Unaangalia vitu gani wakati wa kukagua gari jipya au lilotumika ?

Unaangalia vitu gani wakati wa kukagua gari jipya au lilotumika ?

Mwamba1961

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2016
Posts
626
Reaction score
409
Habari zenu,

Aisee ni vitu gani muhimu vya kuangalia wakati nachukua gari jipya au lililotumika?
 
Likishakuwa jipya na kama linauzwa sehemu rasmi basi sizani kama kutakuwa na mambo ya kuangalia,

Ilimradi utakuwa umenunua gari uioendayo.

Lakini kama limeshatumika hapo ndiyo panahitajika umakini mkubwa.

Matharani;

Miongoni mwa vitu vya kuangalia ni pamoja na ;
Mileage: Je gari imeshatembea km ngapi tangu ianze kutumika,
Ijapokuwa hapa wengine huwa wana temper na hizo km wanaweza kuonyesha chache ambazo siyo halisi ili kuvutia wateja.

Cylinder capacity
Utumikaji wa mafuta. Wewe motives zako ni zipi?
Je hali yako ya uchumi ikoje?
Kwa wengine hiyo siyo ishu kwa kuwa hela ya kuweka mafuta itakuwepo siku zote ya kutosha bila mawazo.

Service &maintenace
Baadhi ya magari ukiwa nayo ni kama kulea au kutunza mtu .
Gari inahitaji regular service kila baada ya kutembea km kadhaa kwa mujibu wa mtengenezaji,
Sasa magari mengine service yao huwa bei ghali kuliko aina nyingine za magari.

Fikiria hiyo gari utakapotaka kuiuza je itaweza kuuzika kirahisi?

Siyo wote wanaweza kufikiri hayo .

Je utapenda uitumie muda mrefu au miaka miwili mitatu tu?!

Pia angalia kama gari haijapata breakdown yeyote,

Kama ni kwenye mtandao uone maeneo muhimu ya gari yote kwenye picha.

Pia zingatia bajeti yako pamoja na ushuru

N.k


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari zenu,

Aisee ni vitu gani muhimu vya kuangalia wakati nachukua gari jipya au lililotumika?
Unaponunua gari kuna mambo mengi ya kuangalia....
Uchumi wako, Matumizi yako na Ukubwa wa injini.(cc)....yaani unatakiwa ununue gari ambalo utalimudu mafuta na huduma nyinginezo.

1 .Gari jipya..
Gari jipya hapa tunazungumzia gari ambalo ni 0 km....yaani limetoka kiwandani ukalinunua na wewe ndiyo unakuwa mtumiaji wa kwanza.

Unaponunua gari jipya suala la msingi la kuangalia ni je, unanunua gari hilo kwa matumizi yapi? Biashara?Familia? Au kubeba mizigo? na kadhalika

Lakini pia unaponunua gari jipya unaangalia uchumi wako kwa sababu gari jipya ni hmgharama kubwa sana na ndiyo maana ni watu wachache sana kwenye nchi yetu wanamudu kununua gari jipya.

2. Gari la Mtumba kutoka JAPAN, SINGAPORE, ULAYA au AMERICA.
Magari ya mtumba ndiyo magari yanayoongoza kwa kununuliwa sana hapa nchini kulingana na bei zake kuwa chini.

Mara nyingi watanzania tumezoea mtumba kutoka Japan huko Beforward.......watu wengi wamekuwa wakijidanganya kuwa wameagiza gari jipya kutoka Japan ilihali ADOmeter inasoma mfano km 10,000.
Hili Siyo gari jipya bali ni gari linaloletwa kwenye Mazingira mapya..

Unaponunua mtumba kutoka Japan,Ulaya, Singapore au Marekani....kumbuka hawa wenzetu ni watunzaji na wanazingatia kanuni zote za utunzaji wa gari, hivyo hii hufanya kuwa na uhakika kwa asilimia kubwa kubwa mtumba wa gari unaotaka kuagiza hauna shida sana....

