Jamani kuna mtu wakati naongea naye amenishtua kidogo pale aliponambia kwamba; anashangaa kila akimaliza kula anahisi kama hajashiba. Kiukweli binafsi sijawahi kusikia kitu cha aina hiyo, sasa nikaona niwaletee hapa wadau pengine kuna mtu ana experience au umahili wa jambo hili ambalo ningependa kujua kama ni ugonjwa au kitu kingine.
Ikibidi kama ni ugonjwa ni:-
1. Aina gani ya ugonjwa
2. Sababu
3. Tiba
Wataalamu mkuje tafadhali!