Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
Protein ni muhimu mno kwa ujengaji wa mwili wa mama na wa mtoto. Katika trimester ya pili na
tatu(miezi ya tatu ya pili na ya mwisho) mtoto anakuwa kwa kiasi kikubwa sana na ni katika kipindi
hiki mama asipopata protein ya kutosha basi mwili utafanya kazi kubwa na kuathirika.
Katika trimester ya kwanza na pili mama anahitaji 60 - 80gms za protein kila siku hii huongezeka
mpaka 80 - 100 gms katika trimester ya tatu.
Kuna vyakula vingi sana vyenye protein kwahiyo huwezi kuboreka na kukosa choice ya vyakula.
Chini ni mifano ya vyakula vya Protein na kiwango cha Protein ili kukusaidia kujua jinsi ya
kutosheleza mahitaji yako ya protein ya kila siku.
Vyakula vyenye asilimia kubwa ya Protein
Mifano ya vyakula vyenye gram 20 ya protein katika makundi mbali mbali.
Maharage, Jamii ya kunde na Karanga
3oz Karanga
Kikombe kimoja na nusu cha maharage yaliyopikwa
Maziwa, jamii ya maziwa na mtindi
2/3 kikombe cha cottage cheese
Vikombe viwili vya mtindi
3oz ya aina nyingine za cheese/jibini kama swiss, cheddar
2oz cheese aina ya parmesan
Mayai matatu
Glass mbili na nusu ya maziwa
Nyama na Samaki
3oz, nyama aina ya kuku, ya ngombe, mbuzi, nguruwe, turkey
3oz samaki aina ya salmon, trout tilapia
Shrimp/kamba wakubwa 17 au kikombe kimoja na nusu cha shrimp wadogo
31/2 nyama ya lobster, crab