Umri wa chuji wakwama...

du kama ni ndugu wa tumbo wamepishana miezi mitatu kama watoto wa paka mimba za miezi 3
 

yesuuuuu unisamehe kwa kufungua hii mada loh nchi mbaya hii
 
Yoyo yoyooo ipo siku mtavunja ndoa za watu kwa udadisi huu wallahi kwi kwi aisee very fantastic wife ameshatoa keki ya bday mara anasoma anakuta kumbe unaitaji keki nyingine ya bday teeehh teehhh
tanzana eehh nchi yangu eeeehh yapendeza eehhh karibuni muone

mnamkumbuka huyu mtotojaman kaliimba sijui nchi gani kadogo mambo yake sijui nacho kana miaka 5 ile ile
 
Mimi nilishangaa sana kuna dogo zamani namfahamu alikuwa ananzidi umri kinoma noma akasajiliwa timu moja hivi aiseeee eti akawa na 18yrs....wakati mie wakati huo nilikuwa nakimbilia 30+
 
Inavyosemekana wachezaji wa Africa wanaochezea soka Ulaya wenye umri sahihi ni wale walianza kucheza toka wakiwa watoto wakiwa huko ka Etoo, ila hawa wengine wazamiaji wengi ni wasanii tu.
 
cha ajabu huyu ana passport inayoonyesha hiyo miaka so wazimu sio tu kwa chuji hadi serikali washenzi kabisa
 
jamani..unaumiza kichwa buree..wachezaji wakibongo wana umri halisi..na pia wana umri wa kwenye passport...na kama hamjui hata wale wa copa cocacola wanaghushi umri..nina ushahidi wa kutosha...na hata pale RITA na UHAMIAJI kuna watu wanahusika na hili..hasa kipindi hiki cha usajiri wa copa cocacola...
 
Tuangalie utunzaji wa kumbukumbu pia. hawa wachezaji kuna wakati wana wekewa rekodi bila kujua. mfano ni swala la nurdin ambapo simba na tff walikuwa na rekodi tofauti. sababu kubwa ni kufanya mambo ya zima moto hasa pale wanapokuwa wanawahi deadlines kama zile za caf n.k
 
timu yetu ya vijana ikiwa inacheza siku zote huwa nashabikia timu pinzani, kuna wachezaji u-21 walikuwa wamezidi miaka 10 na mbaya zaidi TFF inaengineer hayo
 

Huo wenyewe wanaita umri wa kutafutia maisha ambao unakua kwenye ppt za kusafiria,hili si tatizo la tanzania ni la africa nzima sema tanzania tumechelewa sana katika hili wenzetu walianza mapema toka enzi za kina abedi pele na ghana ndio nchi iliyoathirika zaidi miaka hiyo wazungu walikua wakishangaa why ghana inafanya vizuri sana kwenye mashindano ya vijana lakini ilikua haingii kwenye world cup kitu ambacho si cha kawaida kweye mambo ya soka kwani inaaminika timu nzuri ya vijana ya leo ndio timu bora ya taifa ya kesho sasa haiyumkiniki timu ya vijana ishinde kikombe ya africa kwa vijana au world cup ya vijana halafu next world cup ya wakubwa nchi husika ishindwe hata kupata tiketi ya kushiriki....!wale vijana wanakuwa wameenda wapi???

Wazungu wakawaambia ghana kinaga ubaga ghana kwamba "wanachezea" umri wa wachezaji wao jambo ambalo halitawafikisha popote kwa kuwa ukidanganya mchezaji wa miaka 25 eti ana chini ya miaka 18 ni wazi miaka mitatu toka udanganye ambapo mchezaji aliyekua kweli na 18 anatakiwa kuwa na 21 umri ambao ndio haswa wa mcheza husika kuitumikia timu ya wakubwa huyo kijana atakua miaka 28,yani miaka 2 kabla ya kuwa veteran wakati huo ndio mchakato wa kutafuta tiketi za kwenda world cup unaanza so atakua kisha choka kuhimili mikiki mikiki ya damu changu 20-25!

Wote kina drogba wanaingia kwenye mkumbo huo huo,ndio maana unamuona mtu kama Anelka licha ya kuwa mkubwa zaidi ya Drogba bado ana uwezo,yuko fit haumii umii kila wakati kama Drogba.Anelka ni mweusi kama sisi lakini ikumbukwe amezaliwa na kukulia ulaya ambako hakuna u.puuzi wa "kuchezea' umri wa vijana!
 
Agreed............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…