Unaifahamu siki(Vinegar) aliyonywesha Yesu?

Unaifahamu siki(Vinegar) aliyonywesha Yesu?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Siki ni nini? Siki hutokana na pombe. Ili kutengeneza pombe fangasi hubadili sukari(Glucose) kuwa pombe(Ethanol). Sasa kuna bakteria wanaweza kuibadili hiyo ethanol kuwa asidi(Acetic acid), na hiyo ndiyo siki. Kiasili siki inatoka kwenye pombe. Kwa wakazi wa nyanda za juu kusini watakuwa wanafahamu ulanzi unaoitwa mkangafu. Ni ulanzi uliokaa muda mrefu na huwa mkali sana, wengi wanadhani kuwa ndiyo unalewesha sana. Si kweli, ulanzi ule pombe yake inakuwa imebadilika kuwa acetic acid. Unakuwa unakunywa maasidi yasiyolewesha.

Ukichukua pombe, kama wine na ukaiacha kwa muda mrefu utaona bakteria hawa wameanza kujijenga. Juu ya hiyo pombe hutengeneza utando mzito unaofanana na maini mabichi. Huo huwa mchanganyiko wa bakteria wa kutengeneza siki. unaitwa Mother of Vinegar. Hata juisi ukiiacha kwa muda mrefu utaona inatengeneza pombe na kisha kuunda huo utando baada ya bakteria kuanza kutengeneza siki.

Siki inatumika sana kwenye msosi. Ni kama limao au ndimu kwenye chakula. Pia kwa sababu ni asidi, inafaa sana kusafishia vitu. Inang'arisha sana. Pia wengine wameitumia kama dawa na pengine kutesea watu kama walivyofanya kwa Yesu. Wale waliomtesa walizamisha kitambaa kwenye siki na kumnyooshea anywe.

Mother of vinegar(Mama siki) akiwa ametolewa kwenye vinegar.
Apple-Cider-Vinegar-Mother-3.jpg

FDVO82ZZHIEXCFKWS0.jpg
 
Acha uongo wewe, ngano za kale zinatuambia mtu mzima alinywesha sifongo.
Unaijua sifongo?
 
Aliyekwambia mtu hunywa ulanzi mkangafu akidhani utamlewesha ni nani?

Kwa taarifa yako watu hunywa mkangafu kwakuwa huwa hauleweshi kwani unakuwa umeshakufa
 
Watoto wa siku hizi akisha google basi ameshamaliza kila kitu, wewe umewahi kunywa mkangafu wewe
 
Ila huyo Yesu inaonekna aliwachachafya haswa ndo maana walipomkamata walimpa tocha ambayo hadi leo ukiitafakari inatisha.
 
Sifongo ni neno la kiswahili likimaanisha sponge. Walichukua sponge wakaichovya kwenye siki na kumnywesha. So usifikiri wanavyosema alinyweshwa siki na sifongo basi sifongo ni kinywaji🙂
Kaja speed kumbe hajui hata sifongo ni nini? [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom