Una kipaji usichokitumia?

Una kipaji usichokitumia?

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
2,977
Reaction score
3,798
Mimi kipaji changu ambacho sikitumii kabisa ni kupiga gitaa, hasa hasa gita la solo. Hiki kipaji Mungu alinipa toka utoto wangu,nilianza kwa kupiga madebe, makopo, nikapiga marimba, zeze, ndipo nikawa nawafata wana miziki nawaomba gitaa wananipa na hatimae nikafaulu sana nikawa mpiga mzuri mno.

Nilivyoenfa kusoma nje ya nchi niliendelea kupiga gitaa sana,na nikawa najilipia kozi ndogo ndogo za miziki. Nilipokuwa likizo narudi tz na kaka yangu mmoja alikuwa tajiri na biashara nyingi, basi nikawa namsaidia kazi zake na alinipenda sana,kila akisafiri anasafiri nami ili nimsaidie kazi.

Siku moja tukaenda Mwanza tukakaa Mwanza Hotel, jumamosi huwa na dinner and dance, kuliliwa na residence band,ambayo mida ya mchana huwa wanafanya mazoezi, nami siku moja nikaenda nikaomba kufanya nao mazoezi, wakanipa gitaa na nilipiga vizuri sana na nikawa rafiki yao sana.

Siku moja mpiga solo wao akaugua ghafla akiwa jukwaani na watu wamejaa na mimi na kaka yangu tupo hapo, basi wakaja kuniomba nikapanda jukwaani nikalikung'uta gitaa la solo vizuri hadi saa 8 ndipo nikaenda kulala.

Kaka yangu alishangaa kabisa.Siku nyingine ntapa stori nikampigia solo marehemu king kikii.
 
Hivi kupiga chabo ni kipaji Kaka ?
Mimi kipaji changu ambacho sikitumii kabisa ni kupiga gitaa,hasa hasa gita la solo.Hiki kipaji Mungu alinipa toka utoto wangu,nilianza kwa kupiga madebe,makopo,nikapiga marimba,zeze,ndipo nikawa nawafata wana miziki nawaomba gitaa wananipa na hatimae nikafaulu sana nikawa mpiga mzuri mno.Nilivyoenfa kusoma nje ya nchi niliendelea kupiga gitaa sana,na nikawa najilipia kozi ndogo ndogo za miziki.Nilipokuwa likizo narudi tz na kaka yangu mmoja alikuwa tajiri na biashara nyingi,basi nikawa namsaidia kazi zake na alinipenda sana,kila akisafiri anasafiri nami ili nimsaidie kazi.Siku moja tukaenda Mwanza tukakaa Mwanza Hotel, jumamosi huwa na dinner and dance,kuliliwa na residence band,ambayo mida ya mchana huwa wanafanya mazoezi,nami siku moja nikaenda nikaomba kufanya nao mazoezi,wakanipa gitaa na nilipiga vizuri sana na nikawa rafiki yao sana..Siku moja mpiga solo wao akaugua ghafla akiwa jukwaani na watu wamejaa na mimi na kaka yangu tupo hapo,basi wakaja kuniomba nikapanda jukwaani nikalikung'uta gitaa la solo vizuri hadi saa 8 ndipo nikaenda kulala.Kaka yangu alishangaa kabisa.Siku nyingine ntapa stori nikampigia solo marehemu king kikii
 
Kuchora!
Nikiwa Primary zile kazi za sanaa nilikuwa napelekwa Ofisini nachora picha mbali mbali, picha kadhaa zilibandikwa kwenye ofisi ya walimu na zingine zilipelekwa maktaba ya shule.
Tangia niache shule, na mambo ya uchoraji yaliishia shuleni.
safi sana
 
Mimi ni mchoraji mzuri sana na mbunifu, nimesoma fine art toka o-level hadi A-level nimeshiriki club nyingi sana za uchoraji ! Na mashindano mbalimbali Ila huku ukubwani kipaji hiki sikitumii kabisa !!
Namwomba Mungu akinipa uwezo na Afya mbeleni nataka kuanzisha club ya
ART THERAPY kwa njia ya uchoraji na kupaka rangi na kutengeneza vitu vya ubunifu hii kitu nitaianzisha kwa shule za msingi ambapo nitauomba uongozi wa shule wanitengee siku moja kwa wiki muda ni saa moja nakua na kundi la wanafunzi 30 tu tunapaint , tunachora na kubuni vitu mbali mbali.

Gharama zote zitakua juu yangu vifaa na vitendea kazi vyote kama rangi za aina zote (za maji , za mafuta , pencils , canvas n.k) , Drawing board yan kila kitu nitanunua mimi.
Nitaanza kwa shule moja ila nikikaa njema nitakua nitaongeza ziwe nyingi zaidi.

Kusambaza tone la upendo tu
 
Mm Nina kipaji Cha kutembea umbali mlefu bila kuchoka wastani wa km 10 mfulilizo bila kupumzika lakini hichi kipaji sikitumii.
 
Back
Top Bottom