Unaponunua mtumba wa gari suala la msingi la kuzingatia ni Matumizi yako (Je unahitaji gari la matumizi gani.), Ushuru wa TRA ili usije ukaliacha bandarini, Muundo wa gari unaokupendeza, Aina ya gari mf Toyoga, Nissan, Suzuki, Audi,BMW nk., lakini pia unaangalia mazingira utakayokuja kutumia gari lako. Je, utakuwa unaliendesha mjini tu au na huko mashambani na milimani..
Jambo jingine la unaponunua gari la mtumba ni kuangalia Umri wa gari toka lilipotengenezwa japo kuna watu wanapenda magari ya zamani, pia kama unanunua mtumba wa gari angalia gari lenye ADOmeter inyosoma chini ya Km 100,000....japo suala la mile age halina guarantee kwamba gari ni zima.
Kuna mabo mengine unayoweza kuyaangalia kwenye picha za gari husika mfano kama limebondeka mahali watakuwekea picha.

Baada ya kuangalia mambo hayo, unatafuta kampuni unayodhani itakidhi haja yako, kisha unaagiza kupitia wao au wakala wao mfano Beforward, SBT na wengineo wengi..
Mtumba ambao hujatumika bongo, pia unaweza kuupata hapa hapa nyumbani kwenye Yard za kuuza magari..

3. .Gari la mtumba lililotumika nje ya nchi, kisha likatumika hapa Tanzania.

Hili ni gari lilionunuliwa nje ya nchi likiwa mtumba, mbongo kalitumia kisha naye kaamua kuliuza kwa sababu moja au nyingine....
Pengine analiuza ili aongezee pesa anunue lingine, Pengine analiuza alipe mkopo wa benki au ada za watoto au PENGINE ANALIUZA KWA SABABU LINAMSUMBUA NA FUNDI WAKE KAMSHAURI TAFUTA BOYA UMSHIKISHE.

Kununua gari lililotumika bongo ni bahati nasibu (50/50)....Unaweza kula au Ukaliwa..

Unaponunua gari lililotumika bongo unatakiwa uangalie mambo mengi sana kwa sababu hapa ni sawa na kubet..

Kwanza usipende kununua gari lililooshwa injini mchana na wewe ulinunue jioni, pengine kuna sehemu nyingi zinavuja oil hivyo wameosha ili kumhadaa mteja.

Washa injini, itapendeza zaidi kama injini itakuwa imepoa yaani gari halijaendeshwa kwa muda wa masaa sita na kuendelea....hii itasaidia kuona uwakaji wa injini ni wa kulazimisha au inawaka kawaida, je ikishawaka RPM ipo ngapi, na RPM inashuka kwa wakati na kufikia kiwango kinachohitajika..?Je sailesa yake ikoje, ipo rafu au imetulia?Je unapowasha hakuna pipe yoyote inayovuya aidha hewa, maji au oil..?
Je unapowasha moshi wake ukoje, mweupe au wa blue kwa gari za petrol...kama ni mweupe kama mvuke basi gari linaunguza coolant kwenye combustion chamber, kama ni wa blue basi linaunguza oil.
Je inji inatetemeka?Hapa yaweza kuwa misfiring au Mounts zimechoka..

Injini inapokuwa ON, je bado kuna taa za tahadhari zinaendelea kuwaka kwenye dashboard..? Kama zipo je ni zipi?

Kagua sehemu za chini zenye maungo yanayozunguka kuona kama kunavuja grease au oil kwa mfano Boots za CV joints..

Na ukiridhika kununua gari kwa mbongo, liendeshe kwa umakini kwenye barabara mbovu ambayo si lami...hii itakusaidia kusikia kama kuna sehemu zinagonga gonga na kama una utundu wa magari utagundua kuwa milio inayotoka ni major issues au minor issues..

Washa gari sehemu ambayo ni tambarare, kama ni auto weka D kisha achia brake usikanyage mafuta...Gari likiondoka taratibu ni ishara kuwa gear box bado nzima... (hii si guarantee)....likikataa kuondoka mpaka ulazimeshe kwa kukanyaga mafuta, basi gear box imeanza kuchoka.

Endesha gari hilo kwenye high way ili uone uchanganyaji wake, kwenye miinuko ya kawaida jaribu kuona kama lina pooling ya kufikia angalau speed 100.

