wanatuhimiza tukajiandikishe kupiga kura wakati tukipiga kura,kura za tume CCM na polisi CCM ndizo zinazopita,kura zetu zinakuwa haramu.
 
Waache siasa ,michezo Yao tunaijuaa jinsi wanavyocheza na masanduku ya kura🤔
 
Kitambukisho chakupigia kura ni cha kupigia kura sio vingenevyo.

Tulipewe Nida ili iweje?
 
Back
Top Bottom