Umuhimu wa watu Maishani

Umuhimu wa watu Maishani

Nyanda Banka

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2023
Posts
304
Reaction score
1,054
Siku utakapotambua kuwa pesa hazimziki mtu ndiyo utakapojua thamani ya watu,

Tuishi kwa kupendana na kuheshimiana LIFE HAS NO FORMULA
 
Hata watu wakikuzika, wewe unafaidika nini? Utaliwa na funza, utaoza na hakuna maumivu yeyote.
Hata mzoga wako uliwe na wanyama wa porini au mbwa na nguruwe, ni sawa tu na aliyezikwa na watu.

Tuishi kwa kupendana kwa sababu tunahitajiana katika maisha. Si kwa sababu tutazikana.

Siku utakapotambua kuwa pesa hazimziki mtu ndiyo utakapojua thamani ya watu,

Tuishi kwa kupendana na kuheshimiana LIFE HAS NO FORMULA
 
Bora ukose pesa ila upate wa kukuzika?
 
Misemo ya masikini bwana! 😁😁

Hivi kwanini masikini tuna roho mbaya sana? Mfano mleta anataka wote tusiwe na hela bali tuweke tu utaratibu wa kulogana na kuzikana
 
Hata watu wakikuzika, wewe unafaidika nini? Utaliwa na funza, utaoza na hakuna maumivu yeyote.
Hata mzoga wako uliwe na wanyama wa porini au mbwa na nguruwe, ni sawa tu na aliyezikwa na watu.

Tuishi kwa kupendana kwa sababu tunahitajiana katika maisha. Si kwa sababu tutazikana.
Hoja muruwa.
Tunategemeana sana.
 
Watu weusi tuna mambo ksng ksng sana kmmk hizi taka taka za hivi ndizo zimejaa kwenye jamii zetu bado zina akili za ksng za kufuatilia maisha ya watu.
 
Hakuna mtu alikosa wa kumzika, tena ni bora ukiliwa na wanyama pori au samaki kuliko hao funza na nyenyere.
Utakosa wa kukuuguza au kukudhamini Polisi au mahakamani lakini hutakosa wa kukuzika.
Marehemu ana ndugu, jamaa na marafiki wengi.
 
Ushawahi kuta maiti imeozea mtaani??? We ishi utakavyo,,, ukifa utazikwa na manispaa!!
 
Umeniwahi dokta. Nizikwe na mtu mmoja au na dunia nzima kama alivyozikwa Mandela mi inanisaidia nini? I am dead!

Watu wamegeuza misiba sasa kuwa sehemu ya kujionyesha na kuzidiana idadi ya waombolezaji.

Kwa upande wangu hata wanitupe porini niliwe na wanyama haitaniathiri cho chote as long as I am not there.

When I am alive, my death is not. When my death is "alive", I am not. So ngoma droo!

Na kwa hili nawapenda sana Waislamu. Unakata moto sasa hivi saa saba mchana ushazikwa tena kwenye mkeka tu bila mbwembwe za kuwekwa kwenye sanduku la mamilioni, maua, kwaya na utopolo mwingine
😂😂😂
 
Siku utakapotambua kuwa pesa hazimziki mtu ndiyo utakapojua thamani ya watu,

Tuishi kwa kupendana na kuheshimiana LIFE HAS NO FORMULA
Acha uongo wewe, ukiamua pesa ikuzike inawezekana. Ni huku tu bongo ila kwa wenzetu kuna kampuni za mazishi zinasimamia kila kitu hadi kukuzika...hatq majirani msipokuja mtu anazikwa.
 
Back
Top Bottom