Unafiki wa Watanzania katika sakata la Mwakinyo kumuomba msamaha na Rashid Matumla

je parle

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2018
Posts
2,022
Reaction score
3,919
Siku mbili tatu kuliibuka mijadala mtandaoni kama Instagram FB Twitter na mitaani kuhusu kijana Mwakinyo kumwambia Matumla kuwa hana alipofika kutokana na kile alichokisema kama mchambuzi siku ya pambano kuwa Mwakinyo anatakiwa kutafuta kocha mwingine

Maana kuwa hakuwa na mbinu za kumpigia Tinampay na badala yake alikuwa akilalia kamba tu. Ni kitendo kilichomuhuzinisha Mwakinyo na kusema aliyo yasema.

Sasa suala linakuja wabongo wengi haswa haswa wenye kumiliki vifollowers walipiga kelele kwamba Mwakinyo hana heshima na badala yake anatakiwa kuomba radhi.

Sasa bwana leo wamekutanishwa Azam TV na kuombana radhi lakini chakushangaza wale walipiga firimbi na zumari waliokuwa wanataka Mwakinyo aombe radhi wametulia tuli kama hawaoni kilichotokea kwamba watu wameombana msamaha.

Hiii inaonesha ni kwamba watanzania waliowengi haswa wenye followers ni wepesi Sana katika kuchafua watu kuliko watu kuliko kuwasafisha

Watanzania hawapendi mtu awe maarufu kuliko wao awe na kipato kuliko wao hii ni chuki na roho mbaya Kwa baadhi ya watanzania haswa wanaomiliki followers wa kuchovya
 
Duh kwani Mwakinyo alikuwa halalii kamba siku ile?
Kulalia kamba ni mbinu pia.
Pambano lake alilompiga Sam Eggington alikuwa analalia kamba vile vile.
Na wapo mabondia wengi sana wametumia hiyo mbinu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…