Umri wa miaka 40

Umri wa miaka 40

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Huu ndio umri wa watu wengi wa lala salama katika mahusiano ya kufa na kuzikana.

Kama umefikisha huo umri,na mahusiano yako hayaeleweki eleweki, chukua hatua mapema.

Kama ni mwanamke, na una kipato na hujapata mtu wa kueleweka, tafuta mwanaume yeyote choka mbaya ambaye atakuheshimisha na kukupa faraja huko tuendako; awe karibu na wewe utakapoanza kukutana na changamoto za uchakavu wa viungo vya mwili, maradhi n.k

Kama umeolewa,na unaona kabisa ndoa yako haitakuwa na manufaa pale uchakavu wa mwili utakapotokea, nakushauri uipige chini ukatafute wa kufanana na wewe ata asiyekuwa na kipato; kwa sababu huko tunakoelekea utu unahitajika zaidi kuliko pesa.

Kama ni mwanaume na huna mahusiano ya kueleweka, tafuta mwanamke yeyote bila kuangalia sura, muonekano wala kipato, tafuta mwenye utu muanze kusindikizana kwenye nyakati zako za mwisho wa hapa duniani.

Kama umeoa, na bado unaona chenga chenga; piga chini na utafute mtu sahihi mwenye utu; huko tuelekeapo tunahitaji faraja ya utu zaidi kuliko muonekano wa sura na shepu.

Pia kumbuka, katika umri huo wewe ndio baba na ndio mama; baba yako na mama yako waliokuzaa watakuwa choka mbaya kwa uzee na hawatakuwa na msaada mkubwa na wewe; kwa hiyo ile kauli ya kusema nitakimbilia kwa baba au mama, hiyo inakuwa haipo.

Hapo ndipo ile kauli inakuja; ''asiyefunzwa na mamaye........''

Kwa leo ni hayo tu.​
 
Strategic relationship inatakiwa ianze mapema unapoingia miaka 30, Ila vijana wengi huwa hatuelewi namna ya kuset mikakati katika mahusiano, na hata kama tukikumbushwa huwa hatuzingatii na tunakuwa tunaendelekeza shape, sura na hali ya fedha.

Wenza wazuri wa kufanya maisha hawapatikani kwenye 40s, kwenye umri huwa unatakiwa uwe tayari una bond nzuri na mwenzako. Mtafuta mwenza kimkakati wakati upo collage ama University mnapokuja mtaani unaimarisha familia kwa kuweka pamoja mawazo yenu na kuongeza watoto.

Utakapokutana kwenye 40 mzee tunakuwa tushachafuliwa na hali mbaya mbaya nyingi, kukata tamaa na machukizo ya kisirani cha maisha. Wengi wetu tunakuwa tumeumizwa sana akili za kimapenzi zishadumaa hatuwezi kuamini na uchaguzi wetu unakua wa kujinufaisha sana.

Mwanamke anakaa kwa mwanaume kisa anastirrika, ila moyoni hana mahaba na mwenzawake. Mapenzi anayatengeneza ukiwa nawe ila ana mwenza akilini mwake anamtawala muda wote na ndio maana kesi za kutokufikishana kileleni ziko nyingi umri huo.Hisia zimekata kwa visirani tulivyopitia awali.

Hali mtaani sio shwari, changamoto za kiuchumi ni nyingi ambazo husababisha matatizo mingi ya kijamii hasa kimahusiano.

KIJANA WA 20s FANYA CHAGUO LAKO MAPEMA UKIWA UNANGUVU NA MAARIFA. KUWA MKWELI NA UPAMBANE NA USALITI MAPENZI YANAHARIBU MAARIFA YA MAISHA.
 
Strategic relationship inatakiwa ianze mapema unapoingia miaka 30, Ila vijana wengi huwa hatuelewi namna ya kuset mikakati katika mahusiano, na hata kama tukikumbushwa huwa hatuzingatii na tunakuwa tunaendelekeza shape, sura na hali ya fedha.

Wenza wazuri wa kufanya maisha hawapatikani kwenye 40s, kwenye umri huwa unatakiwa uwe tayari una bond nzuri na mwenzako. Mtafuta mwenza kimkakati wakati upo collage ama University mnapokuja mtaani unaimarisha familia kwa kuweka pamoja mawazo yenu na kuongeza watoto.

Utakapokutana kwenye 40 mzee tunakuwa tushachafuliwa na hali mbaya mbaya nyingi, kukata tamaa na machukizo ya kisirani cha maisha. Wengi wetu tunakuwa tumeumizwa sana akili za kimapenzi zishadumaa hatuwezi kuamini na uchaguzi wetu unakua wa kujinufaisha sana.

Mwanamke anakaa kwa mwanaume kisa anastirrika, ila moyoni hana mahaba na mwenzawake. Mapenzi anayatengeneza ukiwa nawe ila ana mwenza akilini mwake anamtawala muda wote na ndio maana kesi za kutokufikishana kileleni ziko nyingi umri huo.Hisia zimekata kwa visirani tulivyopitia awali.

Hali mtaani sio shwari, changamoto za kiuchumi ni nyingi ambazo husababisha matatizo mingi ya kijamii hasa kimahusiano.

KIJANA WA 20s FANYA CHAGUO LAKO MAPEMA UKIWA UNANGUVU NA MAARIFA. KUWA MKWELI NA UPAMBANE NA USALITI MAPENZI YANAHARIBU MAARIFA YA MAISHA.
Changamoto ni nyingi
 
Mbona kama mawazo ya kukata tamaa haya mkuu🤔🤔
Wamekusikia lakini
Sio kukata tamaa mkuu, ndio hali halisi; kuna mshangazi hapa mtaani alikuwa na mtazamo kama wako, tumeenda kumjuia hali huko hospitalini, kuna cha kujifunza.
 
Haijalishi umri umekwenda kiasi gani,nashauri tusiokoteokote tu...chagua moyo kile umetaka ili kikikubomokea asiwepo wa kumlaumu.Utuuzima kuwa na stress na mahusiano haitakiwi
 
Back
Top Bottom