Kagua ubora wa body, je imerudiwa rangi au haijarudiwa., kama imerudiwa rangi penda kujua ni kwa nini, huenda gari lilipata ajali..

Kaguq mambo mengine madogo madogo mfano AC, Wiper, Power Windows,Power mirror na kadhalika...

###$$$&&&....Endapo umekagua mambo hayo na ukaridhika na ukaamua kununua gari husika, lioeleke garage....Mwaga injini oil weka unayoiamini, badili Spark plugs, badili air filter kama imechoka, badili fuel filter, badili transmission fluid na uweke uliyopendekezwa.....Kwa nini ufanye yote haya..? Ni kwa sababu hujui mtumiaji wa awali alikuwa anafanya service za uhakika au laa..

Mwisho kabisa peleka gari CAR WASH likaogeshwe kuondolewa gundu....pengine gari hilo lilikuwa linatumika kuchepukia na wake za watu...yaani ni guest house...
Au litakase kwa imani yako coz wengine wanazindika magari yao kwa waganga..

Hii ndiyo BONGO...[emoji847][emoji847][emoji847][emoji847]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
gari jipya ni hmgharama kubwa sana na ndiyo maana ni watu wachache sana kwenye nchi yetu wanamudu kununua gari jipya

SIO nchi yetu pekee, hata Uzunguni huko hawanunui gari jipya isipokuwa kwa mpango wa kudunduliza, "car note," za dola mia tatu mia tatu kila mwezi kwa miaka minne, mitano!

Wa kwenda na cash kununua mpya ni wachache mno.... Tena siku hizi hata kununua hawanunui, wanakodi kwa miaka mitatu mine wanarudisha. Nyumba pia wananunua kwa malipo ya miaka 30, hawana chao.

Hakuna mtu Afrika analipia kitu miaka mitano!

TEMBEENI KIFUA MBEREEE
 
Unaponunua gari kuna mambo mengi ya kuangalia....
Uchumi wako, Matumizi yako na Ukubwa wa injini.(cc)....yaani unatakiwa ununue gari ambalo utalimudu mafuta na huduma nyinginezo.

1 .Gari jipya..
Gari jipya hapa tunazungumzia gari ambalo ni 0 km....yaani limetoka kiwandani ukalinunua na wewe ndiyo unakuwa mtumiaji wa kwanza.

Unaponunua gari jipya suala la msingi la kuangalia ni je, unanunua gari hilo kwa matumizi yapi? Biashara?Familia? Au kubeba mizigo? na kadhalika

Lakini pia unaponunua gari jipya unaangalia uchumi wako kwa sababu gari jipya ni hmgharama kubwa sana na ndiyo maana ni watu wachache sana kwenye nchi yetu wanamudu kununua gari jipya.

2. Gari la Mtumba kutoka JAPAN, SINGAPORE, ULAYA au AMERICA.
Magari ya mtumba ndiyo magari yanayoongoza kwa kununuliwa sana hapa nchini kulingana na bei zake kuwa chini.

Mara nyingi watanzania tumezoea mtumba kutoka Japan huko Beforward.......watu wengi wamekuwa wakijidanganya kuwa wameagiza gari jipya kutoka Japan ilihali ADOmeter inasoma mfano km 10,000.
Hili Siyo gari jipya bali ni gari linaloletwa kwenye Mazingira mapya..

Unaponunua mtumba kutoka Japan,Ulaya, Singapore au Marekani....kumbuka hawa wenzetu ni watunzaji na wanazingatia kanuni zote za utunzaji wa gari, hivyo hii hufanya kuwa na uhakika kwa asilimia kubwa kubwa mtumba wa gari unaotaka kuagiza hauna shida sana....

