Unajua tofauti Toyota Crown Athelete na Toyota Crown Royal na toyota crown majesta

Unajua tofauti Toyota Crown Athelete na Toyota Crown Royal na toyota crown majesta

dengue f

Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
18
Reaction score
47
.

NAJUAA wengi sana huvitiwa sana magari haya aina ya crown na hata bei zake sio rahisi ki hivyo, na kwa ushauri wangu usinunue crown ya bei rahisi utakuja kulia , hilo nakukuhakikishia , ni gari yenye teknolojia juu kidogo

Na sio sisi tu Wanachato tuno penda hizi CROWN , hata wajapan wenyewe kwao ni gari yenye hadhi yake

Mnamo 9 APRIL 2011 chini ya JAPAN NEW CAR ASSESSMENT PROGRAM (JNCAP) walitoa Awards za juu yenye nyota 5 ,kwa magari haya kati magari aina 40 yaliyo jaribiwa,

Na mwaka 2014 walitoa awards ingine ya Grand prix kuwa magari yaliyo ongoza kwa usalama endapo ikitokea ajali , jaribu kutafuta Taasisi hii iitwayo JNCAP kujua inavofanya kazi.

Haya turudi kwenye Mada ,
je kuna tofauti kati ya CROWN ATHLETE, CROWN ROYAL NA CROWN MAJESTA?

NI kweli kuna tofauti kubwa tu,katk magari haya, hemu tuanze na

CROWN ROYAL
Gari ni gari luxury kidogo yenye mbwembe nyingi sna, sisi tuna ziita mult optional, or full optional, gari hii ina Air bags nying zaid kama 7 hivi ndani, na dash board yake ina curtains tofauti kidogo, vilevile gari hii ina mziki ulio chujwa zaidi,

Upande wa body gari je?

gari hii tofauti kidogo ni ndogo kidogo kwenye widht, hupungua kidogo kwenye bampa zake , taa zake tofauti , taa zake ni mfumo wa AUDI ,tyres ni size 16.

Upande wa INJINI je?
gari hizi nyingi zina injini kubwa kidogo nyingi ni cc 3000, ila zipo zenye injini 2.6
japokuwa zote ni V6 na nyini ni 3GR na chache 4GR.

Upande wa Bei je ?
Gari hizi za miaka 2004 mpk 2007 bei zake ni chini kulinganisha na zingine, demand zake ni ndogo sana kutokana na wengi kuchagua vitu wavipendavyo km cc na muonekano

Toyota CROWN ATHLETE
Hizi ndio wanachato wengi sna huvutiwa nazo,
muonekano wa ndani hautofatiani sana na Toyota crown Royal , japokuwa zenyewe zina Air bags 4
seats ni sawa na tu na Royal

Upande wa body je
Hizi kidogo ndipo zilipo shinda na kupendwa , eneo hili la muonekano wa body limeifanya ATHLETE Kuwa kipenzi cha wanachato, ATHLETE ina body kit kuanzia kwenye bumper zote,
Taa zake ni mfumo wa Benz, tyre zake ni size 17 panga 5, show yake mbele gril zake zimekaa kisport kidogo kuliko zingine

Upande wa Injini Je
Hili ndo eneo lingine limefanya crown Athlete kuwa chaguo la wengi, nyini ni cc 2.5 labda zenye GRS 181,182,183 hizi ndo zenye mi cc kubwa mpk 3000 na 4WD Juu.

Upande wa bei je
Gari hizi ni bei kidogo kwa sababu ya demand kubwa na RANGI nyeusi ndio yenye bei zaid kuliko nyingine, silver ndo zenye bei chini.

CROWN MAJESTA
Hizi siku zote tofauti kwa kila kitu na zote ni V8 , cc mpk 4.5 baaddi za injini zake ni 2UR ,na chache sana kama hamna kukuta 3GR

Na Bei yake kidogo ni juu, Hizi ni za matajiri kidogo

Mwenye kuelewa zaidi karibu ujazilizie

N.B Jamani nashukuru kwa sapoti yenu ila napata upinzani mkali sana messenger kuna madalali wa magari wananitukana sana .... Nafikiria kama kuacha maana nawaharibia dili zao za kuwaelimisha watu magari na kiwa na elimu ya magari
From . J maduhu
image_search_1586445406031.jpg
image_search_1586445203349.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi ndinga mtaani tunaziita jini mmbwia mafuta, kama kipato chako ni cha kudunduliza achana na huu mtambo, utaishia kuupaki na na pia ni ndoa ya kikarismatiki, kama unauwezo wa laki atleast kwa wiki kwa ajiri ya wese ni ndinga kali hasa kubebea mabebez akiingia kwenye ndinga hatoki
 
Hzi ndinga mtaani tunaziita jini mmbwia mafuta,kama kipato chako ni cha kudunduliza achana na huu mtambo, utaishia kuupaki na na pia ni ndoa ya kikarismatiki, kama unauwezo wa laki atleast kwa wiki kwa ajiri ya wese ni ndinga kali hasa kubebea mabebez akiingia kwenye ndinga hatoki

Akiingia tuu chupi imeshalowa
 
Hzi ndinga mtaani tunaziita jini mmbwia mafuta,kama kipato chako ni cha kudunduliza achana na huu mtambo, utaishia kuupaki na na pia ni ndoa ya kikarismatiki, kama unauwezo wa laki atleast kwa wiki kwa ajiri ya wese ni ndinga kali hasa kubebea mabebez akiingia kwenye ndinga hatoki
Unamiliki au ulishawai kumiliki crown au ndio zile story za kuambiwa tu inakula mafuta. Lazima tukubaliane hakuna gari inayokula maandazi ili itembee, crown inatumia mafuta kawaida sna kulingana na ukubwa wa engine yake
 
Hzi ndinga mtaani tunaziita jini mmbwia mafuta,kama kipato chako ni cha kudunduliza achana na huu mtambo, utaishia kuupaki na na pia ni ndoa ya kikarismatiki, kama unauwezo wa laki atleast kwa wiki kwa ajiri ya wese ni ndinga kali hasa kubebea mabebez akiingia kwenye ndinga hatoki
Kumbe mafuta ya laki tu?kwa wiki?....mbona rahisi ,so 500k kwa mwezi si mbaya
 
Habari zenu wakun!

Naomba kujua tofauti zilizopo kati ya Toyota Crown Athlete dhidi ya Toyota crown Royal Salon! Masuala ya uimara stability barabarani, speed, specifications nk japo zinaonekana ni zenye kufanana. Tofanti nizo ziwe ni general pasina kujali toleo gami japo ziwe za matoleo ya miaka ya karibuni.

(Picha zaja)
 
Thread imeandikwa kikawaida mno haitoshi kudai madalali wanatukana.
 
Back
Top Bottom