Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) yatoa tena lori la vifaa vya msaada Hanang'

Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) yatoa tena lori la vifaa vya msaada Hanang'

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda amekabidhi Lori tatu za vifaa vya Msaada kwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe Queen Sendiga ikiwa ni muendelezo utoaji wa misaada kwa watu waliopata majanga.​

Akizungumza Mara baada ya kukabidhi Misaada hiyo Mwenyekiti Chatanda amesema msaada huo ni Muendelezo wa ahadi waliyotoa Kusaidia watu waliopatwa na Maafa ya Mafuriko Hanang kama Mashuka 2000, Khanga 400, balo za Nguo, taulo za kike, Shuka za Kimasai, Vikombe 1440 na Vifaa mbalimbali.

"Mimi kama Mwenyekiti wa wanawake Tanzania kwa Kushirikiana na Makamu wangu na wanawake wote tutaendelea kuleta misaada mbalimbali ili kuweza kuwafariji wananchi wetu wa Manyara.

#UWTImara #JeshiLaMama #KaziIendelee

WhatsApp Image 2023-12-08 at 16.44.20.jpeg
View attachment 2836603
WhatsApp Image 2023-12-08 at 16.44.20(2).jpeg
 
Wenyewe wanaishi kwenye maisha ya anasa wao na familia zao, halafu wanarubuni raia na kanga? Hii haina tofauti na zile T-shirt wanazogawa wakati wa uchaguzi.
 
UWT motomoto. Hongera Mwenyekiti wetu. Kazi nzuri. Ziwafikie wahanga tu ndio ombi letu. Naipenda hii modern UWT.
 
Hii ndio UWT inayotambuliwa na wanawake wote Tanzania kuwa ni mtetezi wa mwanamke. Ni taasisi imara na bora kabisa Duniani. Ndio maana huwezi ukamwambia mtu mwenye akili Timamu apeleke kura yake ya ndio upinzani na kuiacha CCM. Kila mtanzania anajuwa kuwa CCM Ndio chama pekee chenye uchungu na maisha yao.ndio maana kwa sasa kipo bega kwa bega na wahanga.

Sasa nenda kule Bawacha uwaulize wamefanya nini Kusaidia wahanga uone watakavyo toa macho.
 
Hii ndio UWT inayotambuliwa na wanawake wote Tanzania kuwa ni mtetezi wa mwanamke. Ni taasisi imara na bora kabisa Duniani. Ndio maana huwezi ukamwambia mtu mwenye akili Timamu apeleke kura yake ya ndio upinzani na kuiacha CCM. Kila mtanzania anajuwa kuwa CCM Ndio chama pekee chenye uchungu na maisha yao.ndio maana kwa sasa kipo bega kwa bega na wahanga.

Sasa nenda kule Bawacha uwaulize wamefanya nini Kusaidia wahanga uone watakavyo toa macho.
Chama chenu wanawake wajane kinawajali mnoo.
 
Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda amekabidhi Lori tatu za vifaa vya Msaada kwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe Queen Sendiga ikiwa ni muendelezo utoaji wa misaada kwa watu waliopata majanga.​

Akizungumza Mara baada ya kukabidhi Misaada hiyo Mwenyekiti Chatanda amesema msaada huo ni Muendelezo wa ahadi waliyotoa Kusaidia watu waliopatwa na Maafa ya Mafuriko Hanang kama Mashuka 2000, Khanga 400, balo za Nguo, taulo za kike, Shuka za Kimasai, Vikombe 1440 na Vifaa mbalimbali.

"Mimi kama Mwenyekiti wa wanawake Tanzania kwa Kushirikiana na Makamu wangu na wanawake wote tutaendelea kuleta misaada mbalimbali ili kuweza kuwafariji wananchi wetu wa Manyara.

#UWTImara #JeshiLaMama #KaziIendelee

View attachment 2836602View attachment 2836603View attachment 2836604
Hongereni na ahsante UWT.
 
Back
Top Bottom