Victor Mlaki
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 4,151
- 4,277
Naandika kwa masikitiko makubwa sana juu ya uchuro unaofanywa na watu wanaojiita manabii katika Nchi ya Tanzania. Bila shaka nimefuatilia uchuro mwingi sana jambo ambalo nimeona siyo vyema kuacha kuandika ili kama wapo humu waelewe tumeshawagundua na jambo la msingi zaidi waache uchuro ili unabii wa kweli ufanye kazi yake.
Kumekuwa na utitiri wa manabii uchuro kuliko manabii halisi katika Nchi ya Tanzania jambo ambalo likiachiliwa na kuendelea kushamiri yatajirudia yale yaliyowapata wafuasi wa Kibwetere. Hivyo,basi kabla hawa wachuraji hawajafika mbali zaidi ni zikachukuliwa hatua za mapema za tahadhari "proactive measures".
Viongozi wakubwa wa kisiasa wamekuwa wakichuriwa vifo na manabii uchuro kila uchao. Unabii umekuwa ni wa kutabiri juu ya mabaya yatakayoyokea kuliko mazuri. Swali la kujiuliza kimyakimya ni je, hawa manabii wao huoneshwa mabaya tu na siyo mazuri?
Kuna nabii mmoja nimefuatilia maelezo yake kwa karibu leo nikacheka sana kwa sababu ni usanii mtupu anafanya halafu watu wanamtumia pesa na kumuita MTUMISHI wa Mungu. Kibaya zaidi anajipa sifa kama kawaida yao ilivyo na kusema ana sifa nabii bora katika Tanzania kama alivyo Mtu wa Mungu T.B Joshua. Ametabiri kuwa ndani ya mwezi huu wa tatu na ukipita basi wa tisa kuna Kiongozi mwingine mmoja ambaye akisimama ana alama mwilini tofauti na wenzake na jina lake ni namba tano yupo kwenye hali ngumu tumuombee sana na akaahidi ana package nyingine ataisema siku nyingine. Hawa jamaa wanacheza sana na mashaka ya watu juu ya jambo na kutumia mwanya huo kama fursa ya kuongeza hofu zaidi kwa watu ili kujinufaisha wao.
Hawa jamaa wanafahamika sana na kuna watu wameshatiwa sumu akilini na hawa wasanii ndiyo wanaowafanya kuwa na kizuri cha kuendelea kutumia mashaka na tashwishwi za watu juu ya wakati ujao kama njia ya wao kuzidisha hofu na ujinufaisha.
Hawa watu wanapaswa kulipa kodi kutokana na biashara wanyoifanya ili angalau kila fursa inayopatikana nchini ilifaidishe Taifa hili. Kama wafanyabiashara wadogo wanaotafuta shilingi Mia Mia kila siku wanaolipa kodi hawa wanaobumbabumba mambo na kutumia milioni moja, mbili n.k nao walipishwe kodi ili mapato ya Taifa hili yatufaidishe wote.
Nina uhakika hawa manabii uchuro wakilipishwa kodi litakuwa ni jambo zuri sana kwa sababu watakuwa wamempa pia Kaisari haki yake kama wanavyojibainisha kuagizwa na Mungu.
Kumekuwa na utitiri wa manabii uchuro kuliko manabii halisi katika Nchi ya Tanzania jambo ambalo likiachiliwa na kuendelea kushamiri yatajirudia yale yaliyowapata wafuasi wa Kibwetere. Hivyo,basi kabla hawa wachuraji hawajafika mbali zaidi ni zikachukuliwa hatua za mapema za tahadhari "proactive measures".
Viongozi wakubwa wa kisiasa wamekuwa wakichuriwa vifo na manabii uchuro kila uchao. Unabii umekuwa ni wa kutabiri juu ya mabaya yatakayoyokea kuliko mazuri. Swali la kujiuliza kimyakimya ni je, hawa manabii wao huoneshwa mabaya tu na siyo mazuri?
Kuna nabii mmoja nimefuatilia maelezo yake kwa karibu leo nikacheka sana kwa sababu ni usanii mtupu anafanya halafu watu wanamtumia pesa na kumuita MTUMISHI wa Mungu. Kibaya zaidi anajipa sifa kama kawaida yao ilivyo na kusema ana sifa nabii bora katika Tanzania kama alivyo Mtu wa Mungu T.B Joshua. Ametabiri kuwa ndani ya mwezi huu wa tatu na ukipita basi wa tisa kuna Kiongozi mwingine mmoja ambaye akisimama ana alama mwilini tofauti na wenzake na jina lake ni namba tano yupo kwenye hali ngumu tumuombee sana na akaahidi ana package nyingine ataisema siku nyingine. Hawa jamaa wanacheza sana na mashaka ya watu juu ya jambo na kutumia mwanya huo kama fursa ya kuongeza hofu zaidi kwa watu ili kujinufaisha wao.
Hawa jamaa wanafahamika sana na kuna watu wameshatiwa sumu akilini na hawa wasanii ndiyo wanaowafanya kuwa na kizuri cha kuendelea kutumia mashaka na tashwishwi za watu juu ya wakati ujao kama njia ya wao kuzidisha hofu na ujinufaisha.
Hawa watu wanapaswa kulipa kodi kutokana na biashara wanyoifanya ili angalau kila fursa inayopatikana nchini ilifaidishe Taifa hili. Kama wafanyabiashara wadogo wanaotafuta shilingi Mia Mia kila siku wanaolipa kodi hawa wanaobumbabumba mambo na kutumia milioni moja, mbili n.k nao walipishwe kodi ili mapato ya Taifa hili yatufaidishe wote.
Nina uhakika hawa manabii uchuro wakilipishwa kodi litakuwa ni jambo zuri sana kwa sababu watakuwa wamempa pia Kaisari haki yake kama wanavyojibainisha kuagizwa na Mungu.