Umuhimu wa kilimo

Umuhimu wa kilimo

Nsibwene

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2017
Posts
227
Reaction score
160
Nilikuwa nasoma bajeti ya elimu.

Nimeona mambo mazuri ya vyuo vya ufundi vya cheti, astashahada, stashahada na shahada, na kuona kila wilaya inatarajiwa kuwa na chuo cha veta na vinginevyo. Najua ni jambo jema. Lakini havyo vyote na vya kujiajiri na wanahitaji kula.

Ninachojiuliza kwanini hakuna mkazo mkubwa kuhusu kilimo kielimu?

Sijaona po pote inaelezea vyuo au mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kilimo yanafanyika. Nashukuru kwa kuongeza vyuo vikuu lakini tunahitaji elimu ndogo ndogo kuhusu kilimo na mifugo na umwagiliaji isambae kwa wananchi au kuanzisha vyuo vya muda mfupi ili watu wajitegemee kwa kilimo.

Je wizara ya elimu haihusiki na hili?
 
Wao wanaamini kuwa kilimo ni nguvu,wakati sisi wakulima tunaamini kilimo ni uwekezaji kuanzia mtaji,elimu,muda mpaka maamuzi.
 
Wao wanaamini kuwa kilimo ni nguvu,wakati sisi wakulima tunaamini kilimo ni uwekezaji kuanzia mtaji,elimu,muda mpaka maamuzi.
Sasa shivi serikali, wanafanya juhudi ya kuwapeleka wanafunzi wa vyuo kwenye kilimo nakuwapa mitaji ni jambo jema; fikiria wakulima walioko vijijini ambao wamezoea kilimo cha enzi na enzi; tutawasaidia vipi?
Tumeona kampeni mbalimbali zinazofanywa huleta matunda yenye tija. Kama kweli kilimo ni uti wa mgongo katika nchi hii ni muhimu kuwekeza kwenye elimu ya kilimo na mifugo kimaeneo. Hao wa VETA na Vyuo vya jumuia watakula hivyo viwanda vyao au....
 
Sasa shivi serikali, wanafanya juhudi ya kuwapeleka wanafunzi wa vyuo kwenye kilimo nakuwapa mitaji ni jambo jema; fikiria wakulima walioko vijijini ambao wamezoea kilimo cha enzi na enzi; tutawasaidia vipi?
Tumeona kampeni mbalimbali zinazofanywa huleta matunda yenye tija. Kama kweli kilimo ni uti wa mgongo katika nchi hii ni muhimu kuwekeza kwenye elimu ya kilimo na mifugo kimaeneo. Hao wa VETA na Vyuo vya jumuia watakula hivyo viwanda vyao au....
Bado tunasafari ndefu kifikra
 
Back
Top Bottom