Umri wa Tupac na Martin Luther King Jr unatia shaka

Umri wa Tupac na Martin Luther King Jr unatia shaka

KyemanaMugaza

Member
Joined
Jan 7, 2025
Posts
89
Reaction score
138
Salama wakuu wote wa hili jukwaa

Mara nyingi nimekuwa na wasiwasi juu ya umri sahihi wa hawa watu wawili maarufu katika historia ya dunia, mwanamziki Tupac Amar Shakur na mwanaharakati wa haki za binadamu Martin Luther King Jr Huwa naona maumbile yao au mwonekano wao unaonyesha kuwa walikuwa na umri mkubwa kuliko ule ambao tumeandikiwa wakati wa kufa kwao

1. Je, huko nje suala la kudanganya umri huwa lipo labda sisi ndo hatujui?
2. Je, yawezekana hao watu hudanganya umri ili kuzua mijadala ambayo itawaongezea umaarufu wa kujadiliwa mara kwa mara?
3. Je, ikibaainika mtu hasa maarafu kadanganya umri , hili kosa linaweza kuleta impact yoyote kwenye career yake mfano kushuka kipato na kukosa udhamini wa makampuni ya biashara?
3. Kama ni kweli hilo lipo kwanini mtu adanganye juu ya umri wake?

Hili jambo ni common sana kwa nchi za kiafrika hasa kwa wachezaji wa mpira wa miguu.

Yote kwa yote Martin Luther King Jr na Tupac Amar Shakur wameacha legacy kubwa sana licha ya kuishi muda mfupi sana hapa duniani, watu kama hao ni wachache sana kwenye kizazi cha sasa. Their legacy still lives on.

Nawasilisha
 
2pac anaweza kuwa kweli alikuwa na 25 ila ni vile amepitia heka heka kwenye maisha. Vipindi vigumu vinazeesha watu na vile alinyoa nywele tena na zile busara akaonekana kama mkubwa zaidi.

Lakini mkuu hauonagi hata huku bongo kuna watu wanaanzaga kwa kuzeeka halafu wakipata hela ndio wanarudi kuwa vijana? Vipindi vigumu kwenye maisha vinazeesha.
 
Back
Top Bottom