Unaponunua mtumba wa gari suala la msingi la kuzingatia ni Matumizi yako (Je unahitaji gari la matumizi gani.), Ushuru wa TRA ili usije ukaliacha bandarini, Muundo wa gari unaokupendeza, Aina ya gari mf Toyoga, Nissan, Suzuki, Audi,BMW nk., lakini pia unaangalia mazingira utakayokuja kutumia gari lako. Je, utakuwa unaliendesha mjini tu au na huko mashambani na milimani..
Jambo jingine la unaponunua gari la mtumba ni kuangalia Umri wa gari toka lilipotengenezwa japo kuna watu wanapenda magari ya zamani, pia kama unanunua mtumba wa gari angalia gari lenye ADOmeter inyosoma chini ya Km 100,000....japo suala la mile age halina guarantee kwamba gari ni zima.
Kuna mabo mengine unayoweza kuyaangalia kwenye picha za gari husika mfano kama limebondeka mahali watakuwekea picha.

Baada ya kuangalia mambo hayo, unatafuta kampuni unayodhani itakidhi haja yako, kisha unaagiza kupitia wao au wakala wao mfano Beforward, SBT na wengineo wengi..
Mtumba ambao hujatumika bongo, pia unaweza kuupata hapa hapa nyumbani kwenye Yard za kuuza magari..

3. .Gari la mtumba lililotumika nje ya nchi, kisha likatumika hapa Tanzania.

Hili ni gari lilionunuliwa nje ya nchi likiwa mtumba, mbongo kalitumia kisha naye kaamua kuliuza kwa sababu moja au nyingine....
Pengine analiuza ili aongezee pesa anunue lingine, Pengine analiuza alipe mkopo wa benki au ada za watoto au PENGINE ANALIUZA KWA SABABU LINAMSUMBUA NA FUNDI WAKE KAMSHAURI TAFUTA BOYA UMSHIKISHE.

Kununua gari lililotumika bongo ni bahati nasibu (50/50)....Unaweza kula au Ukaliwa..

Unaponunua gari lililotumika bongo unatakiwa uangalie mambo mengi sana kwa sababu hapa ni sawa na kubet..

Kwanza usipende kununua gari lililooshwa injini mchana na wewe ulinunue jioni, pengine kuna sehemu nyingi zinavuja oil hivyo wameosha ili kumhadaa mteja.

Washa injini, itapendeza zaidi kama injini itakuwa imepoa yaani gari halijaendeshwa kwa muda wa masaa sita na kuendelea....hii itasaidia kuona uwakaji wa injini ni wa kulazimisha au inawaka kawaida, je ikishawaka RPM ipo ngapi, na RPM inashuka kwa wakati na kufikia kiwango kinachohitajika..?Je sailesa yake ikoje, ipo rafu au imetulia?Je unapowasha hakuna pipe yoyote inayovuya aidha hewa, maji au oil..?
Je unapowasha moshi wake ukoje, mweupe au wa blue kwa gari za petrol...kama ni mweupe kama mvuke basi gari linaunguza coolant kwenye combustion chamber, kama ni wa blue basi linaunguza oil.
Je inji inatetemeka?Hapa yaweza kuwa misfiring au Mounts zimechoka..

Injini inapokuwa ON, je bado kuna taa za tahadhari zinaendelea kuwaka kwenye dashboard..? Kama zipo je ni zipi?

Kagua sehemu za chini zenye maungo yanayozunguka kuona kama kunavuja grease au oil kwa mfano Boots za CV joints..

Na ukiridhika kununua gari kwa mbongo, liendeshe kwa umakini kwenye barabara mbovu ambayo si lami...hii itakusaidia kusikia kama kuna sehemu zinagonga gonga na kama una utundu wa magari utagundua kuwa milio inayotoka ni major issues au minor issues..

Washa gari sehemu ambayo ni tambarare, kama ni auto weka D kisha achia brake usikanyage mafuta...Gari likiondoka taratibu ni ishara kuwa gear box bado nzima... (hii si guarantee)....likikataa kuondoka mpaka ulazimeshe kwa kukanyaga mafuta, basi gear box imeanza kuchoka.

Endesha gari hilo kwenye high way ili uone uchanganyaji wake, kwenye miinuko ya kawaida jaribu kuona kama lina pooling ya kufikia angalau speed 100.

Kagua ubora wa body, je imerudiwa rangi au haijarudiwa., kama imerudiwa rangi penda kujua ni kwa nini, huenda gari lilipata ajali..

Kaguq mambo mengine madogo madogo mfano AC, Wiper, Power Windows,Power mirror na kadhalika...

###$$$&&&....Endapo umekagua mambo hayo na ukaridhika na ukaamua kununua gari husika, lioeleke garage....Mwaga injini oil weka unayoiamini, badili Spark plugs, badili air filter kama imechoka, badili fuel filter, badili transmission fluid na uweke uliyopendekezwa.....Kwa nini ufanye yote haya..? Ni kwa sababu hujui mtumiaji wa awali alikuwa anafanya service za uhakika au laa..

Mwisho kabisa peleka gari CAR WASH likaogeshwe kuondolewa gundu....pengine gari hilo lilikuwa linatumika kuchepukia na wake za watu...yaani ni guest house...
Au litakase kwa imani yako coz wengine wanazindika magari yao kwa waganga..

Hii ndiyo BONGO...[emoji847][emoji847][emoji847][emoji847]


Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa umetoa darasa zuri sana washindwe wao.
 
Angalia afya ya vitu vinavyosuguana, vitakavyo gharimu muda na pesa kuimarisha. Hapa Injini, gia boksi na bushes vina husika.

Injini
Angalia kwanza ubora wa injini, pima oil kwenye "dipstick" uone kama inachembe chembe za vyuma. Iwashe gari, sikiliza kama ina mlio wa kugonga (rod knock sound) kama haina angalia tena oil kama ni nzito. Wauzaji wa magari mabovu huwa wanaweka "thick oil" ili kupungunza makelele ya rod knock.

kama utaweza fanya "leak down test" au ikishindikana fanya "compression test" kujua kama injini bado nzuri. Hapa utaweza kujua kama injini ina "leak" sehemu, hii itakusaidia kujua kama injini hiyo inakula mafuta na kama bado ina nguvu.

Gearbox
Endesha ukitilia maanani jinsi gari inavyobadilisha gia, kama inapiga kelele au inakuwa ngumu kubadilisha gia juwa kuwa kuna tatizo kwenye transmission/gearbox.

Suspension
Kwenye suspension angalia kama bushing bado ziko poa, hii ni pamoja na "engine mount", "control arm" (wishbone) na tie rods (CV joints). Angalia hizi kwaajili ya usalama wako. Kama control arms zikiharibika tairi linaweza chomoka likiingia kwenye shimo hasa ukiwa kwenye mwendo kasi. Kupona hapo ni Mola tuu anajuwa.

Kwa kuongezea "run some codes" kupitia OBDII scanner, kujuwa kama kunatatizo. Hii inaweza isiwe njia sahihi sana kwa kuwa muuzaji wa gari anaweza kuziondoa codes na usijuwe kama gari inakasoro.
 
Mileage
Engine condition
Body condition
Gearbox condition
Hivyo ndio vya msingi
Habari zenu,

Aisee ni vitu gani muhimu vya kuangalia wakati nachukua gari jipya au lililotumika?

Jr[emoji769]
 
Bora nidundulize niagize mtumba kutoka nje au ninunue mtumba showroom hapa bongo kuliko kumvua m-bongo mwenzangu...haya mambo unaweza kufa kwa pb

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Darsa swafi,ila kuna mwamba alinunua gari mpya kabisa 0 km.sasa akalepeka tena gereji nikamuuliza kwa nini?akanambia ameenda kitoa thermostat,


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kununua gari used bongo inabidi ulikague kama wiki hivi na uliendeshe high way na kwenye foleni. Mi nlinunua cami mpaka sasa 1M ishanitoka matengenezo. Engine kumbe ilibadilishwa iliyowekwa haifungwa vizuri so nimeifanyia matengenezo kibao hadi ikaa sawa
Bora nidundulize niagize mtumba kutoka nje au ninunue mtumba showroom hapa bongo kuliko kumvua m-bongo mwenzangu...haya mambo unaweza kufa kwa pb

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu uzi safii sana... Kuhusu suala la kurudiwa rangi naliogopa...

Hivii Tunavoeka & Inspection Wakati Wa Kuagiza BeForward Ni Kweli Wanalikagua Gari Au Ni Changa La Macho???


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom